Msinilaumu. Siamini alichosema Waziri Mkuu Bungeni, naona ni porojo za siasa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameeleza Bungeni kuwa hivi karibuni serikali itaifufua reli ya kwenda Arusha kupitia Segera na Moshi. Pia amesema serikali itaifufua reli ya kwenda Tanga, na kujenga reli toka Mtwara, kupitia Tunduma hadi Mbamba Bay. Mpango ni kujenga reli hizi katika standard gauge.

Wana JF acha mnilaumu, lakini ukweli ni kwamba siamini hiki kilichosemwa na Waziri Mkuu. Naona hapa alikuwa anafurahisha genge tu, na kama wabunge wameamini haya maneno basi wanaweza kuamini lolote watakalodanganywa na serikali (believe this and you will believe anything)

Labda kama Waziri Mkuu anamaanisha kwamba hizi reli zitafufuliwa miaka 50 ijayo, au siku tukipata mafuta yetu. Ikiwa ni hivyo basi si sahihi kwa Waziri Mkuu kuongelea kufufuliwa na kujengwa kwa hizi reli kama vile ni jambo litafanyika miaka miwili ijayo.

Au labda Tanzania inayohangaika kupata fedha za kujenga flyover hapa Dar na kulipa mafao ya wafanyakazi waliostaafu ina fedha kibindoni kuweza kufanya haya anayosema Waziri Mkuu? Iweje serikali imeshindwa kulipa mafao ya wastaafu wanaosubiri zaidi ya miaka mitatu na iongelee kujenga na kufufua reli zote hizi? Au serikali imeamua kwa makusudi kuwadhurumu wastaafu ili kutekeleza miradi yake ya kukiinua chama tawala?

Is the Prime Minster trying to insult the intelligence of, not only honorable MPs, but all Tanzanians?

Siamini hata kidogo alichosema Waziri Mkuu. Naona kaongea propaganda tu kwa ajili ya chama chake.
 
Kwani kasema zinafufuliwa ndani ya awamu hii?

Soma thread yote kabla ya kujibu

"Labda kama Waziri Mkuu anamaanisha kwamba hizi reli zitafufuliwa miaka 50 ijayo, au siku tukipata mafuta yetu. Ikiwa ni hivyo basi si sahihi kwa Waziri Mkuu kuongelea kufufuliwa na kujengwa kwa hizi reli kama vile ni jambo litafanyika miaka miwili ijayo."

upload_2018-6-8_11-19-49.png
 
sio ww tu, hata yeye akisikiliza upya akiwa ametulia hawezi amini uongo huu na atashangaa sana inawezekana vp? mtu kudanganya namna hii.
Hilo ni tatizo la kuwa na wabunge wengi walio pale kwa kuunga mkono kila linalosemwa na serikali, na wabunge wa upinzani wanaoondolewa bungeni au kuzuiwa kumuuliza Waziri Mkuu maswali. Hivyo Waziri Mkuu anajua kabisa anaweza kuongea chochote hata iwe pumba vipi na haitakuwa tatizo
 
sio ww tu, hata yeye akisikiliza upya akiwa ametulia hawezi amini uongo huu na atashangaa sana inawezekana vp? mtu kudanganya namna hii.
...ha haaa watawala sasa wanawajua vzr watu wao huwa wanapenda kusikia Porojo kuliko uhalisia wa mambo nawao ndio wanafanya usishangae ukipita baadhi ya Mitaa kuwakuta watu wanapongeza Kauli ya PM
 
najiuliza tu wajerumani walitumia jumla ya miaka mingapi kujenga mtandao wa reli yote nchini.
 
najiuliza tu wajerumani walitumia jumla ya miaka mingapi kujenga mtandao wa reli yote nchini.
Mkuu, kuna wakati nasoma matamko ya serikali ambao naona kabisa ni uongo naona kama wananitukana mie binafsi - insulting the intelligence of all Tanzanians
 
sio ww tu, hata yeye akisikiliza upya akiwa ametulia hawezi amini uongo huu na atashangaa sana inawezekana vp? mtu kudanganya namna hii.
Uongozi kweli dhima mpaka kwa Mungu,naamini kabisa K.M yuko kwenye swaumu.
 
Hilo ni tatizo la kuwa na wabunge wengi walio pale kwa kuunga mkono kila linalosemwa na serikali, na wabunge wa upinzani wanaoondolewa bungeni au kuzuiwa kumuuliza Waziri Mkuu maswali. Hivyo Waziri Mkuu anajua kabisa anaweza kuongea chochote hata iwe pumba vipi na haitakuwa tatizo
Kwani haiwezekani kuzifufua hizo reli?
 
najiuliza tu wajerumani walitumia jumla ya miaka mingapi kujenga mtandao wa reli yote nchini.
Acha kabisa Mkuu!
Mjerumani hakuwa Mtu wa Mchezo mchezo

Kazi iliyofanywa Na Mjerumani Kwa Miaka Kama 30 tu ( 1884-1914) inazidi kazi iliyofanywa Na Muingereza + TANU + CCM

Mjerumani kaondoka katuachia Reli ya kuunganisha Tanganyika Na Kigoma, katuachia Shule Kongwe Na Imara, katuachia Meli kongwe Duniani MV Liemba, katuachia Mahakama ngazi mpka ya Wilaya ikiwemo Ikulu ya Dsm katuachia vitu vingi Imara sana ambavyo mpaka Leo tunaviona!

