Mtaji wa 2.5m/-, Naweza kufanya biashara gani?

mbongowakweli

JF-Expert Member
Aug 24, 2011
841
671
Wakuu msaada, najua kuna vichwa humu, naombeni msaada wa biashara gani nifanye, nina capital ya 2.5m/-.

Asanteni
 
Inabidi ueleze unataka kuwekeza ktk mji gani, maana kila sehemu kuna opportunities tofauti.
 
Taja mambo yafuatayo na utapata msaada wa mawazo:
1) Upo mji gani?
2) Una ujuzi gani lengo ni kujua strengths na weaknesses zako
3) Je umetenga muda gani kui supervise business yako?/ je, hujaajiriwa sehemu full time.
4) Aina gani ya biashara inayokujia kichwani? Na unatamani uifanye?
 
Hizi thread za biashara mtaji milioni, laki, elfu kumi sasa zimezidi!
Biashara nyingi zishasemwa humu ni swala la wewe kuangalia kama mwenzio alikuwa na 2m akashauriwa afuge kuku basi na wewe wa 2.5m biashara hiyo itakufaa.
Mwenye 10m anaweza fanya biashara sawa na mwenye 2m ila scale yenu ya b'ness ndio mkatofautiana.
 
Umesahau kwamba business environment ni dynamic, umesahau pia mawazo ya biashara gani ufanye yanabadilika kila sekunde, kumbuka pia wachangiaji wanaongezeka au kupungua katika jukwaa la biashara na mengineyo kila siku.
Hizi thread za biashara mtaji milioni, laki, elfu kumi sasa zimezidi!
Biashara nyingi zishasemwa humu ni swala la wewe kuangalia kama mwenzio alikuwa na 2m akashauriwa afuge kuku basi na wewe wa 2.5m biashara hiyo itakufaa.
Mwenye 10m anaweza fanya biashara sawa na mwenye 2m ila scale yenu ya b'ness ndio mkatofautiana.
 
Hizi thread za biashara mtaji milioni, laki, elfu kumi sasa zimezidi!
Biashara nyingi zishasemwa humu ni swala la wewe kuangalia kama mwenzio alikuwa na 2m akashauriwa afuge kuku basi na wewe wa 2.5m biashara hiyo itakufaa.
Mwenye 10m anaweza fanya biashara sawa na mwenye 2m ila scale yenu ya b'ness ndio mkatofautiana.

Taja mambo yafuatayo na utapata msaada wa mawazo:
1) Upo mji gani?
2) Una ujuzi gani lengo ni kujua strengths na weaknesses zako
3) Je umetenga muda gani kui supervise business yako?/ je, hujaajiriwa sehemu full time.
4) Aina gani ya biashara inayokujia kichwani? Na unatamani uifanye?

1) Upo mji gani?

Niko Dar

2) Una ujuzi gani lengo ni kujua strengths na weaknesses zako

Nina elimu ya chuo na masters, na nimefanya kazi toka nikiwa na miaka 18! Nimeanzisha ka bucha, inajiendesha vyema tu, nataka kuanzisha aina nyingine mkuu, sio bucha.

3) Je umetenga muda gani kui supervise business yako?/ je, hujaajiriwa sehemu full time.

Ntaisimamia mwenyewe, kuanzia mwanzo mpaka mwisho

4) Aina gani ya biashara inayokujia kichwani? Na unatamani uifanye?

Kwa sasa sina idea nyingine mkuu, na ndio maana nikaja hapa wazee
 
Umesahau kwamba business environment ni dynamic, umesahau pia mawazo ya biashara gani ufanye yanabadilika kila sekunde, kumbuka pia wachangiaji wanaongezeka au kupungua katika jukwaa la biashara na mengineyo kila siku.
sijasahau chochote, ngoja nisome kama kuna mtu atakuja na business idea mpya kabisa ambayo sijawahi kuisoma jf.
 
Mkuu, anzisha outlet ya nyama choma, mishkaki ya utumbo, kongoro special....something of the kind.
Kwa vile una bucha, utaweza kupata malighafi safi sana.
What you need to do is make something different, chukua jiko kwenye bar ya kawaida tu....utanambia mkuu.
 
Mkuu unachokisema ni kweli! Kwa kuwa jamaa ana biashara ya bucha tayari...atafute jiko sehemu aanze hiyo biashara na mimi naamini itamtoa.Unaweza kudharau lakini ROI yake ni ya ukweli na inawaweka wengi mjini.

Alternatively, kwa mtaji wako unawez a kufanya biashara ya nafaka. Uza mchele, maharagwe, karanga, kunde, njegere, unga wa kupima, mafuta etc Tembelea maeneo ya Manzese Tiptop, soko la Tandika kufanya survey kwa wauzaji wa jumla. Hiyo kitu ni guarantee watu lazima wale, we ni kucheza na bei tu. Buy low ..sell a little high!
Mkuu, anzisha outlet ya nyama choma, mishkaki ya utumbo, kongoro special....something of the kind.
Kwa vile una bucha, utaqweza kupata malighafi safi sana.
What you need to do is make something different, chukua jiko kwenye bar ya kawaida tu....utanambia mkuu.
 
Mkuu,unamiliki bucha,unaishi Dar,umesoma mpaka Masters,unasema utasimamia mwenyewe,Duh! sasa ktk SWOT ya fasta fasta tayari umeshashinda,wewe ni kufanya foward intergration tu,au backward int.kutegemea upo confortable na kipi,

nakushauri ununue mashine ndogo ya kutengeneza sosegi, chukua mabaki yako ya buchani tengeneza sosegi kama ulaya,tafuta kijana afanye usambazaji ,au tumia vijana wanaopita mtaani na ktk bar za dar wakiuza sosegi za Farmers Choice, nawe tengeneza brand yako kama hiyo ,tumia rangi za hivyo hivyo,ila jina tu liwe kama hilo tu. eg Farmers choices,Farmers sausege, au Farmers Sosegi,au Farm Choice,au Best Choice,ila kumbuka rangi na nembo yako vifananefanane na farmers choice,
hiyo wanaita brand extension e.g Azam cola ,badala ya Cocacola

this link itakupa all the details about how to start to make your own brand sausages
Sausagemaking.co.uk

b
ei za machine zinaanzia laki3 tu
http://www.designasausage.com/pages/prods.asp?catid= 1&subcatid=32
 
Ndg yangu Mbogowaukweli, sema tu una Sh. 2,500,000.00 ambazo hujui uzifanyie nini!

Hiyo ni hela ya kula na siyo capital aslan!

Umesema una Masters haya jiandalie mchanganuo wa biashara kama fedha hiyo haiishii kwenye mchakato tu wa biashara na siyo kuanzisha biashara? Hapa ndo maana tunakushauri fedha hiyo we kaifanyie shopping familia yako next time ukipata capital ndo uombe ushauri.

Nakushauri tena mtoe out my wife wako mkatumie hela hiyo ikuzoee ndo utapata maarifa ya kutafuta CAPITAL.
 
Ndg yangu Mbogowaukweli, sema tu una Sh. 2,500,000.00 ambazo hujui uzifanyie nini!

Hiyo ni hela ya kula na siyo capital aslan!

Umesema una Masters haya jiandalie mchanganuo wa biashara kama fedha hiyo haiishii kwenye mchakato tu wa biashara na siyo kuanzisha biashara? Hapa ndo maana tunakushauri fedha hiyo we kaifanyie shopping familia yako next time ukipata capital ndo uombe ushauri.

Nakushauri tena mtoe out my wife wako mkatumie hela hiyo ikuzoee ndo utapata maarifa ya kutafuta CAPITAL.

Boss wewe una hatari kweli, ungejua tu jinsi nilivoweza kuidunduliza io hela usingesema ivyo!

Anyway ndio maana ya kuomba msaada, itabidi nimeze mate na ushauri wa wazee wanaoona hii hela ndogo!
 
Wala usivunjike moyo mkuu, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake .....ndogo kwake kubwa kwako!!!!! Watu ambao wamezipitia changamoto za maisha watakupa michango yenye kukupa mwanga ni jinsi gani uta grow kwa kutumia hiyo hiyo capital yako inayoonekana ni ndogo kwa baadhi ya members!
Boss wewe una hatari kweli, ungejua tu jinsi nilivoweza kuidunduliza io hela usingesema ivyo!
Anyway ndio maana ya kuomba msaada, itabidi nimeze mate na ushauri wa wazee wanaoona hii hela ndogo!
 
mkuu anzisha joint ya choma ya game meat (nyama pori)


utauza
 
nafuatilia nyendo za ushauri kwa ukaribu...nipo mtwara nalima ufuta, si haba na net out 3 mil after 4 months
 
Kaweke heshima bar! On a serious note: biashara nzuri kwako itatokana na hobby yako. Hakuna hobby isiyo gharimiwa (which means kuna kugharamia ili kuipata). Kwa hiyo wageuze wanaopenda hobby yako kuwa wateja wako
 
Mtu hujawahi kununua chochote maisha yako yote kwa ajili ya kuuza halafu unakimbilia business forum kutoa ushauri wa kifala ****! Ingia kwenye forum zinazoendana na wewe u-discuss miss tanzania. Hili ni jamvi la wapiganaji wanaotaka kuingia front!!!

Nirudi sasa kwenye mada. Kaka bila kusita tafuta sehemu yenye watu wengi ufungue MPESA na TIGOPESA haraka. Nakwambia ndani ya robo ya mwaka utakua unapata 1m kila mwezi. Baada ya mwaka utakua una mtaji wa kutosha kufanya shughuli zingine. Tena huna haja ya kukodi fremu mwenyewe unaweza ukaongea na mtu mwenye fremu tayari ukachangia kodi ili ufanye kazi kwenye sehemu yake.

Hii ni fursa ya kukusanya mtaji. KIKUBWA punguza sana gharama zako za kuishi kadri iwezekanavyo kipindi chote unachokusanya mtaji halafu jaribu kuongea na watu positive sababu kuna mijitu iko hapa duniani kuvunja wengine moyo tu.....
 
Hiyo ni pesa mbuzi kwa biashara kwa mtu mwenye Masters, itoe tu sadaka kanisani au msikitini, mungu atakuongezea maradufu.
 
Back
Top Bottom