MSOMAJI RAIA: USALAMA wa TAIFA (TISS) ndiyo "... kamati ya ufundi" YA siasa za CCM, tufanyeje?

Status
Not open for further replies.
piga kura linda kura!arusha,ubungo,arumeru n.k wamefanikiwa iweje wengine washindwe?
 
siasa za ushindani za Chadema na CCM zimechangia sana kuichafua TISS. Hii ni kwa sababu chadema hawataki kukubari kwamba wanashindana kisiasa bali kuna mkono wa TISS unaowafanya wasiingie Ikulu. Fikra hii hata kama sio kweli inaaminika sana miongoni mwa wafuasi wa chadema na ndio wepesi kuichafua TISS kadri wanavyoona inatosha kuwajenga kisiasa.

msomaji Raia anataka tuamini kwamba TISS si chochote si lolote hata ikivunjwa leo nchi itakuwa salama zaidi?

what is the way forward.

wapo wanaosema TISS ivunjwe

wapo wanaosema CHADEMA ivunjwe.

Wapo wanagsema TISS na CHADEMA vifutwe.
 
Ila mleta mada kaTISS ketu kana nguvu hata CIA wanaquestion uwezo kalikonao kachombo hako. Tusikadharau jamani. Utulivu wa nchi ni mikakati makini inayofanywa na hivyo vijamaa ambavyo hapa jukwaani tunavidharau.

Vishkaji kiukweli ni hatari. Mi nina kajamaa kangu tumepiga nako shahada ya 1 pale UD kumbe kalikuwa kashushu bwana lakini huwezi amini hakuna aliyekajua hadi tunamaliza.

Siku moja nikakaona Mwanza kwenye msafara wa Pinda ndo nikajua ni kashushushu. Tusividharau aise vijamaa viko njema ile kichizi.

Mjenga,

wewe umebaki na taswira ya tiss ya 1949. Hivi mpaka leo hujiulizi meno ya tembo na twiga wamefikaje ugaibuni? Unachoshangaa ni hako kamjamaa kumlinda 'liwalo na liwe'. Hama kweli kazi tunayo!

Hakika nimejiuliza maswali mengi juu ya usalama wa nchi hii na kukosa majibu. Ukweli sitashangaa nchi kuwa sawa na the DRC. Kongo mambo yalianza hivi: Rais kujilimbikizia mali nje ya nchi , aliligawa jeshi baadhi wakamlinda na baadhi wakatumia bunduki zao kujilipa mishahara, walimu wakalipwa na wazazi mishahara, kwa ufupi nchi ikajiendesha yenyewe.

Imefika atua nafikiri maana ya serikali hata spati jibu! Hivi serikali genge la watu wachache wenye mamlaka kujilimbikizia mali au ni watu wachache waliopewa dhamana na wengi ili kulinda na kugawa sawa raslimali za taifa kwawananchi wake?

Hebu tujiulize kazi za Hossea wa takukuru ni zipi? Nini anachokifanya Rais kwa kutokutoa tamko lolote! mauaji ya Mwangosi? Kwa nini tume ya uchaguzi mpaka leo haiwezi kutoa idadi kamili ya kula za urais 2010?

Matokeo ya sensa yako wap? vitambulisho vya taifa??! Nachukia sana viongozi mnaojilimbikizia mali kwa mwanvuli wa amani yetu. Tiss rejesheni heshima ya aifa letu!" Fichueni haraka nani ameweka pesa zetu uswiss, Fichueni haraka nani aliyekuwa mmiliki wa dowarns....
 
TISS wanapimwa kwa mabaya tu hawana mazuri.

Kama Mwandishi anajua mabaya yao TISS basi na mazuri yao anayajua angeweka yote jamvini kisha kazi ya kuhukumu angetuachia wasomaji wake.
 
Intelijensia zote ulimwenguni wana dili na maslahi ya nchi kwanza, mbali ya ulinzi. Hii Tiss yetu inaona tunaachiwa mahandaki, wanyama wanaenda, wachache wanajilimbikizia....huku wamembonji.....halafu inatuhubiria amani kwa watu wanaokula mlo mmoja kwa siku...?!

Tiss inatakiwa ihidhinishe mkataba wowote wa nchi, baada ya kujiridhisha kupitia wataalamu wake kuwa makataba huo una maslahi kwa nchi...ndipo viongozi wausaini.....! SAsa unamlinda kiongozi na ving'ora viiingi anayejiuzia KIWIRA kwa bei cheee, halafu unatamba kama zuzu kuwa kazi inafanyika....!
 
huyo mwandishi si critical thinker na wala si great thinker bali ni great tenker kwani hajaeleza kinagaubaga hayo mabaya ya TISS,mimi nadhani ndugu zanguni wana jamvi tusiwe kama ng'ombe tuliokosa matumaini kwa kuendeshwa na tu na mawazo finyu ya mtu mmoja ati ndo tukafanya CONCLUSION ya hoja zake dhaifu kuwa ndio ukweli...Lazima tukubali ukweli hata kama ni mchungu kuwa HAKUNA NCHI INAYOWEZA KUWA SALAMA KAMA HAINA INTELLIGENCE COMPANY,unapoleta hoja dhaifu kuwa hao jamaa ni corrupt tunahitaji mifano dhahiri na sio tuhuma tu zisizo na msingi,nawaombeni wanajamvi wenzangu tufikiri vizuri kabla ya kuendeshwa na EMOTIONS na mawazo ya huyo mwandishi ambaye hajawahi kusifia utendaji wa serikali au taasisi yoyote ya serikali hata siku moja
 
huyo mwandishi si critical thinker na wala si great thinker bali ni great tenker kwani hajaeleza kinagaubaga hayo mabaya ya TISS,mimi nadhani ndugu zanguni wana jamvi tusiwe kama ng'ombe tuliokosa matumaini kwa kuendeshwa na tu na mawazo finyu ya mtu mmoja ati ndo tukafanya CONCLUSION ya hoja zake dhaifu kuwa ndio ukweli...Lazima tukubali ukweli hata kama ni mchungu kuwa HAKUNA NCHI INAYOWEZA KUWA SALAMA KAMA HAINA INTELLIGENCE COMPANY,unapoleta hoja dhaifu kuwa hao jamaa ni corrupt tunahitaji mifano dhahiri na sio tuhuma tu zisizo na msingi,nawaombeni wanajamvi wenzangu tufikiri vizuri kabla ya kuendeshwa na EMOTIONS na mawazo ya huyo mwandishi ambaye hajawahi kusifia utendaji wa serikali au taasisi yoyote ya serikali hata siku moja

hoja ya nguvu.
 
TISS imewajeruhi wengi naona wameamua kulipa kisasi kwa kupaka matope

Kimantiki mwandishi ana hoja lakini ina shutuma za jumla jumla kupita kiasi.
 
Uandishi wa namna hii ambao unalenga kulalamika tu mwalim nyerere alikuwa anauita uzuzu

Itawezekanaje tiss ndio wapendekeze majina ya ccm wakati ccm wenyewe wapo?kwa hiyo ccm ni robot?tusidanganyane hapa

Akili ya kuambiwa changanya na yako.aka mbayuwayu style.

Huyu mwandishi ningeambiwa nimchagulie jina ningemuita great sinker... Sababu ninazo,nia ninayo na uwezo ninao.

Mbaazi ikikosa maua husingizia jua.sasa hapa pia mwandishi amekosa la kuandika ameamua kuja na kulalamika style.mana uandishi wa namna hii ndio uliosababisha mauaji ya kimbari rwanda na waandishi walihukumiwa kunyongwa kwa matumizi mabaya ya kalam na uchochezi

Huwa napenda sana vituko vya ziro,yeye kila siku ni kuboronga tu.hii makala haina tofauti na majibu ya zero huwa anatoa majibu kwa kujiamini sana akiamini yuko sahihi kumbe ni mkorogo mtupu

Kwa tanzania ya leo huwezi kupata umaarufu bila kuitaja tiss so mwandishi nae anatafuta kula yake tusimlaum sana
 
Ila mleta mada kaTISS ketu kana nguvu hata CIA wanaquestion uwezo kalikonao kachombo hako. Tusikadharau jamani. Utulivu wa nchi ni mikakati makini inayofanywa na hivyo vijamaa ambavyo hapa jukwaani tunavidharau.

Vishkaji kiukweli ni hatari. Mi nina kajamaa kangu tumepiga nako shahada ya 1 pale UD kumbe kalikuwa kashushu bwana lakini huwezi amini hakuna aliyekajua hadi tunamaliza.

Siku moja nikakaona Mwanza kwenye msafara wa Pinda ndo nikajua ni kashushushu. Tusividharau aise vijamaa viko njema ile kichizi.

Kaka, hapo kwenye blue ndo ulipoharibu, yaani ufiti wao unausifia ni kuwa kwenye msafara wa Waziri mkuu? mbona hii nadhani ni level ya polisi tu, mi nilidhani unamifano ya jinsi gani walivyo fiti kudhibiti mambo kimataifa, kama watu wameweza piga dili za uhakika hadi Bank kuu na kuchuka pesa TISS hawana habari, tena zipo zipo deal zingine kama Deep Green Finance n.k hawa jama hawakua na habari then eti tuwasifu kwa kuwepo kwenye msafara wa PM? Aaah, hiki nacho ni kituko, mi sidhani kama kwenye msafara wa PM tulitakiwa kuweka Graduate! Mtu wa CCP Moshi alitosha kabisa, kwani hapa Tanzania, hasa ziara ya Mwanza inakitisho gani kwa usalama wa PM?
 
mwandishi angekuwa muwazi zaidi namna TISS wanavyotumika
Mkuu nitajaribu kufafanua kidogo lakini kwa kirefu!!

*Utendaji wa juu wa CCM huwa unashirikiana sana na idara nyeti za serikali(Dola) kama Polisi, TISS, JWTZ nk hii kutokana na historia na mfumo uliokuwepo yaani chama kushika hatamu, maana kikao cha juu cha maamuzi ya nchi yetu ni kamati kuu ya CCM(sio baraza la mawaziri), ndio maana usishangae vikao vya kamati kuu kufanyika Ikulu au vikahudhuriwa na mkuu wa majeshi, IGP, Mwanasheria mkuu, gavana wa BOT, Mkurugenzi wa PCCB nk.
ndio maana vinafanyika kwa siri sana tena wakati mwingine hata usiku wa manane.

*Ushindi wowote wa CCM katika uchaguzi mkuu ni lazima uratibiwe na vyombo vya dola(Polisi, TISS, JWTZ nk) kumbuka reaction ya Shimbo, Mwema, ZZoka wakati wa uchaguzi mkuu 2010 au Mahita na visu vya CUF 2000.

*CCM kwa sasa wako katika mpango mkakati mkubwa sana(Pigo la mwisho) kujiandaa kwa ''manoeuvre'' katika uchaguzi mkuu wa 2015 hivyo idara nyeti kama TISS lazima ihusishwe katika kutoa mapendekezo yake.

*Why Mangulla na Kinana?
Haya ni mapendekezo ya TISS kwa kushirikiana na Mkapa kwa sababu
1/Kipindi cha Mkapa ndio wakati ambao upinzani ulizimwa zaidi kimkakati Mangulla akiwa Katibu mkuu ikishirikiana na TISS.

2/Wakati wa chaguzi zote toka kuanza upinzani Kinana amekuwa kampeni manager wa CCM na ameshirikiana vizuri na TISS katika mipango ya kuchakachua na ilifanikiwa vizuri sana!!


Bahati mbaya sana ''This is hundred percent Edward Lowassa's Project.''
LOWASSA----TISS----MKAPA----KINANA-----PRESIDENCY.
 
msomaji Raia anataka tuamini kwamba TISS si chochote si lolote hata ikivunjwa leo nchi itakuwa salama zaidi?
Mkuu TISS wanafanyakazi gani kwa sasa?

Kama mamia ya wanyama wanatoroshwa kila siku nje ya nchi na TISS wako wanaangalia tu, kuna haja gani kuwa na hii taasisi?
 
Ila mleta mada kaTISS ketu kana nguvu hata CIA wanaquestion uwezo kalikonao kachombo hako. Tusikadharau jamani. Utulivu wa nchi ni mikakati makini inayofanywa na hivyo vijamaa ambavyo hapa jukwaani tunavidharau.

Vishkaji kiukweli ni hatari. Mi nina kajamaa kangu tumepiga nako shahada ya 1 pale UD kumbe kalikuwa kashushu bwana lakini huwezi amini hakuna aliyekajua hadi tunamaliza.

Siku moja nikakaona Mwanza kwenye msafara wa Pinda ndo nikajua ni kashushushu. Tusividharau aise vijamaa viko njema ile kichizi.

Kazi kwelikweli, kwahiyo kutomtambua wakati mkiwa shule ndo kigezo chako kuwa wanafanya kazi?. Unanikatisha tamaa ngugu yangu, mbona mimi mimesoma nao lakini hata uwezo wa kufikiri ni questionable?. Unawapa sifa zisizostahili hata kidogo,badala ya kufanya kazi kwa maslahi ya taifa kama inavyotakiwa, wanafanya kazi kwa maslahi ya CCM. Hawana issue yoyote kaka, angalia nchi za wenzetu wanavyofanya kazi, utapenda.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom