MovingForward
JF-Expert Member
- Nov 10, 2009
- 489
- 49
Katika hali ya kufurahisha sana, muda mfupi uliopita Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limeridhia kwa kauli moja (100%) kuchomolewa kwa mswada wa usalama wa kuunda Baraza la Usalama wa Taifa uliowasilishwa na Mh Simba.
Hali Mh Simba akiwa amepigwa bumbuazi, ameurejesha muswada ukajadiliwe upya kweneye kamati.
Wakati akiwasilisha hoja yake, alimsifu Mwanasheria Mkuu wa serikali kwa namna alivyowezesha kukamilishwa kwa mswaada uliopigwa chini.
Ninahoji uwezo wa mwanasheria mkuu wa serikali. Naona hayupo makini kabisa.
Habari Leo
WABUNGE wameukataa muswada wa Baraza la Usalama wa Taifa wa mwaka 2009 kwa madai kuwa sheria ambayo ingetungwa ingemnyang'anya Rais wa Tanzania mamlaka ya kuamua mambo yanayohusu ulinzi na usalama wa nchi.
Wabunge hao wamedai kuwa, kama wangeukubali muswada huo, nchi isingekuwa na siri za masuala ya ulinzi na usalama kuwa watu wengi wangehusika kutoa uamuzi wa mambo hayo nyeti.
Wamesema, ulinzi ni amri, si suala la kupigiwa kura hivyo Rais wa Tanzania aachiwe mamlaka ya kuamua masuala ya ulinzi na usalama wa taifa.
Wabunge wamesema, baraza hilo si chombo cha mjadala na kupiga kura, ni cha kuamua.
Wametoa msimano huo bungeni wakati wanajadili Muswada wa Baraza la Usalama wa Taifa wa mwaka 2009 uliowasilishwa jana.
Msimamo huo wa wabunge ulimlazimisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Sophia Simba, aombe kuundoa na kuurudisha kwenye Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, Bunge limekubali.
Kiongozi wa shughuli za upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed, amesema, sheria ambayo ingetungwa kutokana na muswada huo ingeweza kusababisha Rais wa Tanzania apinduliwe.
Mohamed amesema, hakuna sehemu yoyote duniani inayopiga kura kuhusu masuala ya ulinzi hivyo muswada huo haufai.
"Suala la ulinzi ni time, ukichelewa dakika mbili umekosea" amesema Hamad wakati anazungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.
"Na ulinzi bwana ni amri...hakuna sehemu duniani ulinzi unapigiwa kura" amesema Hamad na kudai kuwa Baraza la Usalama wa Taifa lililopendekezwa kwenye muswada huo ni kubwa kuliko Baraza la Mawaziri.
Mbunge wa Ilemela, Anthony Diallo, amekataa kuunga mkono muswada huo huo kwa madai kuwa, Baraza la Usalama wa Taifa litakuwa kubwa sana, na utakuwa mzigo kwa walipa kodi na Serikali.
Diallo amelieleza Bunge kuwa, kitaalamu, watu saba hadi tisa tu ndiyo wanaoweza kutunza siri za Serikali, wakizidi utakuwa ni sawa na mkutano wa hadhara.
Amewaeleza waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge kuwa, muswada huo unahitaji kuboreshwa kwa kuwa unamnyang'anya Rais wa Tanzania madaraka yake.
Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo, amesema, Baraza la Usalama wa Taifa si kongamano au sehemu ya kujadiliana, ni mahali pa uamuzi.
Shellukindo amesema bungeni kuwa, Rais wa Tanzania ni Amiri Jeshi Mkuu, aachiwe madaraka yake ya kuamua kuhusu masuala ya ulinzi na usalama wa taifa.
Mbunge huyo amehoji, wakati Rais wa kwanza wa Tanzania , Julius Nyerere alipoamua taifa liingie vitani Kagera, kongamano gani lilikaa?
Mbunge wa Mtera, John Malecela amesema, muswada huo umewasilishwa bungeni wakati usio muafaka, ukarekebishwe, upelekwe bungeni wakati unaostahili.
Malecela ametaka Rais aachiwe madaraka ya kuamua kuhusu masuala ya ulinzi wa nchi na ameuliza, ni wapi Rais aliyechaguliwa anakuwa na kamati kubwa ya kumshauri kuhusu masuala ya vita.
Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai amesema, muswada huo una kasoro, haukutazamwa vizuri hivyo urekebishwe.
Mbunge wa Karatu, Dk Wilbroad Slaa amesema, muundo wa Baraza la Usalama wa Taifa ni lazima uwe mzuri, hivyo wahusika waangalie nchi nyingine wanafanya nini.
Msemaji Mkuu wa kambi ya Upinzani katika Wizara ya Utawala Bora, Shoka Hamis Juma, ameupinga muswada huo kwa madai kuwa kuwa si sahihi kuwa na sheria tatu za usalama wa taifa.
