Wakuu,
Hakuna atakayebisha kwamba upepo wa kisiasa Tanzania umebadilika kabisa, harufu ya mageuzi imetanda, CCM imepotenza nguzo muhimu karibia zote na imebakiza hii ya KINA MAMA.
Siku ambayo mama zetu watastukia kwamba CCM sasa hawana jipya basi ndiyo itakuwa mwisho wake, wengi tunajua mama zetu ni wagumu sana kubadili uelekeo kwa ghafla, ingawa wao ndiyo wanapata shida kubwa sana hasa vijijini - lakini ndiyo wanakuwa kwa kwanza kushabikia CCM na kuvaaa khanga za chagua kikwete ambazo wengi huzitunza vizuri sana na kuzivaa wakati wa mikutano ya CCM.
Nachowasikitika CCM ni kupoteza nguzo ya VIJANA, vijana wengi kama si wote wapo CDM, unapopoteza nguzo hii ujue chama chako kinaingia shimoni, na kibaya zaidi CCM imekosa watu makini wa kujaribu kurudisha imani ya wananchi hasa vijana na hii ni hatari kubwa sana kwao.
CCM wanapofikia mahala pa kusema ushindi ni ushindi tu - hata wa kura moja zaidi ni ushindi - yaani hapo ujue kwamba sasa chama kimekosa mvuto na kinakufa, Chama kinapoanza kuangukia wazee wastaafu wakaokoe jahazi kwenye kampeni ina maana hakina vijana makini wa kukisemea mbele ya jamii na wakakubalika.
Chama kila kinapoenda kwenye mikutano yake ya kampeni lazima kiende na muziki na maigizo kuvuta wananchi- hapa lazima ufikiri mara mbili kwamba hoja zao hazina ushawishi kwa walio wengi kwa sasa. ndugu zangu hadi leo hatujui ni kwa nini baadhi ya wana CCM walizuiwa kufika igunga - hii inaonyesha ndani ya CCM yale makundi sasa ndiyo yamekomaa.
Mwisho nawapongenza wana CDM kwa ushindi wa kishindo Igunga na tunawaomba wana igunga wote kwamba muda ukifika CDM itarudi kuwashukuru, kazi nzuri sana na CDM sasa imepata focal point katika ukanda huo, hii itasaidia kupeleka ujumbe wilaya zingine jirani kama Sikonge, Urambo kwa 6, Nzega na hapo Tabora Mjini kwa mzee wa Mi-Bastola.
Kina mama, mama zetu tunawaomba imeifikia muda sasa muwaambie CCM kwamba khanga basi, vitenge basi ila mnataka utatuzi wa kero zenu.
Hakuna atakayebisha kwamba upepo wa kisiasa Tanzania umebadilika kabisa, harufu ya mageuzi imetanda, CCM imepotenza nguzo muhimu karibia zote na imebakiza hii ya KINA MAMA.
Siku ambayo mama zetu watastukia kwamba CCM sasa hawana jipya basi ndiyo itakuwa mwisho wake, wengi tunajua mama zetu ni wagumu sana kubadili uelekeo kwa ghafla, ingawa wao ndiyo wanapata shida kubwa sana hasa vijijini - lakini ndiyo wanakuwa kwa kwanza kushabikia CCM na kuvaaa khanga za chagua kikwete ambazo wengi huzitunza vizuri sana na kuzivaa wakati wa mikutano ya CCM.
Nachowasikitika CCM ni kupoteza nguzo ya VIJANA, vijana wengi kama si wote wapo CDM, unapopoteza nguzo hii ujue chama chako kinaingia shimoni, na kibaya zaidi CCM imekosa watu makini wa kujaribu kurudisha imani ya wananchi hasa vijana na hii ni hatari kubwa sana kwao.
CCM wanapofikia mahala pa kusema ushindi ni ushindi tu - hata wa kura moja zaidi ni ushindi - yaani hapo ujue kwamba sasa chama kimekosa mvuto na kinakufa, Chama kinapoanza kuangukia wazee wastaafu wakaokoe jahazi kwenye kampeni ina maana hakina vijana makini wa kukisemea mbele ya jamii na wakakubalika.
Chama kila kinapoenda kwenye mikutano yake ya kampeni lazima kiende na muziki na maigizo kuvuta wananchi- hapa lazima ufikiri mara mbili kwamba hoja zao hazina ushawishi kwa walio wengi kwa sasa. ndugu zangu hadi leo hatujui ni kwa nini baadhi ya wana CCM walizuiwa kufika igunga - hii inaonyesha ndani ya CCM yale makundi sasa ndiyo yamekomaa.
Mwisho nawapongenza wana CDM kwa ushindi wa kishindo Igunga na tunawaomba wana igunga wote kwamba muda ukifika CDM itarudi kuwashukuru, kazi nzuri sana na CDM sasa imepata focal point katika ukanda huo, hii itasaidia kupeleka ujumbe wilaya zingine jirani kama Sikonge, Urambo kwa 6, Nzega na hapo Tabora Mjini kwa mzee wa Mi-Bastola.
Kina mama, mama zetu tunawaomba imeifikia muda sasa muwaambie CCM kwamba khanga basi, vitenge basi ila mnataka utatuzi wa kero zenu.