Transistor
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 970
- 1,461
Kutokana na changamoto za umeme
kukatika katika au baadhi ya maeneo kutokuwa na umeme
Nimebuni mashine hii ambayo itamwezesha kinyozi kuendelea na shughuri yake ya kunyoa bila kujali umememe upo au haupo.
Mashine hii inatumia nguvu ya jua ambayo inahifadhi umeme katika bank ya umeme iliyojengewa ndani yake,umeme huu unao hifadhiwa baada ya kuvunwa kutoka katika jua hukuzwa na mfumo uliopo ndani ya mashine hii na kutumika katika kuendesha mashine ya kunyolea.
Mashine hii ina uwezo wa kuzitanua na kuzificha panel zake za kuvuna nguvu ya jua hii inasaidia katika usafirishaji wa mashine na utunzaji.
Kupitia mashine hii kinyozi anaweza kwenda katika maeneo yasio na umeme mfano vijiji vya mbali kwa kubeba mashine hii na kwenda kufanya kazi yake ya kunyoa bila shida.Akimaliza konyoa anabeba mashine yake anarudi.
Pia kwa ambao wapo mjini wanaweza kutumia mashine hii kama mbadala wa jenerator kwasababu ukisha kuwa na mashine kama hii hauhitaji tena kununua mafuta kama jenerator.Wakati wote utaimumia bil ghrama ya ziada wala makelele.Nani rahisi kuihifadhi.
MFUMO WA ZIADA WA KIUCHUMI KATIKA MASHINE HII.
Kwa wajasiliamali wanaweza wakamiliki mashine hii na kuwapa vijana kwenda kunyoa sehemu mbalimbali hasa vijijini.
Mashine hizi zimefungwa mfumo wa mita (kama luku),ambayo inapima kiwango cha matumizi.
Hivyo unaweza ukaamua kukodisha mashine yako kwa watu na ukawa unawachaji kulingana na kiasi cha UNIT wanazo kuwa wametumia kwa mwezi.
Kifaa hiki kinaweza kutumika kama mbadala wa generator au kikatumika kama mashine ambayo kinyozi anatembea nayo hasa maeneo ya vijijini na kunyoa watu hasa maeneo ya minada,shule vilabu n.k
Kwa maelezo zaidi tazama video au wasiliana na mbunifu
0629068815
Transistor