Kambi hiyo imetaka iwepo sheria moja tu ya usalama wa taifa kwa kuwa zikiwa nyingi zitatoa mianya ya kufanyika makosa.
Hali Mh Simba akiwa amepigwa bumbuazi, ameurejesha muswada ukajadiliwe upya kweneye kamati.
Wakati akiwasilisha hoja yake, alimsifu Mwanasheria Mkuu wa serikali kwa namna alivyowezesha kukamilishwa kwa mswaada uliopigwa chini.
Ninahoji uwezo wa mwanasheria mkuu wa serikali. Naona hayupo makini kabisa.
Habari Leo
WABUNGE wameukataa muswada wa Baraza la Usalama wa Taifa wa mwaka 2009 kwa madai kuwa sheria ambayo ingetungwa ingemnyang'anya Rais wa Tanzania mamlaka ya kuamua mambo yanayohusu ulinzi na usalama wa nchi.
Wabunge hao wamedai kuwa, kama wangeukubali muswada huo, nchi isingekuwa na siri za masuala ya ulinzi na usalama kuwa watu wengi wangehusika kutoa uamuzi wa mambo hayo nyeti.
Wamesema, ulinzi ni amri, si suala la kupigiwa kura hivyo Rais wa Tanzania aachiwe mamlaka ya kuamua masuala ya ulinzi na usalama wa taifa.
Wabunge wamesema, baraza hilo si chombo cha mjadala na kupiga kura, ni cha kuamua.
Wametoa msimano huo bungeni wakati wanajadili Muswada wa Baraza la Usalama wa Taifa wa mwaka 2009 uliowasilishwa jana.
Msimamo huo wa wabunge ulimlazimisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Sophia Simba, aombe kuundoa na kuurudisha kwenye Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, Bunge limekubali.
Kiongozi wa shughuli za upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed, amesema, sheria ambayo ingetungwa kutokana na muswada huo ingeweza kusababisha Rais wa Tanzania apinduliwe.
Mohamed amesema, hakuna sehemu yoyote duniani inayopiga kura kuhusu masuala ya ulinzi hivyo muswada huo haufai.
"Suala la ulinzi ni time, ukichelewa dakika mbili umekosea" amesema Hamad wakati anazungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.
"Na ulinzi bwana ni amri...hakuna sehemu duniani ulinzi unapigiwa kura" amesema Hamad na kudai kuwa Baraza la Usalama wa Taifa lililopendekezwa kwenye muswada huo ni kubwa kuliko Baraza la Mawaziri.
Mbunge wa Ilemela, Anthony Diallo, amekataa kuunga mkono muswada huo huo kwa madai kuwa, Baraza la Usalama wa Taifa litakuwa kubwa sana, na utakuwa mzigo kwa walipa kodi na Serikali.
Diallo amelieleza Bunge kuwa, kitaalamu, watu saba hadi tisa tu ndiyo wanaoweza kutunza siri za Serikali, wakizidi utakuwa ni sawa na mkutano wa hadhara.
Amewaeleza waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge kuwa, muswada huo unahitaji kuboreshwa kwa kuwa unamnyang'anya Rais wa Tanzania madaraka yake.
Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo, amesema, Baraza la Usalama wa Taifa si kongamano au sehemu ya kujadiliana, ni mahali pa uamuzi.
Shellukindo amesema bungeni kuwa, Rais wa Tanzania ni Amiri Jeshi Mkuu, aachiwe madaraka yake ya kuamua kuhusu masuala ya ulinzi na usalama wa taifa.
Mbunge huyo amehoji, wakati Rais wa kwanza wa Tanzania , Julius Nyerere alipoamua taifa liingie vitani Kagera, kongamano gani lilikaa?
Mbunge wa Mtera, John Malecela amesema, muswada huo umewasilishwa bungeni wakati usio muafaka, ukarekebishwe, upelekwe bungeni wakati unaostahili.
Malecela ametaka Rais aachiwe madaraka ya kuamua kuhusu masuala ya ulinzi wa nchi na ameuliza, ni wapi Rais aliyechaguliwa anakuwa na kamati kubwa ya kumshauri kuhusu masuala ya vita.
Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai amesema, muswada huo una kasoro, haukutazamwa vizuri hivyo urekebishwe.
Mbunge wa Karatu, Dk Wilbroad Slaa amesema, muundo wa Baraza la Usalama wa Taifa ni lazima uwe mzuri, hivyo wahusika waangalie nchi nyingine wanafanya nini.
Msemaji Mkuu wa kambi ya Upinzani katika Wizara ya Utawala Bora, Shoka Hamis Juma, ameupinga muswada huo kwa madai kuwa kuwa si sahihi kuwa na sheria tatu za usalama wa taifa.
Kambi hiyo imetaka iwepo sheria moja tu ya usalama wa taifa kwa kuwa zikiwa nyingi zitatoa mianya ya kufanyika makosa.