Mtaa wa Mshume Kiyate zamani mtaa wa Tandamati

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,839
30,168
Ukweli ni kuwa Mtaa wa Mshute Kiyate haupo kwa sababu wahusika wamekataa kubadili kibao cha jina sasa yapata zaidi ya miaka 20.

Kitwana Kondo
alipokuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ndiye aliyefanya mabadiliko ya majina ya mitaa kuwaenzi wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika kwa kuipa majna yao ile mitaa waliokuwa wakiishi.

Hivyo ndivyo Mtaa wa Kipata ujabadilishwa na kuitwa Mtaa wa Kleist Sykes, Mtaa wa Somali ukaitwa Omari Londo, Mtaa wa Aggrey ukaitwa Max Mbwana, Pugu Road ikaitwa Barabara ya Mwalimu Nyerere, Bi. Tatu binti Mzee akapata mtaa Ilala na Mtaa wa Tandamti ukabadilishwa jina na kuitwa Mtaa wa Mshume Kiyate.

Lakini palizuka malalamiko kuwa kilichomsukuka Kitwana Kondo kubadili majina ni hisia za udini. Hii ni baada ya kuonekana wazalendo wengi waliopewa majina ya mitaa ni Waislam.

Magazeti yakahoji ni michango gani wazalendo hawa walitoa? Kitwana Kondo katika mahojiano aliyofanya na marehemu Sarah Dumba wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) alijibu kwa kusema, ''Ikiwa hamjui michango ya watu hawa ulizeni mtaelezwa.''

tAZ7Q0CbeIpy9U9VrFhQRXVT3KiZoLVWyGRWVQGRN9MQ2MWqQTn6Pdw3hADo7z3DvALdD5Hr-xQ=w724-h567-no

Kushoto: Mwinjuma Mwinyikambi, Max Mbwana Julius Nyerere
na Mshume Kiyate Uchaguzi Mkuu wa 1962

2016%2B-%2B1

Mtaa wa Mshume Kiyate katika mihangaiko ya kutafuta rizki nyakati za
mchana wakati wa kutafuta rizki

20160524_142811.jpg

Mtaa wa Mshume Kiyate karibu na Soko la Kariakoo kama unavyoonekana
hivi sasa
 
Sifuatilia sana hoja zako ila chache nilizofuatilia lazima kuwe na chembechembe za dini ndani yake........ila shukrani kwa taarifa, natumai wahusika watabadili hilo jina.
 
Mzee wangu, Mohamed Said, tatizo la kutoweka historia yetu kimaandishi ama lilifanywa makusudi kwa ajili ya manufaa ya kundi fulani au hatukuona umuhimu wa kuandika kwa wakati ule. Nashauri, kupitia kwako na wenzako mliokuwepo kipindi kile, timizeni wajibu, tuandikieni katika weledi na ukweli wote na wala msichoke. Kazi za kitaalam haziozi. Tutasoma tutajifunza na kuelimika zaidi.
 
Sifuatilia sana hoja zako ila chache nilizofuatilia lazima kuwe na chembechembe za dini ndani yake........ila shukrani kwa taarifa, natumai wahusika watabadili hilo jina.
Sifongo,
Waliotaka kuifuta historia ya wazee wangu walisukumwa na dini.
 
Mzee wangu, Mohamed Said, tatizo la kutoweka historia yetu kimaandishi ama lilifanywa makusudi kwa ajili ya manufaa ya kundi fulani au hatukuona umuhimu wa kuandika kwa wakati ule. Nashauri, kupitia kwako na wenzako mliokuwepo kipindi kile, timizeni wajibu, tuandikieni katika weledi na ukweli wote na wala msichoke. Kazi za kitaalam haziozi. Tutasoma tutajifunza na kuelimika zaidi.
Iza,
Historia ya wazee wetu imehifadhika.
 
Mzee wangu, Mohamed Said, tatizo la kutoweka historia yetu kimaandishi ama lilifanywa makusudi kwa ajili ya manufaa ya kundi fulani au hatukuona umuhimu wa kuandika kwa wakati ule. Nashauri, kupitia kwako na wenzako mliokuwepo kipindi kile, timizeni wajibu, tuandikieni katika weledi na ukweli wote na wala msichoke. Kazi za kitaalam haziozi. Tutasoma tutajifunza na kuelimika zaidi.
sioni kivipi kunaweza kuwa na makusudi ya kutokuandika historia, kwani kuna mtu au hata hao wazee alikatazwa kuandika?
 
sioni kivipi kunaweza kuwa na makusudi ya kutokuandika historia, kwani kuna mtu au hata hao wazee alikatazwa kuandika?
jMali,
Kwa mara ya kwanza nilipoandika historia ya TANU katika gazeti la
Africa Events (London) hii ilikuwa mwishoni mwa miaka ya 1980.

Toleo lote lilipotea kimaajabu kwa wauzaji.

Kwa mara ya kwanza waliowahi kulinunua toleo lile walisoma historia
ya Abdulwahid Sykes kama chachu ya kuundwa kwa TANU.

Watu waliaminishwa kuwa TANU iliundwa na Nyerere 1954 na historia
ilikuwa ikiandikwa hivyo.

Haya ni kwa ufupi tu kuna mengi.
 
Ukweli ni kuwa Mtaa wa Mshute Kiyate haupo kwa sababu wahusika wamekataa kubadili kibao cha jina sasa yapata zaidi ya miaka 20.

Kitwana Kondo
alipokuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ndiye aliyefanya mabadiliko ya majina ya mitaa kuwaenzi wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika kwa kuipa majna yao ile mitaa waliokuwa wakiishi.

Hivyo ndivyo Mtaa wa Kipata ujabadilishwa na kuitwa Mtaa wa Kleist Sykes, Mtaa wa Somali ukaitwa Omari Londo, Mtaa wa Aggrey ukaitwa Max Mbwana, Pugu Road ikaitwa Barabara ya Mwalimu Nyerere, Bi. Tatu binti Mzee akapata mtaa Ilala na Mtaa wa Tandamti ukabadilishwa jina na kuitwa Mtaa wa Mshume Kiyate.

Lakini palizuka malalamiko kuwa kilichomsukuka Kitwana Kondo kubadili majina ni hisia za udini. Hii ni baada ya kuonekana wazalendo wengi waliopewa majina ya mitaa ni Waislam.

Magazeti yakahoji ni michango gani wazalendo hawa walitoa? Kitwana Kondo katika mahojiano aliyofanya na marehemu Sarah Dumba wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) alijibu kwa kusema, ''Ikiwa hamjui michango ya watu hawa ulizeni mtaelezwa.''

tAZ7Q0CbeIpy9U9VrFhQRXVT3KiZoLVWyGRWVQGRN9MQ2MWqQTn6Pdw3hADo7z3DvALdD5Hr-xQ=w724-h567-no

Kushoto: Mwinjuma Mwinyikambi, Max Mbwana Julius Nyerere
na Mshume Kiyate Uchaguzi Mkuu wa 1962

2016%2B-%2B1

Mtaa wa Mshume Kiyate katika mihangaiko ya kutafuta rizki nyakati za
mchana wakati wa kutafuta rizki

20160524_142811.jpg

Mtaa wa Mshume Kiyate karibu na Soko la Kariakoo kama unavyoonekana
hivi sasa
Na mtaa wa Pemba ulipewa jina la Mwl Sakina Mohamed Arab, lkn nao bado umebaki na jina lake la zamani!!
 
Sifongo,
Waliotaka kuifuta historia ya wazee wangu walisukumwa na dini.




Hivi Mzee wangu Mohamed Said kwani wazee wako walikatazwa wasipige kelele pale walipokuwa wanaona historia yao inafichwa? Maneno yako yana ukakasi inaonekana kuna kitu unakificha hutaki kuweka wazi
 
Hivi Mzee wangu Mohamed Said kwani wazee wako walikatazwa wasipige kelele pale walipokuwa wanaona historia yao inafichwa? Maneno yako yana ukakasi inaonekana kuna kitu unakificha hutaki kuweka wazi
Makodinda,
Nitaanza na hili la mwisho.
Sina ninachoficha.

Yote niliyokusudia kusema nimeyasema katika kitabu changu,
''The Life and Times of Abdulwahid Sykes...''

Sisi hatuna hulka ya kupiga kelele.

Ndiyo maana unaona kwa miaka mingi hakuna aliyejua historia
ya kweli ya TANU.
 
sion kwa nn hili jambo liwe la kidin, mosi majina yanayotaka kubadilishwa pia yana muelekeo wa hayo yanayotaka kuwekwa pili historia ni historia jaman iko waz nyerere asingeweza pata uhuru mwenyewe hasa ikieleweka kua dar es salaam ilikua ya waislam yy alikua amesoma tu so kuna kutegemeana hakuna anayeweza sema nilifanya hili peke yangu ila kama historia ilivyo dunia nzima kiongoz ndio anapata all the credit sielew kwa nn watu wanaona hilo ni tatizo
 
Historia hii ilipotoshwa kama zilivyopotishwa historia zote duniani,kinachotakiwa ni kuusema ukweli kila unapopatikana.watawala ndugu zanguni hupenda historia iandikwe kwa kuhalalisha uwepo wao na hicho ndiyo kilichowapata wazee wetu,siyo tu wale wa Dar es salaam lakini hata huko vijijini,niliambiwa kule Biirabo,Nshamba,muleba kagera alikuwepo mzee kalyambabi,hajaelezwa popote.
 
Back
Top Bottom