Msukuma awajibu January na Nape asema kumkosoa hayati Magufuli ni nongwa kwa sababu wabunge wamekula viapo vya utii

Waliapa kwa Jiwe au Bungeni?
Ndiyo ujue kwamba shule ni muhimu! Msukuma anapodai viapo vinaendelea hajui anachoongea. Yeye aliapa mbele ya Spika Ndugai....Lakini Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu, Manaibu K/ Wakuu na Wakurugenzi waliapa na wataendelea kuapa mbele za Rais!!!!
Ndiyo maana Mama Samia ameanza panguapangua kuweka safu yake watakao apa mbele yake. Kiongozi yeyote aliye apa mbele ya Hayati JIWE ni BATILI!
 
Bunge linaweza kumuondoa waziri mkuu na rais . Swala la utii labda kwa mungu sio kwa binadamu.
Nyie ndo huwa mkiingia anga za watu mnakula za kutosha, kumtii Mungu ni kwny bible ila kwny katiba ipo kumtii mkuu wako. Kama unajua kwmb hakuna mkubwa zaid ya Mungu bs achana na kaz zinazokulazimisha kula kiapo.
 
Kwahiyo kwakuwa mmeapa kutotoa Siri na mmepita kwenye uchaguzi, hata yakitendeka maovu msiseme siyo?
Kuwa ccm ni kubeba
Wabunge wa CCM ni wapuuzi sana na hawajielewi!
Kama ulimsikia Kibajaj Lusinde(Mtera) jana utajua kabisa kwanini alitetea kwa nguvu sana Hayati Magufuli kutosemwa vibaya, nimnukuu, "NAJITOA MHANGA LEO, WABUNGE WENGI TUKO HAPA KWASABABU YA RAIS MAGUFULI! UCHAGUZI MWAKA JANA ULIKUWA MGUMU SANA NA WENGI WETU HALI ILIKUWA MBAYA SANA MAJIMBONI..."
Hii manake ni kuwa Lusinde na Wabunge wa WABUNGE WENGI WA CCM HAWAKUSHINDA KIHALALI. Kwa maana hiyo Hayati Magufuli alichakachua na kuiba kura kama zote ili CCM ishinde kwa gharama zozote...!!!
 
Umeishia darasa la ngapi?
Sometimes soma Kwanza comments kabla ya kujibu...kumbe hujui ni nini nimeandika
La 7 tu Msukuma! Lakini hii 👇👇 comment yako itasumbua hata profesa Muhongo, bwana akili kubwa
“CHadema walikuwa jumba bovu ndani ya Bunge na sasa hawapo hizi sarakasi zitaendelea kilasiku”
 
Hili bunge limejaza mataahira haswa, hivi kuna kiapo kinazuia watu kukosoa pale wanapoona kuna mambo hayaendi sawa? Bunge mfu lenye sheria bubu na viongozi vipofu.

kajifunze maana ya utii,sio unashandadia tu.

ndio maana wenzako wanakomaa na katiba mpya ya jamhuri,katiba hii imeruhusu rais awe mwenyekiti wa ccm taifa,wabunge ambao ni wa ccm,wanawajibika kwake upande wa chama.

unaanzia wapi kukosoa!!!ndio maana nyimbo za kuabudu zimehamia kwa mama kwa sasa.
 
Viapo hivi vya kutomkosoa dikteta walikula lini na wapi? Na mwenye hicho kiapo atuwekee hapa.

sio dictator,sema mwenyekiti wa ccm taifa.


kama unazungumzia wabunge wa upinzani sawa.
 
Hesabu zinazotumika na kina jk ni kali sana, hawa lasaba b hawatakuja kuamini macho yao! hao wanao wasema muda siyo mrefu watakuja kuwa mabosi wao. Hapo wametulizwa tu ila game itavyo change wasije kulialia.

msukuma alie,halafu wewe utakuwa na hali gani???

ngosha yule mbali na ubunge pia ana hela.
ikifikia hatua analia yule wewe umekata moto tayari.
 
Inasikitisha sana kuwa na wabunge mfano wa huyu msukuma,na hawa ndio walikuwa waamuzi wasaidizi wa meko.
Badilikeni bana ni enzi mpya chini ya mama Samia.
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Msukuma amesema kuna wabunge wanadai kumkosoa hayati Magufuli siyo nongwa lakini sisi tunasema ni nongwa kwa sababu wabunge tumekula kiapo cha utii.

Msukuma alikuwa anampa taarifa mbunge wa makambako mh Jah people aliyesema wabunge wameingia bungeni kwa nguvu ya hayati Magufuli na wasaidizi wake mama Samia na mh Majaliwa Jah people amesisitiza waliokosa teuzi wawe wavumilivu kwani wabunge ni wengi vyeo ni vichache.

Hayo ni majibu murua kwa wabunge waliopitishwa bila kupingwa January Makamba na Nape Nnauye.

Ramadhan Kareem!
Daah 🤔 kazi ipo!!
 
kajifunze maana ya utii,sio unashandadia tu.

ndio maana wenzako wanakomaa na katiba mpya ya jamhuri,katiba hii imeruhusu rais awe mwenyekiti wa ccm taifa,wabunge ambao ni wa ccm,wanawajibika kwake upande wa chama.

unaanzia wapi kukosoa!!!ndio maana nyimbo za kuabudu zimehamia kwa mama kwa sasa.
Hilo la uenyekiti wa ccm linahusu katiba ya nchi au ya chama? Pia, utii huo ambao jamaa anatakiwa kujifunza, ni kwa rais aliyepo au mwendazake?
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Msukuma amesema kuna wabunge wanadai kumkosoa hayati Magufuli siyo nongwa lakini sisi tunasema ni nongwa kwa sababu wabunge tumekula kiapo cha utii.

Msukuma alikuwa anampa taarifa mbunge wa makambako mh Jah people aliyesema wabunge wameingia bungeni kwa nguvu ya hayati Magufuli na wasaidizi wake mama Samia na mh Majaliwa Jah people amesisitiza waliokosa teuzi wawe wavumilivu kwani wabunge ni wengi vyeo ni vichache.

Hayo ni majibu murua kwa wabunge waliopitishwa bila kupingwa January Makamba na Nape Nnauye.

Ramadhan Kareem!
Kushabikia CCM inabidi uwe na PHD ya uanfiki!
Utii ndio Nini....!
Ama kweli huyu ni Darasa 7 !
Ila inashangaza anapopata wafuasi na washangiliaji!
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Msukuma amesema kuna wabunge wanadai kumkosoa hayati Magufuli siyo nongwa lakini sisi tunasema ni nongwa kwa sababu wabunge tumekula kiapo cha utii.

Msukuma alikuwa anampa taarifa mbunge wa makambako mh Jah people aliyesema wabunge wameingia bungeni kwa nguvu ya hayati Magufuli na wasaidizi wake mama Samia na mh Majaliwa Jah people amesisitiza waliokosa teuzi wawe wavumilivu kwani wabunge ni wengi vyeo ni vichache.

Hayo ni majibu murua kwa wabunge waliopitishwa bila kupingwa January Makamba na Nape Nnauye.

Ramadhan Kareem!
viapo vyao nii kwa mungu au mwanadamu,,vitabu walivyoshika ni vya wanadaamu
 
Back
Top Bottom