Nawasalimu wakuu!
Nimeguswa kuyasema haya kutokana na tabia ya watu wachache wenye viherehere humu JF vya kuponda baadhi ya opportunity zinazotolewa na wadau humu wenye mioyo ya huruma kwa wasio na kazi.
Kitu cha muhimu kumbuka HUNA KAZI hivo usidharau na kukashifu any opportunity, kutoridhika na nafasi iliyopo its okay, sawa hujaridhika basi endelea kusoma thread zingine sio kuponda manake kwa yule mwenye shida utamkwaza kuikubali ile nafasi. Isitoshe kazi ni heshima hata kama hailipi ila unaamka unaoga asubuhi, mkaa bure sio sawa na mtembea bure, mtembea bure huenda akaokota.
Katika safari yenu ya kutafuta kazi naomba niwashauri machache
1. MSIJIDEKEZE. Kama unatafuta kazi mda na hujapata basi ujue hutafuti vya kutosha! Wewe uko mkoani unachofanya ni kuingia zoom na kuapply kumbuka mko million na wote mnaingia na kuapply hata wakipata 100 kila siku uwezekano wa kufikiwa ni mdogo. Kuweni wabunifu/creative kwenye kusaka ajira. Mfano nunua lakuchumpa lako amkaa saa kumi na moja kama wenye kazi, anza kudondosha bahasha yenye cv na criteria zako ofisi mpaka ofisi, wiki nzima hata mwezi ikibidi, trust me Mungu si athumani utapata hata moja, japo soli ya viatu itakuwa imeisha.
2.ACHENI MASHAUZI. We mtu umetoka chuo hata experience huna unapeleka cv ina title Accounting Manager/ Senior Accountant etc, yaani hata mtu hasomi hadi mwisho anaona hujielewielewi. Wewe mahali huna ndugu japo wa kusingiziwa, peleka cv andika any post that fits my qualifications, utapewa hata ucashier au assistant accountant ambayo ni better 100% kuliko kukaa nyumbani. Seriously unaweza kuwa unapeleka sana cv huitwi sababu unachokitaka hakipo, ila ukiomba chochote kilichopo utapata mapema.
3.HAKUNA KAZI NZURI UJANJA WAKO TU. Unaweza kupata kazi amabyo contract mbovumbovu haina hata mvuto, ukaikataa kumbe usilolijua litakusumbua. Kamwe usikatae kuripo kazini kisa mkataba hujakuridhisha, we karipoti tu maybe ufanye hata mwezi ndo uache. Nasema hivi coz kuna kazi hasa hizi zetu za masoko/marketing unakuat mshahara take home 300,000 Mind you hapo una masters yako, unaweza ukakataa, ila nikiwa nina mdamrefu kwenye fani hii nakwambia kubali, coz unaweza kuta comissions hadi 6,000,000m kama utaclose big deals. This is a Fact! sasa hizi comission kwenye contract hazionekani, hiyo siri ya biashara unaweza kuwa umeacha best job you may ever get. Acha comission kuna kazi za Procurement 10% hazionekani kwenye mkataba. Kuna kazi zina mideal ya hatari ambayo ni nomaaa, mshahara ushahidi tu.
4.UKIONA UNATAFUTA KAZI FLANI HUPATI JUA RIZIKI YAKO HAIPO HUKO. Mimi kwa profession ni Accountant, tena nina C.P.A bt sikuwahi kupata kazi ya uhasibu nikaridhika nayo, actually nilikuwa napata bt kazi tembo mshahara sisimizi, kuna rafiki yangu akanitafutia kazi za marketing sikufurahi, tena nilipanga nisiende, bt akanipa altmatum nifanye for 2 weeks nikiboreka niache, nikaenda kutest zali, Nikagundua Marketting is the DEAL. Mishahara midogo ndio, ila allowance za hatari mara 3 ya mshahara, sijui vocha, transport, facilitation, entertainment, acha illegal kama 10% za kuzidisha bei.Im officially a marketer. In short usifocus kuwa in your life lazima ufanye kazi flani, think wider, unaweza kuta kuna kazi nzuri kuliko unayotafuta hujajua tu na ndo riziki Mungu aliokupangia.
5.MTAMALIZA MABUCHA NYAMA NI ILE ILE! Utakuta mtu ukobusy kutafuta kazi in big organisations, its good ila ujue tu mishahara haipishani. Rate za banks ni 300000 , 400000, 500000, 600000 take home chache zinafika mpaka 800,000take home kwa garduate ila nyingi ni 400000 -500000 sasa unaweza kuwa mahali ukahisi unadhulumiwa ukawa mnyonge na kiburi kingi, ukaona wenzio wanafaidii kumbe mnapata sawa sema yeye anabebwa na jina la Bank tu. Watu hawasemi mishahara ya ukweli ila rate ni zile zile tu, so ni heri uridhike na ulipo na kufocus kupanda cheo kuliko kukazana kuhama.
Nimechoka kutype bado nina mengi ila kwa haya yatawafumbua macho na kuwarudisha baadhi yenu kwenye straight line 180degree
ATAFUTAE HACHOKI AKICHOKA KAPATA, ZIDISHENI MAPAMBANO.
Nimeguswa kuyasema haya kutokana na tabia ya watu wachache wenye viherehere humu JF vya kuponda baadhi ya opportunity zinazotolewa na wadau humu wenye mioyo ya huruma kwa wasio na kazi.
Kitu cha muhimu kumbuka HUNA KAZI hivo usidharau na kukashifu any opportunity, kutoridhika na nafasi iliyopo its okay, sawa hujaridhika basi endelea kusoma thread zingine sio kuponda manake kwa yule mwenye shida utamkwaza kuikubali ile nafasi. Isitoshe kazi ni heshima hata kama hailipi ila unaamka unaoga asubuhi, mkaa bure sio sawa na mtembea bure, mtembea bure huenda akaokota.
Katika safari yenu ya kutafuta kazi naomba niwashauri machache
1. MSIJIDEKEZE. Kama unatafuta kazi mda na hujapata basi ujue hutafuti vya kutosha! Wewe uko mkoani unachofanya ni kuingia zoom na kuapply kumbuka mko million na wote mnaingia na kuapply hata wakipata 100 kila siku uwezekano wa kufikiwa ni mdogo. Kuweni wabunifu/creative kwenye kusaka ajira. Mfano nunua lakuchumpa lako amkaa saa kumi na moja kama wenye kazi, anza kudondosha bahasha yenye cv na criteria zako ofisi mpaka ofisi, wiki nzima hata mwezi ikibidi, trust me Mungu si athumani utapata hata moja, japo soli ya viatu itakuwa imeisha.
2.ACHENI MASHAUZI. We mtu umetoka chuo hata experience huna unapeleka cv ina title Accounting Manager/ Senior Accountant etc, yaani hata mtu hasomi hadi mwisho anaona hujielewielewi. Wewe mahali huna ndugu japo wa kusingiziwa, peleka cv andika any post that fits my qualifications, utapewa hata ucashier au assistant accountant ambayo ni better 100% kuliko kukaa nyumbani. Seriously unaweza kuwa unapeleka sana cv huitwi sababu unachokitaka hakipo, ila ukiomba chochote kilichopo utapata mapema.
3.HAKUNA KAZI NZURI UJANJA WAKO TU. Unaweza kupata kazi amabyo contract mbovumbovu haina hata mvuto, ukaikataa kumbe usilolijua litakusumbua. Kamwe usikatae kuripo kazini kisa mkataba hujakuridhisha, we karipoti tu maybe ufanye hata mwezi ndo uache. Nasema hivi coz kuna kazi hasa hizi zetu za masoko/marketing unakuat mshahara take home 300,000 Mind you hapo una masters yako, unaweza ukakataa, ila nikiwa nina mdamrefu kwenye fani hii nakwambia kubali, coz unaweza kuta comissions hadi 6,000,000m kama utaclose big deals. This is a Fact! sasa hizi comission kwenye contract hazionekani, hiyo siri ya biashara unaweza kuwa umeacha best job you may ever get. Acha comission kuna kazi za Procurement 10% hazionekani kwenye mkataba. Kuna kazi zina mideal ya hatari ambayo ni nomaaa, mshahara ushahidi tu.
4.UKIONA UNATAFUTA KAZI FLANI HUPATI JUA RIZIKI YAKO HAIPO HUKO. Mimi kwa profession ni Accountant, tena nina C.P.A bt sikuwahi kupata kazi ya uhasibu nikaridhika nayo, actually nilikuwa napata bt kazi tembo mshahara sisimizi, kuna rafiki yangu akanitafutia kazi za marketing sikufurahi, tena nilipanga nisiende, bt akanipa altmatum nifanye for 2 weeks nikiboreka niache, nikaenda kutest zali, Nikagundua Marketting is the DEAL. Mishahara midogo ndio, ila allowance za hatari mara 3 ya mshahara, sijui vocha, transport, facilitation, entertainment, acha illegal kama 10% za kuzidisha bei.Im officially a marketer. In short usifocus kuwa in your life lazima ufanye kazi flani, think wider, unaweza kuta kuna kazi nzuri kuliko unayotafuta hujajua tu na ndo riziki Mungu aliokupangia.
5.MTAMALIZA MABUCHA NYAMA NI ILE ILE! Utakuta mtu ukobusy kutafuta kazi in big organisations, its good ila ujue tu mishahara haipishani. Rate za banks ni 300000 , 400000, 500000, 600000 take home chache zinafika mpaka 800,000take home kwa garduate ila nyingi ni 400000 -500000 sasa unaweza kuwa mahali ukahisi unadhulumiwa ukawa mnyonge na kiburi kingi, ukaona wenzio wanafaidii kumbe mnapata sawa sema yeye anabebwa na jina la Bank tu. Watu hawasemi mishahara ya ukweli ila rate ni zile zile tu, so ni heri uridhike na ulipo na kufocus kupanda cheo kuliko kukazana kuhama.
Nimechoka kutype bado nina mengi ila kwa haya yatawafumbua macho na kuwarudisha baadhi yenu kwenye straight line 180degree
ATAFUTAE HACHOKI AKICHOKA KAPATA, ZIDISHENI MAPAMBANO.