Msisitizo wa ulipaji kodi uendane na jamii kufahamu kwa undani umuhimu wake.

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,489
13,608
Mwaka 2014 mwezi March Uli Hoeness rais wa zamani wa klabu ya Bayern Munich alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kugundulika amekwepa kodi.

Alikiri mahakamani kwamba alikwepa kulipa jumla ya euro milioni 18.5 ambazo alipaswa kuzilipa kwa benki moja ya Uswisi, ambapo ameweka fedha zake. Kwa shabiki wa kawaida wa Bayern Munich na mjerumani mwenye kuifahamu vizuri historia na mchango wa Uli Hoeness kwenye soka, habari ya kufungwa kwake ilikuja na mshtuko kwa kuzingatia heshima aliyonayo.

Baada ya kutumia nusu ya muda wa kifungo, hatimaye mwaka 2015 akaachiwa huru. Hapa kuna funzo zito sana kwetu sisi watanzania. Tangazo la mheshimiwa rais hurudiwa tena muda ule ambapo watu wanajiandaa kuangalia taarifa ya habari ya kutwa nzima. Kuomba risiti ndio umekuwa utamaduni mpya.

Ikiwa mpaka mtoto mdogo wa darasa la kwanza anakwenda kununua gazeti mtaani halafu anaomba kupewa risiti maana yake anajengewa utamaduni wa kutambua mchango wa ulipaji kodi kwenye maisha yake. Ipo haja kwa TRA na serikali kwa ujumla kukuza zaidi ule utaratibu wa watu kufahamu kwamba ulipaji wa kodi sio mzigo.

Wajerumani walimsikitia Hoeness wakati akienda kutumikia kifungo cha miaka mitatu. Lakini hakuna mjerumani ambaye hafahamu maana ya yeye kuwa mlipa kodi. Kuna kila sababu kwa watu kupewa elimu pana zaidi ya faida za kodi. Rais anajenga hoja kwa kutumia mfano wa mrejesho wa fedha za kodi kwa faida ya kuboresha huduma za jamii. Lakini kodi inayokusanywa kutoka kwa watu wenye ufahamu wa maana na umuhimu wa ulipaji wake, inatumika zaidi ya kuboreshea huduma za kijamii.

TRA na serikali mnalo deni kubwa la kutoa elimu pana ya masuala ya kodi, ili sisi tunaofundishwa umuhimu wa kudai risiti, tusione kwamba ulipaji kodi ni mzigo maishani mwetu.
 
Kodi zetu ni nyingi kwa mfano, gari moja mv licence, sumatra, fire,mapato,vat,nenda kwa usalama.sasa huu ni mzigo wa kodi.
 
Kodi zetu ni nyingi kwa mfano, gari moja mv licence, sumatra, fire,mapato,vat,nenda kwa usalama.sasa huu ni mzigo wa kodi.
Na hizo taasisi zote ulizotaja zina kila sababu ya kufahamika kwa jamii, yaani zinafanya nini ambacho kinahalalisha uwepo wa zenyewe. Mlipa kodi anao uhuru wa kujua ni namna gani fedha anayotokea jasho inavyotumika.
 
Mlipa kodi anao uhuru wa kujua ni namna gani fedha anayotokea jasho inavyotumika.
Huwajui wabongo wewe kwa majibu, mara utaambiwa tunajenga mahakama za mafisadi.nk.piga kura nenda zako,lipa kodi nenda zako.usihoji ndio ukweli.
 
Suala la elimu ya mlipa kodi ni muhimu. Wananchi wanatakiwa kupewa elimu sahihi kuhusu kodi. Maana ya kodi na umuhimu wake kwa maendeleo ya nchi. Elimu hii ni bora ikawekwa kwenye mitaala ya somo la uraia kwa shule za msingi na kwenye somo la civics kwa elimu ya sekondari, GS kwa A level na DS kwa vyuo. Hii itawapa wanafunzi uelewa mkubwa kuhusu umuhimu wa kulipa kodi.
 
ila na michango ipungue, mara madawati, mara mwenge, mara choo cha shule mtuache tulipe kodi tu kama kwenye luku,vat, ewura, rea nk
 
Sio tu wafahamu umuhimu wake bali waone huo umuhimu in reality.
Haiwezekani unanikata kodi kwenye kila nachofanya alafu weekend unaniambia nifunge biashara yangu au niache shuhuli zangu niingie kusafisha mitaro ya jiji.
Hiyo kodi ninayolipa unaifanyia nini?
Umuhimu wa kulipa kodi niuone in real life na sio kunihubiria nadharia za kunifool kama mtu wa ushaghoo .
 
Sio tu wafahamu umuhimu wake bali waone huo umuhimu in reality.
Haiwezekani unanikata kodi kwenye kila nachofanya alafu weekend unaniambia nifunge biashara yangu au niache shuhuli zangu niingie kusafisha mitaro ya jiji.
Hiyo kodi ninayolipa unaifanyia nini?
Umuhimu wa kulipa kodi niuone in real life na sio kunihubiria nadharia za kunifool kama mtu wa ushaghoo .
Asante Daudi, kama upo Tanzania mwambie huyo Mama aliyekuuzia supu, akuongezee chapati nyingine, naongea na simu nikija nitamlipa. Haiwezekani uniambie nilipe kodi halafu sipati breakdown ya aina yoyote ile ya kile kinachotoka mfukoni mwangu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom