Msimamo Rasmi: Wakati Umefika kwa Freeman Mbowe (MB) Kujiuzulu; na Sekretariati Yake...

Binafsi sipendi viongozi kuhodhi madaraka kwa muda mrefu, lakini sijioni kama nina haki ya kumwambia Mbowe ajiuzulu.

Kwa sababu mimi si mwanachama wa CHADEMA.

Wanachama wa CHADEMA ndio wenye haki ya kuamua wawe na mwenyekiti wa maisha au wawe na term limits.

Sasa Mzee Mwanakijiji wewe ni mwanachama wa CHADEMA?

Ndiyo, wanachama wa CHADEMA ndiyo wenye haki na uwezo wa kuamua nani awe mwenyekiti wao na kwa muda gani. Kwa mihula au milele. Hilo ni juu yao.

Lakini pia, CHADEMA kama chama cha umma, tena kinachopewa ruzuku na serikali, ruzuku hiyo ambayo kimsingi ni pesa za walipa kodi, basi pia ni haki ya kila Mtanzania kuweza kujieleza na kutoa maoni yake juu ya yale yanayoendelea kwenye chama hicho.

Sidhani kuwa, kwa Mtanzania yeyote yule, kutoa maoni yake juu ya uongozi wa chama cha umma kilicho cha kisiasa, hata kama yeye si mwanachama mshika kadi wa chama hicho, ni kukipangia au kukiamrisha chama hicho kifanye hiki au kile.

Hata mimi binafsi, kwa maoni yangu, naona kabisa wakati wa Mbowe kujiuzulu ulishafika siku nyingi sana.

Ni maoni yangu tu kama Mtanzania. Katiba inanipa haki ya kuwa na maoni kama hayo.

Uongo?
 
Ndiyo, wanachama wa CHADEMA ndiyo wenye haki na uwezo wa kuamua nani awe mwenyekiti wao na kwa muda gani. Kwa mihula au milele. Hilo ni juu yao.

Lakini pia, CHADEMA kama chama cha umma, tena kinachopewa ruzuku na serikali, ruzuku hiyo ambayo kimsingi ni pesa za walipa kodi, basi pia ni haki ya kila Mtanzania kuweza kujieleza na kutoa maoni yake juu ya yale yanayoendelea kwenye chama hicho.

Sidhani kuwa, kwa Mtanzania yeyote yule, kutoa maoni yake juu ya uongozi wa chama cha umma kilicho cha kisiasa, hata kama yeye si mwanachama mshika kadi wa chama hicho, ni kukipangia au kukiamrisha chama hicho kifanye hiki au kile.

Hata mimi binafsi, kwa maoni yangu, naona kabisa wakati Mbowe kujiuzulu ulishafika siku nyingi sana.

Ni maoni yangu tu kama Mtanzania. Katiba inanipa haki ya kuwa na maoni kama hayo.

Uongo?
Unaruhusiwa kuwa na maoni, lakini, itakuwa vipi kama wanachama wa CHADEMA wanaona Mbowe anawaongoza vizuri sana, halafu wanachama wa CCM hawapendi Mbowe anavyowaongoza vizuri sana CHADEMA, wakaanza kuleta zengwe aondolewe ili CHADEMA kisiwe na uongozi mzuri?

Hapo ndipo umuhimu wa wanachama kuwa na maamuzi juu ya uongozi wao.

Watu wasio wanachama wanaruhusiwa kuwa na maoni, lakini hii ngoma si yao.
 
Mbowe hafai hata kuongoza kijiji katika awamu hii inayohitaji akili kubwa sana na Maarifa mengi huku ukiweka Ubinafsi pembeni.

Mtu yeyeote mbinafsi awamu hii hawezi kuwa kiongozi kamwe.

Mbowe ni Mbinafsi ,Mkabila,Mdini, Bepari ,Beberu mkubwa ,Mhuni ,Mkwepa kodi na fisadi Mla ruzuku kamwe hawezi kuungwa mkono na mtu yeyote safi na mwenye madili.

Mbowe alipaswa aweke mbali ukabila,na ubinafsi wote na kila aina ya sanaa kisha Amshauri vizuri Komredi Tundu Lisu Profesa wa kweli wa sheria Duniani na kukaa mezani na kuweka maridhiano na Ikulu ya Tanzania chini ya Mh.Rais kuachana na siasa za kuchafuana na kutukana na kuanza siasa za hoja na kuweka mbele maslahi ya nchi.
Baada ya hapo wamuombe Rais pawe na maridhiano ya kitaifa kama alivyoandika barua Mbowe. Then Mbowe aachie madaraka na kumkabidhi Chama Tundu Lisu. Katibu Mkuu awe ni Juma Mwalimu.Makamu wa Mwenyekiti awe ni John Mnyika .
Mwenezi awe ni John Heche, Msemaji wa Chama awe ni Msigwa.
Hivi hapo nani anguza Chama ??
Kwa nini tunadanganyana kwa kusikiliza Porojo za Mbowe?
Karne hii msomi gani atakubali kuongozwa na Mbowe asiye na uteuzi wowote kisiasa na kiutawala ? Angekua Mbowe ni Rais watu wangemvumilia kwa kulinda Maslahi yao na usalama wao kijamii lakini kwa Chama cha upinzani haiwezekani msomi kubaki Chadema chini ya udikteta wa Mbowe.
Ni bora mtu akimbilie kwenye nafasi ya udikteta utakaompa kula vizuri na familia yake.Chama ni cha Mbowe na genge lake manasubiri nini huko mpaka muitwe mamluki na wasaliti.

