Mtaalamu wa mifugo (Dr. by Veterinarian): Karibuni kwa ushauri, tiba na dawa za mifugo tu

Dokta Naomba nisaidie hii kitu
Mwaka Jana nilifuga kuku aina ya Sasso ila walipofikisha umri wa miezi mitano changamoto ikawa kwenye majogoo ya kupandishia ili nianze kufaidi mayai ikabidi niuze wote!

Nimeanza tena mwaka huu ila nahisi tatizo litakua lile lile Yaani uhaba wa majogoo yaliyopevuka kuwapanda hawa matetea!

Naomba ushauri wako kama kuna namna ya kuondokana na hii changamoto kitaalamu ( yaani matetea wanapofika hatua ya kutaga na majogoo yawe yanauwezo wa kupanda)
theriogenology
 
Dokta Naomba nisaidie hii kitu
Mwaka Jana nilifuga kuku aina ya Sasso ila walipofikisha umri wa miezi mitano changamoto ikawa kwenye majogoo ya kupandishia ili nianze kufaidi mayai ikabidi niuze wote!

Nimeanza tena mwaka huu ila nahisi tatizo litakua lile lile Yaani uhaba wa majogoo yaliyopevuka kuwapanda hawa matetea!

Naomba ushauri wako kama kuna namna ya kuondokana na hii changamoto kitaalamu ( yaani matetea wanapofika hatua ya kutaga na majogoo yawe yanauwezo wa kupanda)
theriogenology
Kwanza nikupongeze kwa kutokukata tamaa na inaonesha ni jinsi gani ulivyo na moyo wa ufugaji mkuu....

Kwanza kabisa kwa exprience yangu katika industry hii hao kuku aina sasso mara nyingi hufugwa kwa ajili ya nyama na si mayai (ingawa naona wafugaji wanajitahidi kuwafuga kwa ajili ya mayai) ila kiuhalisia productivity yake hasa kwa upande wa mayai ni very very low ku compare na jamii nyingine kama kuroiler...

Kwa ushauri wangu kama kweli unahitaji kufuga kuku tofouti na layer kwa ajili ya mayai basi ni vyema ukaingia moja kwa moja kwa kuroiler and not sasso maana wanachukua muda mrefu kuja kuanza kutaga ambapo huenda hadi miezi saba bila kuanza kutaga....

Na pia feed consumption yao iko juu sana na kwa hili inabidi ujipange vizuri maana ratio yao ya kula iko tofouti kidogo....

Na imani kwa maelezo hayo nifakuwa nimekupa mwanga kidogo mkuu...
 
Kwanza nikupongeze kwa kutokukata tamaa na inaonesha ni jinsi gani ulivyo na moyo wa ufugaji mkuu....

Kwanza kabisa kwa exprience yangu katika industry hii hao kuku aina sasso mara nyingi hufugwa kwa ajili ya nyama na si mayai (ingawa naona wafugaji wanajitahidi kuwafuga kwa ajili ya mayai) ila kiuhalisia productivity yake hasa kwa upande wa mayai ni very very low ku compare na jamii nyingine kama kuroiler...

Kwa ushauri wangu kama kweli unahitaji kufuga kuku tofouti na layer kwa ajili ya mayai basi ni vyema ukaingia moja kwa moja kwa kuroiler and not sasso maana wanachukua muda mrefu kuja kuanza kutaga ambapo huenda hadi miezi saba bila kuanza kutaga....

Na pia feed consumption yao iko juu sana na kwa hili inabidi ujipange vizuri maana ratio yao ya kula iko tofouti kidogo....

Na imani kwa maelezo hayo nifakuwa nimekupa mwanga kidogo mkuu...
ahsante
Uko sahihi kabisa Mkuu kwa ishu ya chakula Sasso ni hatari!
kama ukiwa mbali naweza ukahisi mlishaji ameuza chakula !

Sasa hivi mfano kuloirer wakifikisha hiyo miezi mitano ya kuanza kutagamajogoo wake wanakuwa wanauweza wa kupanda?
au inabidi utafutie majogoo mengine nje yaliyopevuka?
 
ahsante
Uko sahihi kabisa Mkuu kwa ishu ya chakula Sasso ni hatari!
kama ukiwa mbali naweza ukahisi mlishaji ameuza chakula !

Sasa hivi mfano kuloirer wakifikisha hiyo miezi mitano ya kuanza kutagamajogoo wake wanakuwa wanauweza wa kupanda?
au inabidi utafutie majogoo mengine nje yaliyopevuka?
Wanapandwa kama kawaida mkuu... haina haja ya wewe kutafuta jogoo mwingine wa ziada
 
Kwanza nikupongeze kwa kutokukata tamaa na inaonesha ni jinsi gani ulivyo na moyo wa ufugaji mkuu....

Kwanza kabisa kwa exprience yangu katika industry hii hao kuku aina sasso mara nyingi hufugwa kwa ajili ya nyama na si mayai (ingawa naona wafugaji wanajitahidi kuwafuga kwa ajili ya mayai) ila kiuhalisia productivity yake hasa kwa upande wa mayai ni very very low ku compare na jamii nyingine kama kuroiler...

Kwa ushauri wangu kama kweli unahitaji kufuga kuku tofouti na layer kwa ajili ya mayai basi ni vyema ukaingia moja kwa moja kwa kuroiler and not sasso maana wanachukua muda mrefu kuja kuanza kutaga ambapo huenda hadi miezi saba bila kuanza kutaga....

Na pia feed consumption yao iko juu sana na kwa hili inabidi ujipange vizuri maana ratio yao ya kula iko tofouti kidogo....

Na imani kwa maelezo hayo nifakuwa nimekupa mwanga kidogo mkuu...
Dr na Mimi nilikumbana na changamoto kama aliyo ipata Ngushi. Nilikuwa na Sasso kwa ajili ya mayai ila nikaja kugundua ni wazuri kwa nyama kama ulivyo sema. Nilifanikiwa kuwauza wote ila najipanga kuanza upya. Japo changamoto nayo kutana nayo ni kwamba mpaka sasa sijapata uamuzi nichukue kuku aina gani?.

Japo kwa mawazo yangu nilikuwa naangalia uwezekano wa kufuga hawa wa kienyeji pure. Kuroila napata wasi wasi wasije wakawa kama Sasso nikala hasara tena. Kwa ushauri wako kati ya kuroila na hawa wakienyeji pure wapi wana tija hasa kwa kuangalia gharama za matunzo VS kiwango cha utagaji mayai.
 
Dr na Mimi nilikumbana na changamoto kama aliyo ipata Ngushi. Nilikuwa na Sasso kwa ajili ya mayai ila nikaja kugundua ni wazuri kwa nyama kama ulivyo sema. Nilifanikiwa kuwauza wote ila najipanga kuanza upya. Japo changamoto nayo kutana nayo ni kwamba mpaka sasa sijapata uamuzi nichukue kuku aina gani?. Japo kwa mawazo yangu nilikuwa naangalia uwezekano wa kufuga hawa wa kienyeji pure. Kuroila napata wasi wasi wasije wakawa kama Sasso nikala hasara tena. Kwa ushauri wako kati ya kuroila na hawa wakienyeji pure wapi wana tija hasa kwa kuangalia gharama za matunzo VS kiwango cha utagaji mayai.
Kulinganisha productivity kati ya kuroiler na kienyeji ni sawa na kulinganisha passo na range rover mkuu....

Kuroiler anawastani wa kutaga mayai hadi 200 kwa mwaka na kienyeji wanauwezo wa kutaga wastani wa mayai 40-50 kwa mwaka nadhani kuna utofouti mkubwa hapo....

So kwa ushauri wangu nakushauri uende kwa kuroiler unapatikana wapi?
 
Kulinganisha productivity kati ya kuroiler na kienyeji ni sawa na kulinganisha passo na range rover mkuu....

Kuroiler anawastani wa kutaga mayai hadi 200 kwa mwaka na kienyeji wanauwezo wa kutaga wastani wa mayai 40-50 kwa mwaka nadhani kuna utofouti mkubwa hapo....

So kwa ushauri wangu nakushauri uende kwa kuroiler unapatikana wapi?
Nashukuru kwa elimu. Nipo Dar es salaam. Ni vyanzo gani naweza kupata mbegu nzuri ya kuroiler ?
 
Nashukuru kwa elimu. Nipo Dar es salaam. Ni vyanzo gani naweza kupata mbegu nzuri ya kuroiler ?
Nitakuunganisha na my fellow Dr yupo kwa kampuni moja inayotoa first filial generation ambayo utawatumia kwa kuzalisha mayai ambayo kwa hapo baadae ukiwa na mpango wa kutotolesha utatoa vifaranga wenye ubora zaidi.....

Siku ukiwa tayari naomba unitafute mkuu...
 
Nitakuunganisha na my fellow Dr yupo kwa kampuni moja inayotoa first filial generation ambayo utawatumia kwa kuzalisha mayai ambayo kwa hapo baadae ukiwa na mpango wa kutotolesha utatoa vifaranga wenye ubora zaidi.....

Siku ukiwa tayari naomba unitafute mkuu...
Unaweza kuwa na taarifa zao kama Vifaranga vinapatikana vya umri ganii kama ningepata na bei ingekuwa vyema zaidi?, ukiweka oda unachukua baada ya muda gani? Na wanauza kuanzia Vifaranga vingapi? . Kama una majibu ya hayo maswali naomba unisaidie ili nijipange vizur.
 
Mkuu naomba unipe kanuni za ufugaji wa kuku wa kienyeji ulio bora.
Pia ufugaji wa samaki, aina za samaki wafaao kufugwa, uandalizi wa bwawa, mazingira na kina cha maji.

Nitashukuru nikipata ushauri toka kwako ili nipate pa kuanzia.
 
Mkuu theriogenology Naomba msaada wako wa haraka
Kuku wangu wanaumwa sana
Dalili zake wake wanakuwa wamenyong'onyea, Halafu wanakua kama wanaona baridi na mwisho wa nashindwa kula kabisa!

Alianza mmoja nikamtenga nikadhani huenda Ni typhoid nikawapa OTC ila naona haijasaidia mpaka wamekufa! leo tena naona wawili wanaonyesha dalili hizo hizo

Nisaidie nitumie dawa gani ndugu yangu....
 
Mkuu theriogenology Naomba msaada wako wa haraka
Kuku wangu wanaumwa sana
Dalili zake wake wanakuwa wamenyong'onyea, Halafu wanakua kama wanaona baridi na mwisho wa nashindwa kula kabisa!

Alianza mmoja nikamtenga nikadhani huenda Ni typhoid nikawapa OTC ila naona haijasaidia mpaka wamekufa! leo tena naona wawili wanaonyesha dalili hizo hizo

Nisaidie nitumie dawa gani ndugu yangu....
Pole kwa kuuguliwa na kuku wako mkuu... Ningependa kujua ratiba ya chanjo kwa kuku wako mkuu?

Na ukiacha hizo dalili kuna dalili nyingine wanazo onesha? Rangi ya kinyesi iko vipi?

Naomba uwatenge kuku wote wanaoonesha dalili ya kunyong'onyea na pia ningependa uwaanzishie dose Tylodox kwa siku tano mfululizo na pia hao kuku ambao hawana dalili hizo ni vyema wakawa katika the same treatment......

Na mwisho zingatia usafi wa banda lako mkuu na kama wanataga hayo mayai yake naomba usiyaingize sokoni kuepuka madhara ya drug (antibiotics) residue kwa walaji hadi pale dawa itakavyokuwa imekwisha mwilini....

Ni hayo tu mkuu " Goodluck
 
Pole kwa kuuguliwa na kuku wako mkuu... Ningependa kujua ratiba ya chanjo kwa kuku wako mkuu?

Na ukiacha hizo dalili kuna dalili nyingine wanazo onesha? Rangi ya kinyesi iko vipi?

Naomba uwatenge kuku wote wanaoonesha dalili ya kunyong'onyea na pia ningependa uwaanzishie dose Tylodox kwa siku tano mfululizo na pia hao kuku ambao hawana dalili hizo ni vyema wakawa katika the same treatment......

Na mwisho zingatia usafi wa banda lako mkuu na kama wanataga hayo mayai yake naomba usiyaingize sokoni kuepuka madhara ya drug (antibiotics) residue kwa walaji hadi pale dawa itakavyokuwa imekwisha mwilini....

Ni hayo tu mkuu " Goodluck
Ubarikiwe sana ndugu yangu,
Nilikua nazingatia sana ratiba ya chanjo!( hawatagi Mkuu ndio kwanza wamefunga miezi miwili wiki iliyopita)
Toka nimechukua na hivi juzi tu ndio nimewapa chanjo ya ndui( Ingawa hii nilichelewa kidogo nimewapa wakiwa na miezi miwili)

Walionyesha dalili ya damu kwenye kinyesi nikawapa OTC wakawa poa(Ingawa tatizo hili la damu kwenye kinyesi nalo naona linajirudia sana na Mara zote nikiwapa hiyo OTC kinyesi kunarudi kuwa poa) Sasa Sijui haiwafai?
 
Ubarikiwe sana ndugu yangu,
Nilikua nazingatia sana ratiba ya chanjo!( hawatagi Mkuu ndio kwanza wamefunga miezi miwili wiki iliyopita)
Toka nimechukua na hivi juzi tu ndio nimewapa chanjo ya ndui( Ingawa hii nilichelewa kidogo nimewapa wakiwa na miezi miwili)

Walionyesha dalili ya damu kwenye kinyesi nikawapa OTC wakawa poa(Ingawa tatizo hili la damu kwenye kinyesi nalo naona linajirudia sana na Mara zote nikiwapa hiyo OTC kinyesi kunarudi kuwa poa) Sasa Sijui haiwafai?
Kama ni suala la damu kwenye kinyesi yaweza kuwa coccidiosis......

Na kwa upande wa dawa naomba uwapatie ESB3 iko vizuri mno.....
 
Kama ni suala la damu kwenye kinyesi yaweza kuwa coccidiosis......

Na kwa upande wa dawa naomba uwapatie ESB3 iko vizuri mno.....
Mkuu nashukuru sana kuku wangu wamepona mkuu!
Ubarikiwe sana sana aiseee!
Walikufa watano tu nadhani ningeijua mapema hii dawa kusingekuwa na kifo chochote!!

Ungekuwa Iringa wakikua ningekupa mmoja wa mboga

Shukrani sana
 
Mkuu nashukuru sana kuku wangu wamepona mkuu!
Ubarikiwe sana sana aiseee!
Walikufa watano tu nadhani ningeijua mapema hii dawa kusingekuwa na kifo chochote!!

Ungekuwa Iringa wakikua ningekupa mmoja wa mboga

Shukrani sana
Usijali mkuu ukiona wanaonesha dalili za ambazo huzielewi usisite kunitafuta kwa msaada zaidi.....

Hahah wakiwa wengi utaniuzia mmoja unitumie hela ya bia....

Una kuku wa aina gani mkuu....
 

Similar Discussions

36 Reactions
Reply
Back
Top Bottom