Mtaa wetu utakukumbuka kwa muujiza ulioufanya hapa siku za mwishomwisho za uzima wako

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,276
14,511
lita 1000 ya maji ya Chumvi tulikuwa tunanunua Tsh 15000.

Tuliletewa na Gari na lenyewe hadi uwe unachukua kuanzia lita 3000.

Hadi unaondoka tunaipata mubashara kwa tap Lita 1000 T-sh Kama 1500. Punguzo la asilimia

Hatukuwahi kufikiri iko siku Muujiza utatokea maji yatiririke bafuni. Nilisimama kidete kubishana nap kada babu was CCM Kuwa rais katupiga fix tu ili apate kura Anachosema hakitekelezeki.

Nilikuwa nambishia kwa fact maana nilikuwepo awamu iliyopita tulipoona mbwembwe za wachina wenye kaundasuti za kungfuu wakisimamia kwa makeke yote mradi wa Maji ambao haukuwahi kutoa maji zaidi Yale mabomba yaligeuka chakula ya mchwa.

Nilistaajabu nilipopita serikali ya mitaa kukagua maendeleo ya mtaa wangu nilipokuta shehena ya mabomba ya blue Ya Maji (nchi 6+).
Sijakaa sawa baada ya kusafiri nakuta mbele ya maskani yangu yanazikwa mabomba na mtaro umechimbwa kitambo.

Nikamfata kada Mzee wangu nikamuuliza, "nini hiki?" mzee ananiambia "Dogo usiishi kwa mazoea hiki ni chuma, kikisema jambo lazima kitokee".

Leo mtaa mzima shida sio maji shida ni ujinga mkubwa wa kataasisi kalikopewa kutusambazia maji. Wanazidiwa ari na sisi wananchi.

Nakushukuru Mama nanii ulipoamaua Kwenda kuwatolea uvivu Ofisini ukijua hawawezi kuleta nyodo maana chuma kimeshika usukani. Fasta siku hiyohiyo wakaachilia maji hadi leo. Sina hakika kama wangekuwa na wepesi huo in absence ya chuma, Mwamba, hapa kazi tu.

Mwezi ujao nitakuja Chato hapo nione ulipolazwa maana jana nilipania nikuone lakini Wapo waliopania zaidi yangu hadi wakajikuta wanaunga mkono juhudi.

Ni hayo tu...
 
Hahaha nimependa hapo walipania hadi wameunga mkono juhudi

Binafs hicho chuma kwenye maendeleo ya vitu nakipa heko Sana si utani

Ila maendeleo ya watu ndio mtihan kwel kwel labda mama ata balance mambo

Afungue na uhuru wa kujieleza hasa demokrasia

# aliyesimama mbele yenu n Rais mwenye maumbile ya kike tu
 
Africa tuna kazi sana haki inafanywa hisani maji safi na salama kuletwa ulipo ni huduma ya kimsingi kwa binadamu yoyote na ni jukumu la serikali..

Ninapokua ughaibuni huku na ninaona niliyoyaacha miaka 19 huko iliyopita huko nyimbani ni yale yale napata wasiwasi sana kusikia mtu anasema "mabeberu wanatuonea wivu "

Hivi inawezekanaje mtu ana umeme wa kutokana na nyuklia, upepo ,gesi nk na bado halali kuzidi kuongeza ziada yake ashindane na mtu ambaye baada ya miaka 60 anapata maji na kuona ni tukio la kustaajabisha na la kuhitaji sherehe kabisa?
 
Picha ya mabomba na mitaro?
Mkuu tuchimbue tena!!!
Hawako kwenye project tena sasahivi ni operation. Labda Picha ya control number kulipia bili
Africa tuna kazi sana haki inafanywa hisani maji safi na salama kuletwa ulipo ni huduma ya kimsingi kwa binadamu yoyote na ni jukumu la serikali..

Ninapokua ughaibuni huku na ninaona niliyoyaacha miaka 19 huko iliyopita huko nyimbani ni yale yale napata wasiwasi sana kusikia mtu anasema "mabeberu wanatuonea wivu "

Hivi inawezekanaje mtu ana umeme wa kutokana na nyuklia, upepo ,gesi nk na bado halali kuzidi kuongeza ziada yake ashindane na mtu ambaye baada ya miaka 60 anapata maji na kuona ni tukio la kustaajabisha na la kuhitaji sherehe kabisa?
Liloshindikana miaka 60 au siku 21,960 limefanyika kwa siku 30.
 
Picha ya mabomba na mitaro?
Mkuu tuchimbue tena!!!
Hawako kwenye project tena sasahivi ni operation. Labda Picha ya control number kulipia bili
Africa tuna kazi sana haki inafanywa hisani maji safi na salama kuletwa ulipo ni huduma ya kimsingi kwa binadamu yoyote na ni jukumu la serikali..

Ninapokua ughaibuni huku na ninaona niliyoyaacha miaka 19 huko iliyopita huko nyimbani ni yale yale napata wasiwasi sana kusikia mtu anasema "mabeberu wanatuonea wivu "

Hivi inawezekanaje mtu ana umeme wa kutokana na nyuklia, upepo ,gesi nk na bado halali kuzidi kuongeza ziada yake ashindane na mtu ambaye baada ya miaka 60 anapata maji na kuona ni tukio la kustaajabisha na la kuhitaji sherehe kabisa?
Liloshindikana miaka 60 au siku 21,960 limefanyika kwa siku 30.
 

Similar Discussions

5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom