Mtaani Serikali ya Rais Samia inapoteza uungwaji mkono kwa kasi ya kutisha

Kosa halianzii kwake bali linaanzia kwa Mwendazake alipomteua kuwa Mgombea mwenza.

Bazungu balonga; it is a vicious cycle.
Usikute makamu wa Rais anautamani Urais kaamua kumchuuza mama awanyanyase wapinzani ili apate laana tokea kwa wananchi baadae yeye awe Rais
 
Wamemshauri vibaya ili aharibu apate chuki tokea kwa watanzania yafaa mama azinduke mapema kabla chuki hajiasambaa zaidi
 
Mitaa ipi??Huku nnapokaa watu hawajadili siasa kabisa..hawana hata time na mijadala..

Ukiingia JF ndo unakuta malalamiko tele..

Huku mitaani no body cares that much

Unakaa mitaa ya maiti hai.
 
Mitaa ipi??Huku nnapokaa watu hawajadili siasa kabisa..hawana hata time na mijadala..

Ukiingia JF ndo unakuta malalamiko tele..

Huku mitaani no body cares that much
Hata 'miamala'! Hakuna anayesema kitu?

Hiyo mitaa unayoishi itakuwa ni ya aina yake. Pengine siyo ya nchi hii!
 
  • Thanks
Reactions: cmp
Mitaa ipi??Huku nnapokaa watu hawajadili siasa kabisa..hawana hata time na mijadala..

Ukiingia JF ndo unakuta malalamiko tele..

Huku mitaani no body cares that much
Hivi mkuu kwanini huwa hujiongezi hata siku moja kuwa kwenye ukweli? Hivi ni kweli huoni na kusikia malalamiko ya wananchi kila kona kuhusu tozo?

Watu wameacha kufanya miamala zaidi ya robo tatu hizi ni takwimu halisi kutoka kwenye makampuni ya simu.

Usiwe mtu wakusifia tu wakati mwingine simama kwenye ukweli utaheshimika.
 
Mitaa ipi??Huku nnapokaa watu hawajadili siasa kabisa..hawana hata time na mijadala..

Ukiingia JF ndo unakuta malalamiko tele..

Huku mitaani no body cares that much
Pia ukikuta mijadala jf ujue kuna jambo lisilo la kawaida mtaani ndo maana watu wanaogopa kutoa mawazo yao kuogopa kupewa kesi mbaya za ugaidi kisa kudai jambo la haki.

Kumbuka hao hao waliopo jf ndo hao hao wanaoishi mitaani.
 
Hiyo ya 3 ungeiacha kwa sababu na Mboe pia inatoa povu sana na hiyo biashara hatuelewi, yaani yeye na mama ni wamoja.
Ya 4 hilo kundi unalolisema ni wapinzani hasa wa Ufipa walimfurahia sana mama ila mara alipotia pini yote ndiyo tumeanza kusikia kelele za maumivu zinasikika kama vile siyo wao (ninyi) mnaosemaga CCM ni ile ile. Au mkisema mnaonea tu, eleweni ni kweli CCM ni ile ile...
Ukae stakishari wiki nzima kwanini? Sheria gani inayosema mtu ashikiliwe kituo cha police zaidi ya saa 24 kabla yakupelekwa mahakamani?

Au ndo kule kutawala pasipo kuangalia sheria za nchi?
 
Umeandika vema kabisa.

Nilimkubali sana mama Samia alivyoanza kuzungumzia Haki na maendeleo kwa umma.

Leo mama amerudi kwenye Ule utawala wa kidhalimu .

Uovu waliofanya wale akina Sabaya ulikua ni uovu wa kishetani kwa Taifa letu.

Hivi kweli Mama Samia amekubali Genge la Warundi waliotoroka Kwao kwa kuua watu kwa ajili ya madaraka kuhamishia uovu wao hapa Tanzania. ? Wamejifanya ni Wasukuma na wengine wanajifanya ni Wahaya na wengine wanajifanya ni Wasukuma. Ni kizazi cha wauaji walioua wenzao miaka ya 90 . Ni kizazi chenye Harufu ya Damu kwa ajili ya kusaka Madaraka na Mali. Hawa walikua wanaua watu na kuteka mabasi na kupora Mifugo na Mali za Watanzania wapole huku wakishirikia na ndugu zao waliokua wamejipenyeza serikalini na kwenye vyombo vya Dola.

Awamu ya Tano walifanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kuingia ndani ya mfumo wa kidhalimu. Hawa ndio wanaomyumbisha Rais Samia. Wanataka kumtisha ili wapate fursa ya Madaraka ndani ya vyombo vya dola na Serikali mana wanajua kuwa Watanzania halisi hawawezi kutumia mapanga na risasi kuwaua au kuwatesa binadam wenzao.

Wanajua kuwa kula yao ni kuua na kutisha watu hivyo serikali ya Rais Samia ikikubali kuwa serikali ovu ya mtutu wa Bunduki basi watapata fursa tele za kuonea na kuchinja Watanzania halisi ambao kwa asili ni Wapole. Upole wa Watanzania wameutumia kukalia Tanzania kimabavu huku wakitaka kumwendesha Mama zamia na kumjaza woga kuwa kuna tishio la ugaidi.

