Mtaalamu wa Ugavi na Manunuzi mwenye uzoefu mkubwa wa uondoshaji mizigo bandarini naomba ajira

Kichaafulani

JF-Expert Member
Feb 13, 2015
1,295
1,269
Habari Wakuu,

Kama ambavyo kichwa cha habari kinavyojieleza, mimi ni mtaalamu wa manunuzi niliyethibitishwa na Bodi ya wataalamu wa ugavi na manunuzi (CPSP). Nina uzoefu wa kufanya kazi katika kampuni tatu tofauti kwenye nafasi ya afisa mgavi. Nina uzoefu wa kufanya kazi za uondoshaji mizigo bandarini (clearing and Freight Forwarding).

Ninajitambua, ni mwenye kujituma na muaminifu pia nina ushirukiano mzuri kwa wanyakazi wenzangu na ujuzi wa huduma kwa mteja nipo tayari kufanya kazi katika mazingira tofauti na pasipo usimamizi.

Kwa unyenyekevu mkubwa kabisa naomba kampuni au shirika, mtu binafsi au serikali inipatie kazi ili niweze kutumika kutimiza malengo ya kampuni husika.

Nitashukuru endapo utaweza tumika kama kiunganishi mwana JF mwenzangu.

Natanguliza shukrani na Mungu awabariki sana
 
Back
Top Bottom