Msuya atueleze aliko Sokoine

Mwili wa marehemu kufanyiwa ama kutokufanyiwa uchunguzi, nalo ni swala la imani kiongozi?

Tafadhali tofautisha imani, ambayo ni hakika ya mambo yatarajiwayo na bayana ya mambo yasiyoonekana, na swala halisi kama la kupima ama kutokupima kama mtu kafa ama yuko hai. Hapo kweli kuna imani?

Please be realistic!.

umenisaidia mkuu huyu jamaa haelewi alichosema
 
Kipimo cha akili mbovu na ubongo rojo ni mambo ambao yanatokea vichwani mwetu. Tuna tabia za kijinga sana kujifanya tunajua SIRI ambazo ni ujinga mtupu. Mleta mada ni mmoja wa wale watu wanaolewa pombe na kudai wao ni USALAMA WA TAIFA. Yaani watanzania tuna shida!
Msuya amekemea ushenzi - fikra zako zilizo chini ya ubongo wako uliojaa kiza kinene ukakufunulia kuwa mtuhumu Msuya kuwa aliua sokoine! Akili na tabia yako vina utando wa buibui!

hii inaonyesha jinsi gani unavyokaribia kutuaminisha kuwa msuya alimua kipenz chetu. je mbona hujamjibu alitoa hoja kwamba sokoine walikataza asipimwe kama amekufa na yule aliyesema mwili ulikuwa na matundu? unasemaje basi kuhusu secretary wake aliyepotea ghafla? acha kuropoka povu tuliza akili jibu hoja.
 
Secretary wa Msuya, dada mmoja wa Kipare, alikuwa bado kijana tu, akisali pale Temeke Luth Church.
Dada huyu alikuwa na pacha mwenziwe, ALIPOTEA na asionekane tena katika uso wa dunia.
Sasa ni zaidi ya miaka 30 dad huyu hajaonekana.

Huyo dada alikuwa akiishi Tandika Magorofani, gorofa E. Alipotea ikiwa ni kipindi cha bajeti, wakifanya kazi hadi usiku. Binti aliacha mtoto mdogo kabisa ndo anajifunza kutembea. shame on this stupid Msuya.

Tunayo mengi ya hicho kipuuzi, Kimsuya.
 
Tunapokaribia kuadhimisha miaka 30 tangu kilipotokea kifo kilichojaa utata cha aliyekuwa Waziri Mkuu Ndg.Edward Moringe Sokoine,ni wakati mwafaka sasa kumhoji Mh.Cleopa Msuya juu ya tuhuma za kuhusishwa na kifo cha Mh. Sokoine;kwa sababu Mh. Msuya kwa siku za karibuni amejitokeza kukemea maovu mbalimbali yanayofanywa na viongozi wa CCM bila shaka pia atakuwa na ujasiri wa kujitokeza na kutolea ufafanuzi wa tuhuma hizi.

taarifa gani ilitolewa kupotea kwa binti huyo? au aliuawa au unadhan kitu gani kilimtokea huyo secretary
Huyo secretary, nikikumbuka jina akiitwa nafikiri Uzeeli, hajapatikana hadi leo, baada ya zaidi ya miaka 30.
Sina uhakika wa kuunganisha kupotea kwake na kifo cha Sokoine
 
mzee wako alichukiwa na kinana kwa rushwa zake akamuanzishia skendo ya tembo,,sasa naona baada ya mzee msuya kuusema ukweli mmemuanzishia ya sokoine,,, eti dawa kuwafunga watu midomo wasimguse mzee ambae ni mgonjwa,,,,kazi mnayo kuuza nyanya mbovu itakaaa kwenye friji hadi lini?? nasikia ata kamba za viatu haoni hadi avalishwe

Mimi siko upande wowote. Na kama ni mambo ya ufisadi, wote walaaniwe kwa upumbavu wao, lakini huyo Msuya naye asijidai. Ni mwizi fisadi na muuaji. Aeleze benki kuu ilichomwa na nani, aeleze benki hiyo ilikarabatiwa kwa kiasi gani, aeleze ujenzi wa Mtera alifaidikaje maana data tunazo na upuuzi wake.
 
Mimi nalia na Balali tu,huyu mtu mkubwa katika serikali leo anafia katika nchi ya ugenini halafu eti anazikwa kienyeji tu,hivi ni nini kilikuwa kinafichwa na sisi tukijue!
 
CCM ni genge la wauaji, mafisadi, majizi na ibilisi. wakati tunahoji kifo cha Sokoine tusisahau pia kuhoji kifo cha Kolimba na Dr Mvungi. CCM ni kikundi cha kigaidi kama vile alshaabab, bokoharam, janjaweed na vikundi vijngine kama hivyo.
 
Mnataka kuuleta yale mambo yenu ya kupakazia kama mlivyo mpakazia salimu ahmedi alimua karume.

REAL..... HAYA MACCM NI MACHAWI SANA. HAMTUPATI NG'''OOOO. SISI YETU UKAWA TUMEIPOKEA NA TUMEIELEWA. NATUTAKUWA WAAMINIFU KWAO. CCM MLIE TU NA UCHAWI WENU. MSUYA NI WENU PIA LOWASA NI WENU NA WOTE NI MAFISADI. WACHAWI WALA HATUTISHIKI KWANI TUKO IMARA NA UKAWA YETU

CCM NI WATU WABAYA SANA NYINYI. HATUTADANGANYIKA TENA NA SARAKASI ZENu..
 
Tunapokaribia kuadhimisha miaka 30 tangu kilipotokea kifo kilichojaa utata cha aliyekuwa Waziri Mkuu Ndg.Edward Moringe Sokoine,ni wakati mwafaka sasa kumhoji Mh.Cleopa Msuya juu ya tuhuma za kuhusishwa na kifo cha Mh. Sokoine;kwa sababu Mh. Msuya kwa siku za karibuni amejitokeza kukemea maovu mbalimbali yanayofanywa na viongozi wa CCM bila shaka pia atakuwa na ujasiri wa kujitokeza na kutolea ufafanuzi wa tuhuma hizi.

Ndugu yangu Mleta mada angalia tena vyanzo vyako vya habari kuhusu Kifo cha Marehemu Sokoine,Hizi taarifa unaloleta humu zinasababisha usumbufu kwa baadhi ya ndugu na jamaa wa Marehemu na sisi wengine ambao tunawafahamu hao Wazee wote na utumishi wao Serikalini.Jioni ile ya Jumatano,April 12/1984 pale Wami-Dakawa katika wilaya ya Mvomero,Mzee Sokoine alikufa katika ajali ya kawaida kabisa ya gari? Nasema hivi kwa sababu tulikuwa katika msafara ule.Kulikuwa na makosa yaliyofanywa na gari lililokuwa linakuja upande wa pili,ambalo lilikuwa linaendeshwa na Mkimbizi Dumisani Dube.Gari hilo liliserereka na kugonga gari la Waziri Mkuu,Upande aliokuwa amekaa Sokoine,na wakati huo inasadikiwa Marehemu alikuwa amelala.Mara tu baada ya ajali ile Mkimbizi yule alishikiliwa na vyombo vya usalama.Marehemu Sokoine aliiingizwa kwenye gari Jingine na kukimbizwa Hospitali ya Mkoa,Morogoro mjini.Hakuna aliyeweza kusema pale kwenye ajali ambayo ilitokea saa 10 jioni kama Waziri Mkuu alikuwa Hai au Amekufa.Habari za kifo zilithibitishwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na maelezo yake yalisema Waziri Mkuu alifariki kwenye ajali.

Hizi habari unazoziandika hapa kwamba Mzee Msuya anahusika kwa namna moja ama nyingine hazina ukweli wowote.Marehemu Sokoine alifariki katika ajali ya barabarani.Kuandika habari kama hii unaleta sintofahamu,umemuhusisha Mzee Msuya na tukio jingine la kupotea kwa secretary wake karibu miaka 30 iliyopita,siwezi kulisemea hilo kwa sababu ni mara yangu ya kwanza kulisikia.Lakini naomba usielekeze tuhuma hizi nzito kwa sababu tu ya misimamo tofauti ya Kiitikadi.Mzee Msuya kama wewe anaweza kusema lolote kuhusu hizi harakati za baadhi ya Watanzania kuwania nafasi ya Urais, hana upendeleo wowote kwenye mchakato huu,mwisho wa siku ana kura yake moja tu.Nipo wazi kukosolewa lakini nimeamua kuandika hili kwa makusudi ili tusiifanye forum kama kijiwe cha kuchafua Watanzania wenzetu!
 
Wanabodi,
Mwaka wa uchaguzi ndio huu. Wadau wameanza kufunguka . Tunaomba hints zaidi mwenye walau uelewaa
 

Attachments

  • 1420736485520.jpg
    1420736485520.jpg
    29.4 KB · Views: 6,375
Huyo dada alikuwa akiishi Tandika Magorofani, gorofa E. Alipotea ikiwa ni kipindi cha bajeti, wakifanya kazi hadi usiku. Binti aliacha mtoto mdogo kabisa ndo anajifunza kutembea. shame on this stupid Msuya.

Tunayo mengi ya hicho kipuuzi, Kimsuya.

mkuu machoz yananitoka kikweli watu wachafu sana
 
mze umeeleweka ila ni kutaka kujua kimetokea nin hasa siku ile wala hatupuuzi kama msuiya alifanya hujuma ya kuseti kifo cha sokoine alaf ccm tunajua kwa mauaji ya watu waadilifu na kuwaacha wahalifu siwez kumuamini kiongoz wa ccm
 
Mbona uko na akili kama za nguruwe?unasema alomuua sokoine huyu hapa halafu unataka tukusaidie.!!!!!nenda mirembe si bure
 
Kibanda anataka kuanzisha zogo na ubishi ambao hautakuwa na mwisho. Kibanda huu ni unafiki na upunguani wa daraja la juu kutoa tuhuma nzito kama hizi kwa sababu na manufaa yako binafsi. Ukiambiwa upeleke ushahidi ili tuhuma zichunguzwe utaanza kulalama unafuatwa. Stop this irresponsible writing . All you want is to start a political battle on the social media front and i am sure the aim is purely to settle political scores! You are better than this Kibanda, usijifanye mjinga!
 
Back
Top Bottom