Msimu huu wa 88 tujadili kuhusu maonyesho ya wakulima, kipi kizuri, changamoto na maboresho

Lasway.Jr

JF-Expert Member
Jul 25, 2015
230
402
Uzi huu ni special kwa ajili ya kujadili mambo mbali mbali yanayohusu maadhimisho ya siku ya wakulima ali maarufu kama 88 , ambapo msimu huu huambatana na Maonyesho ya teknolojia za kilimo, mifugo, biashara n.k zinazolenga kuboresha zaidi sekta ya kilimo hapa nchini.

Maonyesho hawa kwa kawaida hufanyika kikanda ambapo mikoa teule huwa na uwanja spesho kwa ajili ya makampuni, mashirika, taasisi, watu binafsi kwenda na kuonyesha bidhaa na huduma zao ambapo mkulima na mfugaji ndio mlengwa kwenye maonyesho haya.

Katika tanzania maonyesho haya hufanyika katika mikoa ya Arusha, Morogoro, Mbeya, Mwanza, Tabora, Simiyu, asante Dodoma, Lindi, Unguja.

Kuna mazuri mengi kwenye viwanja hivi lakini ningependa tujikite zaidi kwenye teknolojia ambazo zinapigiwa debe na kuonyeshwa ili kusaidia wakulima pia nilitamani tujadili mapungufu ya maonyesho haya ili tuone namna ya kuyaboresha zaidi.

Mwaka huu tumeona mabadiliko makubwa hasa kwenye uzinduzi wa bima za Kilimo, ongezeko la makampuni ya nje na ndani yanayojihusisha na uuzaji wa zana za kilimo, mashine, mbegu, madawa, mbolea n.k.

Tumeona na tutazidi kuona viongozi mbali mbali wakitoa kauli na mapendekezo ya serikali kisera ili kusaidia wakulima
Tumeona mwamko wa wakulima kujitokeza kwa wingi na kutaka kujifunza zaid na mengine mengi ambayo wadau watachangia hapa
Pia mapungufu yameoneka hasa pale tunapoona makampuni mengi au wafanyabiashara wengi wasiojihusisha na kilimo na mifugo kuvamia maonyesho haya.

Ushiriki finyu wa makampuni kutoka nje ya nchi na hili nalisemea ninapolinganisha 88 ya hapa tanzania na maonyesho ya wakulima Mjini Nairobi ambapo kuna wingi wa kampuni za kigeni kuleta teknolojia mpya na kuziuza kwa wazawa.

Zaidi sana kampuni nyingi au waonyeshaji (exhibitors) wengi wamebobea kwenye uzalishaji zaidi. Hakuna exhibitors wengi kwenye upande wa masoko na uchakataji wa mazao ya wakulima kitu ambacho kinanipa wasiwasi sana na kuona ni muhimu zaidi kuliangalia suala hili na kulifanyia kazi.

Karibuni

Tujuze 88 mwaka huu ni nini kipya kizuri na changamoto ni zipi?
 
Nipo Mbeya, John Mwakagale, Tunatangaza brand mpya ya kampuni yetu.my concern ni kwa waandaji. Hapa viwanjani kuna vumbi la kufa mtu. Wanakusanya hela ya kutosha, lakini hawazitumii kuboresha miundo mbinu ya uwanjani. I guess after this event I am going to be hospitalized.
 
Kwanza kabisa, namimi nikuunge mkono mtoa mada kwa asilimia zote kuhusu hili swala. 88 kwa sasa imevamiwa na siku ya 77 maana ninanyoielewa mimi hii siku ilitakiwa kuwe na Mambo tofauti tofauti yanayohusu kilimo ikiwemo makampuni kuonesha teknolojia zao, pembejeo na namna wanavyosindika bidhaa zao, masoko na vitu vinginevyo vingi tu vihusuvyo sekta ya kilimo, uvuvi na mifugo, vyama vya msingi vya mazao na Mambo mengine mengi tu hivyo kumfanya mtu anatoka somewhere anafika mahala anarudi na kitu muhimu inampa nguvu yakufanya maamuzi.

Bahati mbaya sana 88 yakwetu mtu katoka kijijini anafika viwanja vya 88 ananunua redio, TV na king'amuzi anarudi nyumbani maisha yanaenda ukifika msimu wa mavuno anakwambia mwaka huu hali imekuwa mbaya sana mahindi yameozea shambani masoko hakuna na mambo kibao tu.
 
Kwanza kabisa, namimi nikuunge mkono mtoa mada kwa asilimia zote kuhusu hili swala. 88 kwa sasa imevamiwa na siku ya 77 maana ninanyoielewa mimi hii siku ilitakiwa kuwe na Mambo tofauti tofauti yanayohusu kilimo ikiwemo makampuni kuonesha teknolojia zao, pembejeo na namna wanavyosindika bidhaa zao, masoko na vitu vinginevyo vingi tu vihusuvyo sekta ya kilimo, uvuvi na mifugo, vyama vya msingi vya mazao na Mambo mengine mengi tu hivyo kumfanya mtu anatoka somewhere anafika mahala anarudi na kitu muhimu inampa nguvu yakufanya maamuzi.

Bahati mbaya sana 88 yakwetu mtu katoka kijijini anafika viwanja vya 88 ananunua redio, TV na king'amuzi anarudi nyumbani maisha yanaenda ukifika msimu wa mavuno anakwambia mwaka huu hali imekuwa mbaya sana mahindi yameozea shambani masoko hakuna na mambo kibao tu....
Hii ni kweli kabisa, inabidi tubadilike na mamlaka husika zifanye kazi.
 
Kuna umuhimu wa kuboresha maeneo husika na pia mpangilio wa waonesha bidhaa. Mfano, taasisi za fedha zikapangwa eneo moja, zana za kilimo sehemu moja, mitandao ya simu sehemu moja nk, hii itasaidia kwa wateja kupata huduma kirahisi. Maandalizi ya maonesho baadhi ya waoneshaji wanachelewa, utakuta mpaka siku ya 3 bado wanajenga banda!
 
Nipo Mbeya, John Mwakagale, Tunatangaza brand mpya ya kampuni yetu.my concern ni kwa waandaji. Hapa viwanjani kuna vumbi la kufa mtu. Wanakusanya hela ya kutosha, lakini hawazitumii kuboresha miundo mbinu ya uwanjani. I guess after this event I am going to be hospitalized.
Hata hapa Morogoro, vumbi limezidi sana kwenye maonesho. Nataman waandaaji wangejaza kokoto kwenye njia hizi wanazopita watu kupunguza vumbi.
 
Hayo maonyesho huwa yanafanyika kwa mazoea tu. Hakuna lolote la muhimu linaloleta mabadiliko kwenye sekta ya kilimo.
 
Morogoro
IMG_20190807_104848.jpeg
IMG_20190807_104845.jpeg
 
Hata hapa Morogoro, vumbi limezidi sana kwenye maonesho. Nataman waandaaji wangejaza kokoto kwenye njia hizi wanazopita watu kupunguza vumbi
Mkuu inawezekana kokoto hazipatikani hapa nchini sasa watatoa wapi pesa za kuagiza kutoka nje ya nchi? viongozi na wasimamizi wa hivyo viwanja hawana uthubutu wa kufikiria nje ya box!
 
Mtaalamu wa asali ya nyuki wakubwa (brown bees) na ya wadogo (black bees) pamoja na mazao mbalimbali yatokanayo na nyuki ...pia mizinga ya nyuki wakubwa na wadogo inapatikana kwa 0753543959
IMG-20190811-WA0001.jpeg
 
Back
Top Bottom