Msingi aliouweka ni mzuri, akachagua jina zuri lakini cdm hamjamsema vizuri:kulikoni?

UWEZO_WAKO

Member
Nov 17, 2010
39
4
Mwalimu aliwasema vizuri CDM, kwa nini nyie CDM hamjasema vizuri? Nauliza kulikoni? Nyerere maisha yake yalipofikia mwisho aliicha familia ambayo kwa hakika inapendwa na watanzania hasa kwa uadilfu wa mwalimu ikiwa ni pamoja na kazi nzuri aliyoifanya Mama yetu Maria kushiriki kikamilifu na yeye kwa nafasi yake. Huo ni kwa upande wa familia lakini kitaifa ni alama ya Taifa au Baba wa wote "Baba wa Taifa". Jina la Mwalimu linatumiwa kote nchini na sasa si la familia peke yao au la ccm peke yao. Kuna wazazi wengi ambao hawana hata ukoo na Mwalimu lakini wakaamua kuwaita watoto wao majina wengine Kambarage, wengine Julius, wengine Mwalimu na wengine Nyerere. Hivyo jina hilo kutumiwa na yoyote hakuna shida na asikudanganye mtu katika hilo. CDM nyie mmefanya nini au mmemuita nani jina la mwalimu. Ninauliza mnipe jibu.

Mwalimu Nyerere aliwahi kuwasifia CDM kuwa ni chama kinachoonyesha kuwa na mwelekeo mzuri, nafikiri aliyasema hayo kwa sababu mara nyingi alikerwa na mwenendo wa chama alichokiasisi yeye. Wakati mwingine aliona kuirekebisha ccm ni ngumu sana ila palipaswa pawepo na chama ambacho kitakuwa na maadili mazuri kitakachokuwa tayari kuchukua nafasi ya ccm. Mwalimu hata kuna wakati alitishia kurudisha kadi ya ccm. Hii ni kwa sababu ni mtu aliyekuwa amechagua jina zuri (Alithamini uadilifu na uthamani wa mtanzania) kuliko yeye kujilimbikizia utajiri na Dhahabu/Almasi. Leo kuna watu wanasema hamna haja ya kuwa na katiba mpya tutaendelea kuwekea viraka iliyopo.

Mwalimu alipoona CDM mna mwelekeo mzuri kwa nini hakunyamaza kwa ajili ya manufaa ya chama chake. Au hamjui ya kuwa alikuwa anawatia moyo kwa ajili ya nyie kuja kuisaidia nchi. Ninaandika haya kwa sababu tuna taka kasi zaidi ili lengo na dhana ya kuwa na upinzani iwepo kwa kiwango cha kutosha. Natumaini mmeona wananchi kuwapa kura nyingi wanataka mabadiliko, ccm ni shamba lililochoka (hakuna tena rutuba) linapaswa lipumzishwe.

Swali langu mnafikiria nini kwa ajili ya Jina la Mwalimu, pale mlipokuwa mnajaribu kulitumia jina la Mwalimu wakati mkijinadi kwa kuenzi Misingi bora aliyoiweka mwalimu hamkuona jamaa walivyokuwa wakali utafikiri wana hati miliki ya Jina. Kwanza hata mwenye jina alitaka kukihama chama chake lakini pia akawasifia nyie. Mimi nawauliza CDM mbona hamjamsema vizuri mwalimu inavyopaswa kuwa? Tumieni jina lake msione aibu, msingi alioujenga mwalimu bado ni mzuri shida ni ukuta, Msifikirie mtajenga juu ya msingi mwingine, msingi ni huo huo tunachotaka kufanya ni kubadilisha ma-engineer wa kujenga.

Nauliza tena CDM mmemuita nani jina la Mwalimu. Nasema msione aibu hata ndani ya CDM kama inawezekana kuwepo na taasisi ya jina la mwalimu fanyeni hivyo. Na hiyo ionyeshe namna amabavyo cdm inafanyia kazi za mwalimu. Mwalimu ana vitabu (ambavyo hata vingine vimefichwa haviko wazi), mwalimu ana hotuba za maadili, nk. Ni vizuri mkawa wabunifu ili pia kuondoa hali iliyopo watu kuita Mwalimu, mwalimu huku wanayoyafanya ni tofauti kabisa na matendo ya mwalimu. Kuweni wabunifu hata ikiwezekani chombo kitakachokuwa kinaratibu kazi za mwalimu watoe hata motisha kuvuta hisia za wananchi ili mradi wang'oe zana ya kwamba Mwalimu ni ccm. Uchaguzi uliopita kuna bibi mmoja aligoma kupiga kura akiomba aonywesha sehemu ya kumpigia Mwalimu maana kura yake alitaka kumpigia mwalimu, mtu mmoja akauliza unamaana unataka kuipigia ccm?. Swali hilo si sahihi, nikataa kabisa hii haikuwa lengo la huyo bibi, badala yake ingekuwa vyema kusema bibi alikuwa anatafuta kumpigia mtu ambaye ana uadilifu kama wa mwalimu...hiyo ingekuwa afadhali. Binafsi hata kama kuna siku CDM mtaiitisha kuwa maalumu ya kuenzi kazi za mwalimu ndani ya CDM hakika nitajumuika. Kweli CDM kiasi fulani mmejitahidi kuonyesha kufuata kwa vitendo yale mwalimu aliyoyaanzisha mazuri lakini swali langu linabaki pale pale MWALIMU ALIWASEMA VIZURI MBONA NYIE HAMJAMSEMA VIZURI MWALIMU? KWENU CDM MMEMUITA NANI JINA MWALIMU AU MNA MPANGO GANI?
 
..nadhani ktk mikutano mingi ya kampeni Dr.Slaa alikuwa akiwaambia wazi wananchi kwamba akichaguliwa atarudisha misingi ya uadilifu,umoja,na amani, aliyoiacha Mwalimu Nyerere.

..pia ni lazima uelewe kwamba wapiga kura wamebadilika, na matarajio yao pia. vijana wengi hawamjui Mwalimu, na hawana habari hali ya kisiasa na kijamii wakati wake ilikuwa ya aina gani. sasa ni vizuri Chadema wakawa-approach wapiga kura haswa vijana wa kileo kwa namna ambayo watawaelewa.

NB:

..mwaka 2005, wakati akiwa mgombea Uraisi, Mbowe alisema hayahaya uliyoelekeza hapo juu, na Kingunge Ngombale Mwiru alikuwa mkali kama mbogo. akidai Freeman Mbowe hamjui Mwalimu.
 
Nani aliyefuta maadhimisho ya MNF ya mwaka huu, nani aliwaita waanzilishi wa MNF wahuni nani walioanza kumwambia Slaa asitumie jina la Mwalimu kwa vile ni mwanzilishi wa CCM mfano kumwambia Leticia asitumie jina la Nyerere kwenye mikutano yake, nani aliyeua Azimio la Arusha nani aliyeyeua falsafa ya ujamaa na kujitegemea sasa ubepari, jamani msipindishe historia.

Afterall those who are singing Nyerereism are they really practicing what Mwalimu was doing? do they walk the talk?
 
..nadhani ktk mikutano mingi ya kampeni Dr.Slaa alikuwa akiwaambia wazi wananchi kwamba akichaguliwa atarudisha misingi ya uadilifu,umoja,na amani, aliyoiacha Mwalimu Nyerere.

..pia ni lazima uelewe kwamba wapiga kura wamebadilika, na matarajio yao pia. vijana wengi hawamjui Mwalimu, na hawana habari hali ya kisiasa na kijamii wakati wake ilikuwa ya aina gani. sasa ni vizuri Chadema wakawa-approach wapiga kura haswa vijana wa kileo kwa namna ambayo watawaelewa.

NB:

..mwaka 2005, wakati akiwa mgombea Uraisi, Mbowe alisema hayahaya uliyoelekeza hapo juu, na Kingunge Ngombale Mwiru alikuwa mkali kama mbogo. akidai Freeman Mbowe hamjui Mwalimu.

Sidhani kama tutafanikiwa kwa kujenga taifa lenye lenye kupoteza historia kwa kiasi hicho.... "No present without the past" na ndio maana hata kuna somo la historia, kujua tumetoka wapi, tuko wapi na tunaenda wapi. Nafikiri ni lazima tuwafundishe vijana na vyama vitoe elimu kwa umma wasipelekwe tu eti kwa sababu wana namna yao ya kufahamishwa... nadhani lengo si kushinda tu lakini tunapaswa watu waielewe historia ya nchi yao. Nchi nyingi hata zilizoendelea zinafundisha kweli kweli historia. Pia nafikiri makumbusho ya mwalimu yaboreshwe.
 
Mgombea wa Chadema jimbola Bunda alipata kura nyingi zidi ya Wasira mgombea wa ccm na kwa sababu Bunda mjini kura zilihesabiwa mapema watu walianza kusherekea wakisema Wasira kaanguka, nadhani ilikuwa ni kwa kudhani na matokeo ya maeneo mengine ya vijijini pia yangekuwa na mwelekeo huo huo. Aa wapi yalipoanza kuingia kura za Wasira zikaenda juu sana. Mimi nilidhani si vizuri kulenga tu vijana, hata watu wazima pia, hakuna kudharau hata kura moja, Mahubiri kuhusu kutekeleza na kuendeleza shughuli nzuri za mwalimu ziboreshwe zaidi zisiachwe. Kuna idadi kubwa hata wengine bado wako serikali wamefanya kazi na mwalimu, mwalimu bado live sana katika akili za watu hata vijana. Kuna watu na mimini mmoja wao na pia ni kijana huwezi kuongea na mimi siasa nisigusie Mwalimu. Kwanza pia ujue kwamba maraisi waliomfuatia Mwalimu hatamkwi sana wanalaumiwa kwa sababu mwalimu ameweka rekodi ya juu ndio wanalinganisha na kusema bado wewe hujafanya kitu. Kikwete mwaka 2005 watu walikuwa na matumainimakubwa wengine wakishangilia wakisema mwalimu amefufuka, kumbe wapi ndio hizokura zimetoka asilimia 80 mpaka asilimia 61 tena zenye kulalamikiwa na wtu wengi hawakuona maana ya kupiga kura. Historia ni muhimu na ungana nawe MAHENE
 
Back
Top Bottom