Pengine Wajerumani wangetutawala mpaka 1961 Pengine South Africa ingekuwa inakuja kwenye Semina Elekezi hapa Nchini

German Ni watu wa kazi, wamepigwa Mara mbili kwenye World wars, wamevunjiwa Na kugawanywa Nchi Yao lakin walipokaa Sawa kuanzia 1989 Leo hii ndio Taifa kubwa lenye nguvu kiuchumi Bara zima la Ulaya
 
Mkuu, kuna wakati nasoma matamko ya serikali ambao naona kabisa ni uongo naona kama wananitukana mie binafsi - insulting the intelligence of all Tanzanians

Mkuu hii serekali ina vituko ile mbaya, sasa hivi wanaisho kwa kudanganya miradi ya maendeleo kisha wanasimama wanaongelea hizo poroho kama ndio maendeleo tayari. Utasikia hela tunakopa kwa ajili ya miundo mbinu ya reli nchi nzima, miradi ya umeme nk. Halafu wakati wanaongea hivyo macho makavu kama ni miradi inayotekelezwa na watu wanashangilia!!

Juzi sasa ndio nimecheka mpaka nikajishangaa, rais anasema awamu ya pili ya sijui kilimo ndani ya hii miaka mitano ataingiza 13.8t. Watu wazima na masuti yao wakawa wanashangilia.

Akajichanganya kada mmoja aliyeshikiwa akili na Polepole. Nikamwambia twende taratibu, SGR inahitaji 7t, SG inahitaji 3t, jumla ni 10t yote hiyo kukamilika ni ndani ya hii 5yrs kama itakuwa inatekekezwa, achia miradi mingine. Nikamuuliza ni wapi serekali hii itapata 13.8t ya kuweka kwenye kilimo. Tukaenda kwenye makusanyo ambayo nayo data zake ni za kupika. tukapiga makusanyo ya mwezi na natumizi pamoja kulipa deni, roughly inabaki chini ya 200b@monthy. Hiyo ikawa haitoshi SGR wala SG; achia miradi mingine. Akasema tutakopa na ufadhili, nikamwabia misaada toka kwa wazungu ina maswali yake kama demokrasia, nikamuambia hapa uwizi wa kura, kina Lisu kupigwa risasi na open government lazima hela ipungue. Hivyo misaada wangalau haitovuka 1t tena kwa shida. Tukaja kwenye mikopo, nako kuna shida zake kama debt ceiling, sifa nyinginezo kulingana wapi tunakopa. Nayo hatukuona wapi itavuka 1t. Tulipofika hapo kwenye uhalisia naona speed yake ya kujibu ikapungua. Akatafakari jinsi ya kupishana na huo ukweli, ikabidi aseme Mungu atajalia! !
 
Mkuu hii serekali ina vituko ile mbaya, sasa hivi wanaisho kwa kudanganya miradi ya maendeleo kisha wanasimama wanaongelea hizo poroho kama ndio maendeleo tayari. Utasikia hela tunakopa kwa ajili ya miundo mbinu ya reli nchi nzima, miradi ya umeme nk. Halafu wakati wanaongea hivyo macho makavu kama ni miradi inayotekelezwa na watu wanashangilia!!

Juzi sasa ndio nimecheka mpaka nikajishangaa, rais anasema awamu ya pili ya sijui kilimo ndani ya hii miaka mitano ataingiza 13.8t. Watu wazima na masiti yao wakawa wanashangilia. Akajichanganya kada mmoja aliyeshikiwa akili na Polepole.

Nikamwambia twende taratibu, SGR inahitaji 7t, SG inahitaji 3t, jumla ni 10t yote hiyo kukamilika ni ndani ya hii 5yrs kama itakuwa inatekekezwa, achia miradi mingine. Nikamuuliza ni wapi serekali hii itapata 13.8t ya kuweka kwenye kilimo. Tukaenda kwenye makusanyo ambayo nayo data zake ni za kupika. tukapiga makusanyo ya mwezi na natumizi pamoja kulipa deni, roughly inabaki chini ya 200b@monthy. Hiyo ikawa haitoshi SGR wala SG; achia miradi mingine. Akasema tutakopa na ufadhili, nikamwabia misaada toka kwa wazungu ina maswali yake kama demokrasia, nikamuambia hapa uwizi wa kura, kina Lisu kupigwa risasi na open government lazima hela ipungue. Hivyo misaada wangalau haitovuka 1t tena kwa shida. Tukaja kwenye mikopo, nako kuna shida zake kama debt ceiling, sifa nyinginezo kulingana wapi tunakopa. Nayo hatukuona wapi itavuka 1t. Tulipofika hapo kwenye uhalisia naona speed yake ya kujibu ikapungua. Akatafajari jinsi ya kupishana na huo ukweli, ikabidi aseme Mungu atajalia! !
Ukitaka kumnyamazisha mwasiasa mpiga porojo, ni kwenda nae kwa namba tu na facts. Huwa ni wepesi sana.
 
Huwezi kupanga kufufua kitu ambacho hakipo. Tofautisha kujenga na kufufua.
Hiyo reli ipo ila kunasehemu chache imevamiwa na watu au mchanga na mawe (deposition) so anachosema kinawezekana. Na nilibahatika kupita mikoa ya tanga hadi moshi, kuna sehemu nimeziona zikitengenezwa na vilevile hata niliona watu waliokuwa wanalalamika mita za utanuzi wa reli hiyo kule Tanga.
So badala ya kuanza kubisha uliza kwanza au tembea uone. Kuuliza si ujinga.
Kwa upande wa standard gauge sina uhakika, ila kwa kuwa wameanza na kuifufua iliyokuwepo nahisi kwa kuangalia mwenendo wa biashara ya usafirishaji wanaweza kuijenga kwa kiasi hicho wanachosema japo wana mipango mingi sana.
 
Waziri Mkuu namjua sio muongo kabisa na hana historia hiyo, tatizo ni hicho chama ukiingia lazima uwe muongo bila hata kujijua.
 
Back
Top Bottom