Mtangazaji aogopa kutamka 'Serunkuma'

Opaque

JF-Expert Member
Oct 24, 2008
1,359
717
Katika hali isiyo ya kawaida, mtangazaji Christina Mbezi alifanya kila awezalo kukwepa kutamka jina la SSerunkuma, mshambuliaji wa Gor Mahia raia wa Uganda aliyetua nchini kufanya mazungumzo na klabu ya Simba. Mtangazaji huyo alikuwa anakwepa kutamka neno hilo wakati akisoma yaliyoandikwa magazetini katika kipindi cha Tuongee Magazetini. Mfano, alipotakiwa kusema 'SSerunkuma atua Dar', yeye alisema 'atua Dar'. Aliendelea kulikwepa neno hilo hata wakati akiisoma habari kwa undani na pia hata alipokutana na jina hilo katika magazeti mengine.

Hii itakuwa ni changamoto kwa waswahili iwapo mshambuliaji huyo atafanikiwa kusajiliwa na Simba!
 
si ataitwa kwa kifupi chake tu . Sseru .. hakuna haja ya watu kuona ugumu wowote

Hata wakiita jina lake lote wala sioni shida yeyote
 
mtangazaji ana fikra chafu...na hili ndo tatizo la watanzania wengi kwa sasa. mtu anshindwa kusema tigo kwa kuwa tayari watu wenye fikra ovu wamehusisha na mambo yao maouvu. mi sioni kama ni mwenye nia safi ashindwe kutamka hilo jina. kuna kampuni ya vifaa vya michezo ya FILA mtangazaji angekwepa kutamka jina hilo ikiwa ndo wadhamini wa jambo husika? aache unafiki.
 
Hawa simba kwa kutuletea majina ya ajabu wako vzr!jina la liboro bado halijaisha wameona haitoshi wanatuletea serunkuma!
 
unajua tatizo la hilo jina, unaanza na sauti ya juu, unashuka ukifiika ru.. afu baada ya hapo sauti unatakiwa upande, sasa ukipanda hilo neno la mbele linasikika kwa sauti zaidi, hahaha! mtangazaji mwenye aibu
 
Watangazaji wengi wa kike ni watupu katika kutamka majina ya wachezaji wa nje...
 
Alianza kumambili keita, mara libolo nao wakatekeleza majukumu ya libolo, na sasa sserunkuma. Tusubiri mwakani.
 
Kuna mtangazaji mwingine nilishamsikia akisema "Ukistaajabu ya Musa utayaona ya yule jamaa ambaye siwezi kumtamka redioni" Na huyo mtangazaji alikuwa anaitwa Mande.
 
Katika hali isiyo ya kawaida, mtangazaji Christina Mbezi alifanya kila awezalo kukwepa kutamka jina la SSerunkuma, mshambuliaji wa Gor Mahia raia wa Uganda aliyetua nchini kufanya mazungumzo na klabu ya Simba. Mtangazaji huyo alikuwa anakwepa kutamka neno hilo wakati akisoma yaliyoandikwa magazetini katika kipindi cha Tuongee Magazetini. Mfano, alipotakiwa kusema 'SSerunkuma atua Dar', yeye alisema 'atua Dar'. Aliendelea kulikwepa neno hilo hata wakati akiisoma habari kwa undani na pia hata alipokutana na jina hilo katika magazeti mengine.

Hii itakuwa ni changamoto kwa waswahili iwapo mshambuliaji huyo atafanikiwa kusajiliwa na Simba!

Sasa Aliogopaje Kuitaja Kitu Ambayo Hata Yeye Mwenyewe Anayo?
 
Back
Top Bottom