Mtangazaji B Dozen amvalisha pete mpenzi wake wa miaka mingi

Halafu shida nyingine ni kwamba unakuta mdada analilia Pete tu kila wakati ni kulia lia huku mwanaume hajajipanga kumuweka ndani basi wanaamua kuwavalisha halafu mwanaume anapita hivi
Hata ndoa bado pia sio kila kitu. Unaweza ukaolewa na bado ikawa unatamani hata usingeolewa. Ndoa zina mengi sana.
Na kuolewa pia sio kwamba ndo umemaliza safari, Kushindwana Kupo, Michepuko ipo na Talaka pia zipo.
Hivo basi usililie Pete ya Ndoa saaaana.
Bora uvae hiyo Pete ya Uchumba kwa furaha kwa Miaka Sita, kuliko kuvaa Pete ya Ndoa yenye Majuto Kibao ila mnaogopa kuachana sababu mnahofia watu.
My point is, Pete ya Ndoa sio suluhisho na Sio kila kitu. Ndoa zina mengi.
Usiingie kwenye Ndoa kama Fashion vile kisa Rafiki zako Wengine wameingia.
KUNA TOFAUTI KUBWA KATI YA "HARUSI(sherehe)" NA "NDOA"...
Ndoa nzito, Maana Kuunganisha FAMILIA MBILI sio mchezo, maana kuna vibweka vya Ndugu wa pande zote MBILI (mashemeji, Mama Mkwe, Baba Mkwe etc.) Ukimpelekea ZAWADI Mama Yako Mzazi basi ujipange pia kupeleka ZAWADI nyingne UKWENI nako.
Ukimlipia Ada ya Shule mdogo wako, heheh! Jiandae kuna Ada nyingne ya Ukweni inakusubiri.
That's why, You need to take time ndefu kwanza kabla ya Uchumba na Ndoa ili myajenge MJUE PESA ZENU MTA-HANDLE VIPI, NDUGU etc.
Otherwise vitu vidogo vidogo kama hivyo huwa taratiiiibu vnabomoa.
TRUST ME, Uhusiano wa U-BOYFRIEND na U-GIRLFRIEND NI MRAHISI SANA KULIKO wa U-HUSBAND na U-WIFE.
Ndo maana Msitulaumu sie Wanaume tukifanya Uchumba miaka SITA 😀😀
 
Kwahiyo inabidi kuwanyima eeh
Ukitunyima UTAMU basi hupati Mtu. Maana hakuna anayetaka kuuziwa Mbuzi kwenye Gunia.
Zama hizi kila mtu anataka aonje kwanza halafu baada ya kuonja, ndo unapima sasa "Je ninunue au nisinunue.?" 😀😀
 
Wamekuwa wote kwa muda mrefu na bado hajapata ujauzito. Hata akioelewa situation itakuwa ni hii maana huwezi sema hawashiriki. Lulu mwenyewe alishasema anatamani kupata mtoto.
Huyo mchumba labda ana wasiwasi juu ya hilo.
😀😀 Zipo njia nyingi sana za kuzuia Mimba. Unaishi kama upo karne ya 6 bana. Amka aisee ni karne ya 21.
Usi-force kupata mtoto kama hauko tayari
 
Cheti cha church ili hata 4shizo akidanja urithi anaumiliki wote
E Media (TV & Radio) ni kampuni ya Familia ya akina Majizo (Ciza's Family).. Angalia hata ripoti za TCRA utaona mgawanyo wa Shares (hisa) za Umiliki Kampuni yao Ulivyo.
Hivo Madam Lulu hawezi kumiliki urithi wote.
Halafu pia Kwenye Sheria, Kwa Wanandoa kabla ya kuingia ndoani hasa Wanandoa kwenye Mali Nyingi (Utajiri) huwa kuna sheria ya PRENUPTIAL AGREEMENT ila hii kusaini ni ukipenda mwenyewe ili kuepusha zengwe la Mali baadae.
 
Wamekuwa wote kwa muda mrefu na bado hajapata ujauzito. Hata akioelewa situation itakuwa ni hii maana huwezi sema hawashiriki. Lulu mwenyewe alishasema anatamani kupata mtoto.
Huyo mchumba labda ana wasiwasi juu ya hilo.
Mmmh hayo ni mambo nyeti sana mkuu, umejuaje lulu hataki kubeba mimba bila ndoa?
 
Mmmh hayo ni mambo nyeti sana mkuu, umejuaje lulu hataki kubeba mimba bila ndoa?
Sio kwamba hataki ila bado hajabahatika kupata. Sasa mwanaume lazima taa iwake, hii inaweza kuwa sababu ya kumfanya avute muda. Mbona Majizo ana mtoto kwa Hamisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom