Mtaalam, mwenye uwezo na mzoefu wa kuongea na maruhani anahitajika

Bainisha umri wa kiti? Nikufanyie kazi yako chapu kwa uzoefu nilionao kwa mambo hayo, sitaki hata mia yako. Maana naweza poteza kila kitu endapo nitapokea hata senti yako kwa kazi hiyo. Kwa kuwa unataka kufunuliwa siri za ulimwengu na milimwengu.
 
Marauhani ni majini yaliokoka yanaomwamini mungu. Kama walivyo baadhi ya binadamu wanaotii amri za mungu. Hadi wanafikia makamu yakutambulika kama ma nabii au ma walii. Ndio hali ya majini. Nadhani kwa ufupi umenielewa
heeee makubwa!
Hii mpya kwangu ndo nasikia leo
 
Daah! kuna ndugu yake babu mmoja (R.I.P) alikuwa anaweza kufanya hiyo kazi aisee, Mzee yule hakuwahi tangu namjua sikuwahi kumuona anashikwa kiu ya kunywa maji( yaaani maji kwake ni kesi/sumu ilikuwa kwa mujibu wa maruhani yake,,,, na chakula alichokuwa anaweza kula ni ubwabwa pekeee). Yaani huyu Mzee alikuwa akifika sehemu anaweza kusema kuwa hapa leo hapako sawa au mambo yako vizuri. Kuna dada etu mmoja alikuwa anaweweseka sana mara maruhani yapande basi mzee anaongea nayo. Ikatokea kuwa kuna kajamaa kuwa ndiyo inatakiwa kamuoe huyo sista lakini Mzee akachungulia akasema huyu dogo Mungu amemuandaa kuwa Mchungaji na tunavyoongea Jamaa ni Mchungaji huko Rock City na Dada yeye amebakia kutanga tanga tuu na wanaume yaani.
Kwa kweli ungepata msaada kutoka kwa huyu Mzee maana ametafasiri ndoto &kuwatuliza sana akina KITI na jamii yao.
Pamoja na hayo,lkn alikuwa anatumika upande wa giza!
Zinaitwa roho za utambuzi!
Na alimpishanisha huyo dada na(mume) huyo mchungaji,walijua akiolewa nae na hayo maruhani,majini yangetoka! Nuru na giza havikai pamoja!
 
Wana Body, anahitajika mtaalam, mwenye uzoefu na mwenye uwezo wa kuongea na MARUHANI, atalipwa kwa kazi hii ya masaa machache au lisaa tu. swala hili ni nyeti sana kuna mazungumzo ya kina na maswali na majibu yatahitaji kujibiwa na kuulizwa.

Anaye mfahamu mtu huyo tafadhali msaada ni kwa nia njema sana maana kuna mambo yanahitaji ufafanuzi.

Karibuni mwenye uwezo mkubwa na caliber hiyo haya ni mazungumzo ya ana kwa ana.
Kitakachofanyika hapo,huwa wanaangalia hayo majini yana uwezo gani,halafu wanayatuliza kwa kukuingizia yenye nguvu zaidi!
You need Jesus!Yesu atayatoa hayo atawekwa huru sio kuyasikiliza yanataka nn,ni ujinga mtupu!
Kitu in Yesu sio majini,maruhani!
 
Back
Top Bottom