Msimamo wangu: Sirudishi biashara zangu Tanzania

Malcom XX

JF-Expert Member
Sep 12, 2020
471
948
Ndugu zangu mimi ni miongoni mwa watanzania wengi tulioumizwa katika awamu ya tano.

Biashara zangu ziliminywa mwanza, arusha, na Dar es salaam.

Maofisa wa TRA na TAKUKURU walinyanganya leseni ya biashara yangu na vile vile serikali wakarevoke account yangu kabla ya kuchukua pesa takribani milioni 600.

Nilitishwa sana na TRA na TAKUKURU, nilisingiziwa kuwa silipi kodi mbali na kuwa nilikuwa mlipaji mzuri wa kodi na pia niliwapa documents za miaka yote ya ulipaji kodi tangu mwaka 2001 nilipoanza biashara zangu za Kubadilisha fedha maarufu kama Bureau De change..

Serikali hii naomba iwalipe fidia wote waliodhulumiwa kwa sababu hata rais Huyu tunayemshangilia alikuwa sehemu ya tatizo hilo ambalo leo tunasahaulishwa kwa nyimbo za kusifu na haleluya za twitter.

Kumuombea mtu mabaya sipendagi lakini inafikia hatua tunaombeana mabaya ili tu angalau nafsi zitulizane kwa sababu ya dhulma tulizofanyiwa na wenye mamlaka.
 
Twitter imeteka akili za wengi sana, ni wachache sana wanaopita kule wanabaki na akili zao, hongera.

Kuhusu kurudisha biashara au vipi endelea kusoma upepo kwanza, maana kama ulivyosema hata huyu aliyepo nae alikuwepo wakati ule, japo yeye anaonekana tofauti ameshatoa agizo kwa TRA tusubiri utekelezaji.
 
Twitter imeteka akili za wengi sana, ni wachache sana wanaopita kule wanabaki na akili zao, hongera.
... tunaweza kupata list ya biashara zilizohamishiwa nje ya nchi kipindi cha utawala wa mwendazake? Au ni just maneno matupu?
Kilichosaidia ni kwamba kuna milioni 900 nilikuwa nimeweka katika benk kuu ya Ethipia ndiyo hawakuweza kuichukua.

Sasa hivi nipo najiiimarisha nchini Ethiopia.
 
TRA na TAKUKURU wanaweza kweli kua na shida lakini pia watu wa kubadilisha pesa mlikua na shida nyingi na kubwa.

TRA imara haiwezi kupendwa na wafanya biashara. Huo ndio ukweli.

Kipindi kile cha kikwete watu wanakwepa kodi hawalipi mbona hatukusikia TRA ikilalamikiwa kua haikusanyi kodi, ni dhaifu? Mbona hatukusikia?

Mama Samia akiingia mtego wa wafanya biashara kukushinikiza ufanye wanavyotaka umekwisha.
 
Jameni,
Kweli hali ilikuwa mbaya kiasi hiki?

Bahati mbaya sana hatupati taarifa za upande wa pili, nako tukajisomea na kuangalia hali halisi..

Inaeleweka, duniani kote, wafanya biashara, au hata mtu wa kawaida tu, ulipaji kodi hakuna hata mmoja anayeushabikia. Lakini inapofikia kiasi hiki, na ukatili/uoneaji juu yake, inashawishi sana kuamini kwamba pamekuwa na ukandamizaji wa wafanya biashara kusikokuwa kwa kawaida.

Kuhusu kutorudisha biashara Tanzania, hizo ni porojo tu. Kama wewe ni mfanyabiashara kweli, na biashara zako unazifanya kwa taratibu na sheria zilizopo, utarudi tu, hali ikiwa nzuri.
Soko lote hili la Tanzania wewe usilikubali, wewe kweli ni mfanya biashara?
 
TRA na TAKUKURU wanaweza kweli kua na shida lakini pia watu wa kubadilisha pesa mlikua na shida nyingi na kubwa.

TRA imara haiwezi kupendwa na wafanya biashara. Huo ndio ukweli.

Kipindi kile cha kikwete watu wanakwepa kodi hawalipi mbona hatukusikia TRA ikilalamikiwa kua haikusanyi kodi, ni dhaifu? Mbona hatukusikia?

Mama Samia akiingia mtego wa wafanya biashara kukushinikiza ufanye wanavyotaka umekwisha.
Atakuwa ishomile a.k.a misifa hana biashara yoyote
 
Uamuzi mzuri sana Mkuu, bila kuona hatua madhubuti za kuwarudishia mabilioni yao kama siyo trillions wote waliodhulumiwa na Serikali dhalimu ya jiwe kutakuwa hakuna jipya. Bank hakuna pesa jiwe alikuwa akikomba zote kidikteta. CRDB wana hali mbaya sana na si ajabu benki zote nchi ziko hoi bin taabani.
 
TRA imara haiwezi kupendwa na wafanya biashara. Huo ndio ukweli.
Wewe unajua unachokisema ? TRA hapaswi kuwa adui bali ni partner inabidi awe mshauri na rafiki.., kifo cha mfanyabiashara ni kifo cha nchi ambayo major employer ni private sector na sio State / Government...

Ukiona wafanyabiashara wanakwepa basi hizo kodi sio rafiki.., na dawa ni kuziba hizo loopholes na sio kuwafirisi au kuwanyanyasa
 
TRA na TAKUKURU wanaweza kweli kua na shida lakini pia watu wa kubadilisha pesa mlikua na shida nyingi na kubwa.

TRA imara haiwezi kupendwa na wafanya biashara. Huo ndio ukweli.

Kipindi kile cha kikwete watu wanakwepa kodi hawalipi mbona hatukusikia TRA ikilalamikiwa kua haikusanyi kodi, ni dhaifu? Mbona hatukusikia?

Mama Samia akiingia mtego wa wafanya biashara kukushinikiza ufanye wanavyotaka umekwisha.

Kama kweli hao wenye maduka ya kubadilishia fedha walikuwa na matatizo, ndio waporwe pesa zao na vyombo vya dola? Je ni wafanyabishara wote wenye hayo maduka walikuwa na matatizo hadi kuporwa? Acha kutetea tabia za kidhalimu kwa kisingizo cha kukusanya kodi. Hakuna mtu anataka kukwepa kodi, lakini kutuma kundi la watu wenye suti nyeusi kupora pesa za watu ni uovu. Kwa maelezo yako inaonekana ww ulikuwa ni mfaidika binafsi wa ule uporaji.
 
Wewe hujui chochote kuhusi biashara, uchumi na uwekezaji. Mawazo yako kuhusu uchumi, yameishia kwenye kuta za chumba chako.

Unachotakiwa kufahamu, ni kuwa hakuna nchi maskini hata moja Duniani iliyowahi kuendela ama kwa kuongeza ukubwa wa kodi au uwingi wa kodi.

Nchi ikiwa masikini inatakiwa kushusha sana viwango vya kodi ili kuvutia uwekezaji. Viongozi wetu wajifunze toka Dubai na Ghana. Wajinga wanadhani kuwa kodi ikiwa kubwa sana ndiyo kupata makusanyo makubwa!!
 
biashara ya takribani mill 600! maana yake ulikuwa na wafanyakazi pia. daah!! magu alikuwa tishio
 
Back
Top Bottom