Mtaalamu wa mifugo (Dr. by Veterinarian): Karibuni kwa ushauri, tiba na dawa za mifugo tu

Mlo Mara ngapi maana hats USIKU naamka! Kwa kifupi napenda sana mbwa,hawa niliwakuta Sokoni wamezaaliwa na mama yao wasamaria wema wakasema hajaonekana siku mbili ikabidi waniuzie Mwenye banda walipo zaliwa
Just twice a day mkuu
 
Mlo Mara ngapi maana hats USIKU naamka! Kwa kifupi napenda sana mbwa,hawa niliwakuta Sokoni wamezaaliwa na mama yao wasamaria wema wakasema hajaonekana siku mbili ikabidi waniuzie Mwenye banda walipo zaliwa
Halafu dawa ya minyoo (ascarten P) unaanza wapa wanapofikisha wiki4 then 6 and 8 wiki ya kumi na mbili unawapa ivermectin na unarudia kila baada ya miezi 3
 
Mkuu kwa case yako kuku kutoa choo cheupe kilichochanganya na kijani ni mwanzo mwa dalili ya homa ya matumbo kwa kuku (fowl typhoid) ama kipindupindu cha kuku (fowl cholera) hivyo basi ningekushauri umtenge huyo kuku mgonjwa na umwanzishie dose ya ESB3 kwa siku tatu changanya vijiko vinne vya chai kwa maji ya lita 20 mpe anywe.....

Na pia ningependa uwaanzishie dose kuku waliosalia kwa kuwapa pia Esb3 iwe kama prophylaxis dhidi ya ugonjwa huu....

Kwanini Esb3 hii dawa ni jamii ya sulfur na inauwezo wa kukinga kuku wako dhidi ya magonjwa matatu nayo ni fowl typhoid fowl cholera na coccidiosis....

Kila la kheri Mkuu....
Asante sana mkuu! Umekua msaada sana tangu ulipoleta uzi huu! Je naweza kuwapa chanjo ya newcastle sambamba na hayo maelezo hapo juu? Au nimalize kwanza ESB3 then ndio niwachanje?
 
Asante sana mkuu! Umekua msaada sana tangu ulipoleta uzi huu! Je naweza kuwapa chanjo ya newcastle sambamba na hayo maelezo hapo juu? Au nimalize kwanza ESB3 then ndio niwachanje?
Wape kwanza ESB3 then waachae kwa wiki moja then uwachanje mkuu....
 
Aisee kuku wangu wanapooza miguu na kufa ndani ya siku moja je ni ugonjwa gan nawapa ile dawa nahic inaitwa t.o.c niliambiwa ni ant-biotic (cjui ndio hvy) lakin aikufanikiwa wanakufa daily.
 
Dr uko vizur sana katika kutoa ushaur kwa wafugaji nakupongeźa kwa hilo majibu yako yanaonesha vet.uliisoma vizur na pia ujuzi wa mtaani umekusaidia sanaa kutatua changamoto mbalimbali za mifugo ilaa ningeomba unapowashaur wafugaji ni vyema ukawaambia watafute watàalamu wa mifugo ili wakajiridhishe kabla ya kununua dawa na kutibu in medicine kuna kauli wanasema telephone diagnosis is not always rewarding .
 
Hello..... Karibuni Sana Katika group linalohusu ufugaji wa nguruwe

Karibu Sana wewe mtaalamu wa mifugo, mfugaji, mnunuzi, pamoja na Wale wenye kiu ya kujifunza zaidi kuhusu ufugaji huu wenye tija na kipato cha uhakika.....

Click link ifuatayo kujiunga......

Zingatia kujitambulisha pindi tu uingiapo katika group hili
ZINGATIA KUJITAMBULISHA PINDI TU UINGIAPO KATIKA GROUP HILI... JINA, MKOA, SHUGHULI

TSA- PIG FARMING
 
Mkuu nakushukuru kwa kujitoa kwako kuwashauri wafugaji katika nchi hii. Huu ndio uzalendo wa kweli unaopaswa kuigwa na kila mtanzania mwenye mapenzi mema. Ubarikiwe sana.
 
Link haifungui
Screenshot_20180505-171339.jpg
 
Dr nataka kuanza Kufuga Kuku was nyama naomba ushaur Kuku aina gani ni wazuri na vifaranga vyake navipata WAP mm npo sumbawanga
Broiler aina ya cornish cross breed wako vizuri....

Na vifaranga wazuri kachukue euro poultry hawa wako maeneo ya airport au mkuza chicks hawa wako ubungo hapo....
 
Mkuu nakushukuru kwa kujitoa kwako kuwashauri wafugaji katika nchi hii. Huu ndio uzalendo wa kweli unaopaswa kuigwa na kila mtanzania mwenye mapenzi mema. Ubarikiwe sana.
Nashukuru sana mkuu na karibu sana...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom