Mswahili mzee Khamis Akida afariki

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
Kama mtakumbuka kile kipindi cha MALENGA wetu huyu mzee alikuwa hana mfano kwa kutoa narratives za kiswahili

sina la kusema zaidi ya Inna Lillah wa Inna Illahi Rajuun.Duh ninayo CD yenye nyimbo za Egyptia hapa na huyu mzee alikuwa kipenzi wa Egyptia kama mimi....ama kweli waswahili sasa hivi tunadondoka kama majani vile

Hawa ndio wazee ambao tulitakiwa tuwa hudumie lakini wapi!



bingwa wa kiswahili hamisi akida hatunaye tena
MTAALAMU wa Kiswahili nchini, Hamis Akida amefariki dunia na kuzikwa Dar es Salaam jana. Mzee Akida alifia nyumbani kwake Mkwajuni katika Manispaa ya Kinondoni. Alikuwa na umri wa miaka 94.
Ofisa Uhusiano wa Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), Mohamed Mwinyi aliliambia HabariLeo kuwa Akida alikuwa kiungo kikubwa cha lugha hiyo.
Alisema kutokana na mchango wake katika lugha hiyo, mwaka 1999 Baraza liliamua kumtunuku Nishani ya Utetezi wa Kiswahili.
Miongoni mwa michango yake ni pamoja na kutunga Kamusi ndogo ya Kiingereza kwa kushirikiana na Profesa Abdallah Safari, kusahihisha lugha, kutafsiri miswada mbalimbali na uandishi wa makala mbalimbali.

Kwa mujibu wa wasifu wa Akida uliopatikana Bakwata, alizaliwa Novemba 22, 1914 mkoani Tanga. Miongoni mwa nafasi alizowahi kushikilia ni pamoja na ile ya Mchunguzi au Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI).
Alianza masomo mwaka 1923 kwa kusoma Kiarabu na kisha alianza shule ya msingi mwaka 1925 hadi 1932 alipomaliza. Kati ya mwaka 1933 na 1934, alikuwa katika Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Tabora.

Alijiunga na Shirika la Posta na Mawasiliano ya Anga mkoani Tanga, mwaka 1935. Mwaka 1939 alihamishiwa Dar es Salaam ambako pamoja na mambo mengine aliyoyafanya, anakumbukwa kwa kuwa mchezaji mzuri wa mpira wa miguu na pia mwamuzi. Wasifu unaonyesha pia kuwa aliwahi kujiunga na Klabu ya Old Boys Sunderland (Simba) na baadaye alijiunga na klabu ya Yanga.
Alikuwa pia mpenzi wa muziki wa taarabu na aliwahi kuwa kiongozi wa The Egyptian Musical Club wakati wa harakati za kupigania Uhuru wa Tanganyika.
 
Kwa mtu yeyote anayeelewa Kiswahili na kukua akisikiliza vipindi vya redio vya lugha ya Kiswahili Tanzania hii ni habari ya pigo kubwa.Mzee Akida ametoa mchango mkubwa sana katika Kiswahili Tanzania na duniani kote.

Apumzike kwa heri.
 
lailah inlahlah Mohhammad rassulluallah....mwnyzi MUNGU amjalie al marhuum hamis bin akida..heri zake....

hakika kila nafsi itayaonja mauti..ila tunasikitika anakufa kabla hajaandika story za maisha yake[memoiors].....ni hasara kwa wazee wastaarab kama hawa wanatutoka hawajatuachia vitabu vya maisha yao..NATOA WITO KWA VIONGOZI NA VIONGOZI WETU WA KIJAMII WAANDIKE HISTORIA ZA MAISHA YAO!!!
 
mungu amlaze pahala pema peponi na tunashukuru mchango wako ktk taifa na daima tutaulinda na kuutumia na kwa mchango huu utakuwa hai milele japo mwili wako hautakuwa nasi

mie nnaona titlt ya thread haijakaa vyema au imewekwa kizushi makusudi.


kwa nini isisemwe mtaalamu wa kiswahili mzee khamis akida atutoka.


hii kidogo haijatulia tafadhali gmt iweke sawa usiwaingize watu majaribuni
 
......mungu amlaze pema peponi mzee Akida. Thank you for everything and Rest In Peace !!.

Hivi yule mzee mwingine aliyekuwa anaghani ktk kipindi cha malenga, somebody Khalfan nae yu wapi!????
 
Mzee Akida, mTanzania na mzalendo safi, aliyelitumikia taifa lake kwa uadilifu mkubwa bila ya makuu.

Ni mfano mzuri wa kuigwa na waTanzania. Mchango wako taifa litauenzi milele.

Mungu airehemu roho yake.

Kama kweli pangekuwepo na haki katika serikali yetu, ni watu kama huyu mzee ndio waliostahili tuzo za juu za taifa hili. Hata hivyo pengine tunaweza kupeleka mapendekezo yetu kwa wahusika, ili walishughulikie.
 
Allah amlaze pema peponi na Amsameh dhambi zake!!! Binafsi nilikutana na Huyu Mzee ktk Wazee ambao watendelea kukumbukwa maishani...

Ni vema kukumbuka MEMA yake na KUSAHAU Mabaya yake
 
Allah amlaze pema peponi na Amsameh dhambi zake!!! Binafsi nilikutana na Huyu Mzee ktk Wazee ambao watendelea kukumbukwa maishani...

Ni vema kukumbuka MEMA yake na KUSAHAU Mabaya yake

Mkuu Chuma. Atakumbukwa wapi? Kwa bahati mbaya hatuna utamaduni wa kuenzi watu kama hawa ambao mchango wao katika jamii inawezekana ukawa sawa kama sio kuushinda hao waliojikita katika siasa. Kama tumeshindwa akiwa miongoni mwetu, tutamkumbuka akiwa hayuko!

Mungu ailaze roho ya marehemu sehemu njema peponi.
 
Nimemfahamu mzee Akida tangu miaka ya themanini wakati huo alikuwa akiishi Chuo Kikuu eneo linaloitwa Ubungo flats. Wakati huo mimi sikuwa na umri mkubwa lakini ninaweza kumkumbuka huyu mzee hadi leo kutokana na upendo aliokuwa nao. MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA PEPONI.
 
Kama mtakumbuka kile kipindi cha MALENGA wetu huyu mzee alikuwa hana mfano kwa kutoa narratives za kiswahili

Hawa ndio wazee ambao tulitakiwa tuwa hudumie lakini wapi!
Mimi namkumbuka kwenye kipindi cha Mbinu za Kiswahili kwenye RTD ya enzi hizo kikiendeshwa na Alhaj Suleiman Hegga, waalikwa wakiwa Hamisi Akida, Abdubari Diwani, Jumanne Mayoka na mwingine wa nne simkumbuki.

RIP Hamisi Akida japo its 9 years latter.

P
 
Back
Top Bottom