spencer
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 3,599
- 3,220
- Nani anaifahamu NCCR ya 1995 iliyokuwa na wabunge karibu ishirini ilikoishia??
Lyatonga Mrema NCCR-TLP
Mabere Marando NCCR-CDM
Kilichotokea Raskazone TANGA-mahali ambapo Mrema aliokolewa na Bodyguard wake-Chama kilisambaratika na wengine kuneemeka kwa kupewa ubunge wa East Afrika na CCM
- Nani anaifahamu CUF ya 1995 jinsi ilivyokuwa ya upande mmoja, Mwaka 2000 Mnakumbuka watu waliokimbilia Shimoni MOMBASA Kenya Toka Pemba?
Visiwani hasa Pemba Elimu Uraia iko juu na ndiyo maana imebidi wakubali matokeo CCM kwa kuamua kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa, Ingawa kwa maoni yangu CUF wametereza, ilifaa waachiwe nchi
- Nani anamkumbuka Warid Aman Kobouru aliyekuwa kiongozi mahiri Kigoma mjini aliyempeleka puta Premji, saivi yuko wapi alitimkia CCM akaiacha Chadema hadi leo Madiwani ni wengi CDM na CDM ndiyo inateua Meya pale.Sishangai kuona baadhi viongozi CDM kuonekana kuyumbishwa na mafisadi, Shauri yao waache wajiue wenyewe kisiasa ila ninachoamini ni kuwa watanzania wengi wanamapenzi ya dhati na CDM na Si mtu. Kumbukeni viongozi wa CCM ni wale wale na mbinu zao ni zile zile, hawana jipya ila kama hawako makini wafamu ya kuwa vijana tupo wengi ambao tuko dedicated kuamsha UMMA wa watanzania.
Thank You
:A S-omg: