Bia Ya Moto
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,221
- 2,801
2.Uharaka wa Katiba..Sawa. Kuna mawili hapo:
1. Umuhimu wa Katiba Mpya
2. Uharaka wa Katiba Mpya
Ushahidi gani unahitajika kwa kila kipengele?
1. Kazi za Wariona na Kisanga ni ushahidi wa kipengele cha kwanza
2. Kipengele cha pili hakina ushahidi hadi sasa, japo Chadema wanakiuma uma midomo tu na kulazimisha kipaumbele cha Chadema kiwe ndio kipamumbele cha Serikali ya CCM.
Mambo hayaendi hivyo.
Tuweke nguvu ya hoja katika kipengele cha pili, cha kwanza kinaeleweka na kukubalika.
Tupo kwenye kipindi ambacho ili tuijenge nchi basi tunahitaji mawazo kinzani na ya kwetu chama tawala,sasa mianya iliyopo kwenye katiba ya sasa inatupa uwezo mkubwa sana hata tusitake wapinzani waseme mawazo yao kinzani..rejea zuio la mikutano ya kisiasa,rejea uwiano wa wabunge wa upinzani bungeni na wa chama tawala,tazama bungeni upitishwaji wa miswada,vifungu vya kisheria spika anasema " wanaopinga waseme hapana,wanaokubali waseme ndiyo" imetupelekea leo tunahaha kuelezea kuhusu hizi TOZO..
Tupo kwenye kipindi mtu anaweza kukausha tu mifuko ya hifadhi na kuamua kuzifanyia pesa jambo jingine bila kushauriana na mtu..
Mimi kama mwana CCM natamani kuiona hali hii na nyingine kama hizi ziondoshwe na wala tusitegemee mbeleko za mapungufu ya Katiba ili tuendelee kuwepo madarakani..