Mama Samia bado hajagundua kuwa wabaya wake wako ndani ya CCM. Leo hii wanaompinga kwa dharau kabisa wapo ndani ya serikali na Chama chake .Gwajima ameonyesha dharau kubwa sana kwa Rais wa nchi kwa sababu tu sio genge lile la Wakuja wanye hulka za ukatili. Hamfrei Polepole naye pia ameonyesha dharau.

Hivi Mama anasubiri nini kuwatimua Wapinzani wake ndani ya Chama? Ambao kimsingi hawana Shukurani zaidi ya dharau na kujiona kuwa wao ndio bora kuliko watu wote. Hivi Gwajima hajui kuwa alibebwa kwenye Uchaguzi? Kama anafikiri kukosoa ni Rahisi kwa nini asihamie upinzani akaona ugumu wa kuwa mpinzani Afrika.

Wapinzani wameumrizwa sana na awamu ya tano. Bado Yale majini na mashetani ndani ya Chama tawala hayajachoka tu kumwaga damu za watu wasio na hatia.

HIVI GWAJIMA ANASEMAJI KUWA ANAMPENDA YESU NA KUWA ALITESWA KWA KUONEWA NA SERIKALI YA WARUMI , WAKATI HAMPENDI MBOWE ANAYEONEWA NA SERIKALI YAKE LEO ?!

HIVI GWAJIMA HAONI KUWA ANGEKUA AMEISHI ZAMA ZA YESU BILA SHAKA YOYOTE ANGESIMAMA NA SERIKALI DHALIMU YA WARUMI KUMUUA YESU?

HIVI GWAJIMA HAONI KUWA ANATUMIA MUDA MWINGI KUFURAHISHA WANACCM WALIOUMIZA WATU AWAMU ZOTE TANGU MKAPA MPAKA SASA SAMIA BADALA YA KUHUBIRI JUU YA KUACHA DHAMBI ; KUACHA UZINZI ULIOJAA KWA WATAWALA,KUACHA UBASHA ULIOJAA KIMYAKIMYA,KUACHA RUSHWA,KUACHA ULAFI,KUACHA ULEVI NA UHUNI UNAOFANYWA NA WATAWALA, KUACHA DHULMA WAKATI WA UCHAGUZI, KUACHA UFISADI NA UPENDELEO WA WAKURUGENZI, KUACHA KUBAMBIKIA WATU KESI, KUACHA KUJILIMBIKIZIA MALI HUKU WENGINE WAKIKOSA HATA MKATE WA KULA , KUACHA MFUMO MBOVU WA TAIFA MOJA KUWA NA WATUMISHI WANAOTUMIKA KWA UJIRA UNAOTOFAUTIANA KAMA MBINGU NA ARDHI, KUACHA KUPATA UTAJIRI NA UTAWALA KWA KUTUMIA USHIRIKINA ?

Haya madhambi yaliyojaa kwenye serikali yake inayobambiwatendajiesi inamaana Askofu Gwajima hayaoni au anaona ni halali kwa sababu yanatendwa na wanaojiita waheshimiwa kama Yeye. Leo Gwajima anaona jambo moja tu Mabeberu.

Hakika Dunia haistahili kupata Amani kwa sababu imejaa madhambi matupu na Mungu hafurahishwi na dhambi.

Ushauri wangu kwa Askofu Gwajima; Kuanzia sasa hubiri watu waache dhambi. Dhambi ndiyo inayoliangamiza Taifa na dunia na sio Korona wala Wazungu.
Hubiri watu waishi kwa Upendo wa Kristo sio wa Makristo wa uongo waliojawa na uchu wa Mali hata kwa kuua na kudhulumu alimradi wapate.
Hivi Gwajima hajiulizi tu kuwa ni kwa nini watu wapo tayari hata kumpiga MTU risasi hadhari ,mtu anayekosoa tu katiba iliyoandikwa na kikundi cha watu.?

Kama Gwajima anaweza kufurahiya mateso ya wapinzani kwa sababu ya kukosoa Katiba inayowaumiza ambayo sio dhambi kuibadili ili itende Haki kwa usawa , atashindwaje kuchochea mauaji ya kidini kutetea imani na vitabu visivyoweza kubadilishwa kabisa ?
.
Gwajima hana amani moyoni kwa sababu anajua wazi kuwa yupo upande wa Dhulma. Na akijifanya ana Furaha huku madhambi yakiwa yanatendwa kila mahali basi anajidanganya na Mungu hafurahishwa na uongo.

Hivi utawasimamaje Madhebahuni na kuishangilia serikali na watendaji wanaotumia kodi za umma kutengeneza hila za kuwaumiza watu na kujenga hofu na chuki na uhasama kwenye jamii , badala ya kuwaleta watu pamoja?


Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
 
Mitaa ipi??Huku nnapokaa watu hawajadili siasa kabisa..hawana hata time na mijadala..

Ukiingia JF ndo unakuta malalamiko tele..

Huku mitaani no body cares that much
People care a lot mkuu, hasa kwenye hizi tozo, people are not happy...that I can tell you. Sema sisi bwana...soon tutasahau maisha yataendelea...
 
Gesi nayo imepanda toka 45 hadi 55 ameamua kukomoa watu
Hii sasa hatari, 10k nzima? Tunakoenda sio poa hata kidogo..

Update nimepewa bei ya mihan...51,000...stupeeed!

Kwenye construction wametangaza bei za bidhaa zinapanda tena kuanzia leo. Kuna agent inabidi nimcheki nipate uhakika

Futseke!![/Color]
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom