GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,872
"Nilikuwa naliangalia lile tukio zima ila nilipoona tu ghafla Msanii Harmonize anapita juu kwa ile Kamba kama Mtu wa Medani nilichukizwa mno kwani hakuonyesha hata tu 5% ya kwamba Yeye ni Mjeshi na alikosea mambo mengi ya Kimsingi sana huku ile tua yake kama Gunia la Viazi Mbatata limerushwa kutoka katika Lori, kutupa Bendera huku akihema hadi kupatwa na Kizunguzungu liliharibu kila Kitu. Rai yangu tu kwa hawa Wasanii waache Kujiita Majina ambayo hayaendani nao Kiuhalisia na bora ya hata huyu sijui Diamond anavyojiita Simba kwani ni kweli kabisa ukimuangalia mambo mengi ni makubwa na ya Kujiamini kama alivyo Simba halisi"
Haya mnaopingana na huyu Mtaalam wa Kijeshi jitokezeni mtoe Hoja zenu za Maana na wale mnaomuunga mkono karibuni katika Kumpongeza tu.
Haya mnaopingana na huyu Mtaalam wa Kijeshi jitokezeni mtoe Hoja zenu za Maana na wale mnaomuunga mkono karibuni katika Kumpongeza tu.