Mtaani kupo kimya utadhani sio mwaka wa Uchaguzi

Ne Mbwitu

JF-Expert Member
Aug 23, 2020
275
802
Kwa kweli mwenendo wa uchaguzi huu ni kielelezo cha ukali wa maisha. Miaka ya nyuma vipindi kama hivi ni hekaheka tu mtaani, wenye vitenge vya chama, kofia, n.k walikuwa busy kuwanadi Wagombea wao wa Udiwani na Ubunge.

Mwaka huu hata mabango ya barabarani, kwenye kuta, nguzo ni ya mgombea mmoja tu (One Man Show).

Hali za maandalizi ya kampeni ni ya kusuasua sana. Kwa kweli hivi ikitokea huyu mnunuzi wa madege ya mabeberu akapenya tena, si watu watakula hadi magome ya miti.

Kwa kweli kama taifa tunahitaji kujihurumia bila kujali umeahidiwa cheo gani.
 
Usisahau pia Mwigulu Nchemba aliyachora mawe ktk barabara zote nchini kwa chokaa akijiita rais.
 
Tatzo asilimia kubwa ya wananchi wamepoteza iman juu ya wanasiasa na hali ngum ya maisha inachangia pia
 
Tatzo asilimia kubwa ya wananchi wamepoteza iman juu ya wanasiasa na hali ngum ya maisha inachangia pia
Yote, pia mzunguko wa pesa upo chini sana. Ukiwabana watumishi, wakandarasi, makampuni, wafanyabiashara, unauua mzunguko wa pesa kwenda kwa watu wenye hali ya chini. Hali ni tete.
 
Kwa kweli mwenendo wa uchaguzi huu ni kielelezo cha ukali wa maisha. Miaka ya nyuma vipindi kama hivi ni hekaheka tu mtaani, wenye vitenge vya chama, kofia, n.k walikuwa busy kuwanadi Wagombea wao wa Udiwani na Ubunge.

Mwaka huu hata mabango ya barabarani, kwenye kuta, nguzo ni ya mgombea mmoja tu (One Man Show).

Hali za maandalizi ya kampeni ni ya kusuasua sana. Kwa kweli hivi ikitokea huyu mnunuzi wa madege ya mabeberu akapenya tena, si watu watakula hadi magome ya miti.

Kwa kweli kama taifa tunahitaji kujihurumia bila kujali umeahidiwa cheo gani.
Wakulungwa tumenyuti, hatufurukuti, tumeshafanya maamuzi, tunasubiri siku ya kuchinja ifike tuchinje takataka za kijani zote
 
Back
Top Bottom