Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Mtafiti mwandamizi mwenye utata katika Taasisi ya Utafiti wa Jamii ya Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, Dk Stella Nyanzi ametimuliwa chuoni hapo kufuatia mabadiliko yaliyowasomba pia wanataaluma wengine 45 katika taasisi hiyo.
Dk Nyanzi aliwekwa rumande katika gereza la Luzira akikabiliwa na mashitaka ya unyanyasaji kwenye mitandao na kumkosesha amani Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Aliendelea kuwekwa rumande katika gereza hilo Desemba 19, 2018 na ilikuwa aile Krismasi gerezani baada ya kuyakana mashitaka ya makosa ya mitandao akisema hayana msingi.
Kwa mujibu wa Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Makerere, Profesa Barnabas Nawangwe amesema idadi kubwa ya wana taaluma hao walioondolewa ni wale waliokuwa watoro kazini kwa zaidi ya miaka mitano huku wengine wakihusishwa na kesi za unyanyasaji wa kijinsia.
Dk Swizen Kyomuhendo ambaye ni mhadhiri wa Shule ya Sayansi ya Jamii naye ameondolewa kutokana na hasara iliyopatikana kwa utendaji uliokiletea sifa mbaya chuo hicho.
Dk Kyomuhendo aliingia matatani baada ya televisheni ya NBS kumhusisha na tukio la kulala na mwanafunzi wake kwa ahadi ya kumpa maksi Februari 26, 2018. Hata hivyo mahakama haikumkuta na hatia kwa makosa hayo.
Dk Nyanzi aliwekwa rumande katika gereza la Luzira akikabiliwa na mashitaka ya unyanyasaji kwenye mitandao na kumkosesha amani Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Aliendelea kuwekwa rumande katika gereza hilo Desemba 19, 2018 na ilikuwa aile Krismasi gerezani baada ya kuyakana mashitaka ya makosa ya mitandao akisema hayana msingi.
Kwa mujibu wa Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Makerere, Profesa Barnabas Nawangwe amesema idadi kubwa ya wana taaluma hao walioondolewa ni wale waliokuwa watoro kazini kwa zaidi ya miaka mitano huku wengine wakihusishwa na kesi za unyanyasaji wa kijinsia.
Dk Swizen Kyomuhendo ambaye ni mhadhiri wa Shule ya Sayansi ya Jamii naye ameondolewa kutokana na hasara iliyopatikana kwa utendaji uliokiletea sifa mbaya chuo hicho.
Dk Kyomuhendo aliingia matatani baada ya televisheni ya NBS kumhusisha na tukio la kulala na mwanafunzi wake kwa ahadi ya kumpa maksi Februari 26, 2018. Hata hivyo mahakama haikumkuta na hatia kwa makosa hayo.