Nitoe wito kwa Wasomi na wote wenye Uwezo wa kupata uteuzi wowote wenye heshima na maslahi bora wamwachie Mbowe Chama Chake wajiunge na CCM na kuweza kupata maisha bora yenye heshima na amani mana ndani ya Chadema ya Mbowe hakuna ndoto ya mtu itakayotimia zaidi ya kuitwa majina mabaya ya usaliti na mamluki.
Chadema sio mama wala baba yenu.
Hongera sana Dk. Mashinji umeona Mbali. Najua unakipenda Chama Chako cha Chadema lakini unalipenda zaidi Taifa letu na familia yako na Kabila lako. Umeona Mbali zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaruhusiwa kuwa na maoni, lakini, itakuwa vipi kama wanachama wa CHADEMA wanaona Mbowe anawaongoza vizuri sana, halafu wanachama wa CCM hawapendi Mbowe anavyowaongoza vizuri sana CHADEMA, wakaanza kuleta zengwe aondolewe ili CHADEMA kisiwe na uongozi mzuri?

Kwa ‘zengwe’ unamaanisha kuingilia mambo yao ya ndani ya chama? Kama ni hilo, hapana. Hilo si vyema.

Hapo ndipo umuhimu wa wanachama kuwa na maamuzi juu ya uongozi wao.

Watu wasio wanachama wanaruhusiwa kuwa na maoni, lakini hii ngoma si yao.

Naona umekubaliana nami! 👍🏾
 
Mbowe hafai hata kuongoza kijiji katika awamu hii inayohitaji akili kubwa sana na Maarifa mengi huku ukiweka Ubinafsi pembeni.

Mtu yeyeote mbinafsi awamu hii hawezi kuwa kiongozi kamwe.

Mbowe ni Mbinafsi ,Mkabila,Mdini, Bepari ,Beberu mkubwa ,Mhuni ,Mkwepa kodi na fisadi Mla ruzuku kamwe hawezi kuungwa mkono na mtu yeyote safi na mwenye madili.

Mbowe alipaswa aweke mbali ukabila,na ubinafsi wote na kila aina ya sanaa kisha Amshauri vizuri Komredi Tundu Lisu Profesa wa kweli wa sheria Duniani na kukaa mezani na kuweka maridhiano na Ikulu ya Tanzania chini ya Mh.Rais kuachana na siasa za kuchafuana na kutukana na kuanza siasa za hoja na kuweka mbele maslahi ya nchi.
Baada ya hapo wamuombe Rais pawe na maridhiano ya kitaifa kama alivyoandika barua Mbowe. Then Mbowe aachie madaraka na kumkabidhi Chama Tundu Lisu. Katibu Mkuu awe ni Juma Mwalimu.Makamu wa Mwenyekiti awe ni John Mnyika .
Mwenezi awe ni John Heche, Msemaji wa Chama awe ni Msigwa.
Hivi hapo nani anguza Chama ??
Kwa nini tunadanganyana kwa kusikiliza Porojo za Mbowe?
Karne hii msomi gani atakubali kuongozwa na Mbowe asiye na uteuzi wowote kisiasa na kiutawala ? Angekua Mbowe ni Rais watu wangemvumilia kwa kulinda Maslahi yao na usalama wao kijamii lakini kwa Chama cha upinzani haiwezekani msomi kubaki Chadema chini ya udikteta wa Mbowe.
Ni bora mtu akimbilie kwenye nafasi ya udikteta utakaompa kula vizuri na familia yake.Chama ni cha Mbowe na genge lake manasubiri nini huko mpaka muitwe mamluki na wasaliti.

Nitoe wito kwa Wasomi na wote wenye Uwezo wa kupata uteuzi wowote wenye heshima na maslahi bora wamwachie Mbowe Chama Chake wajiunge na CCM na kuweza kupata maisha bora yenye heshima na amani mana ndani ya Chadema ya Mbowe hakuna ndoto ya mtu itakayotimia zaidi ya kuitwa majina mabaya ya usaliti na mamluki.
Chadema sio mama wala baba yenu.
Hongera sana Dk. Mashinji umeona Mbali. Najua unakipenda Chama Chako cha Chadema lakini unalipenda zaidi Taifa letu na familia yako na Kabila lako. Umeona Mbali zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo akili kubwa ni ya kuipindua nchi? Ulitaka afanyeje sasa? mnatafuta kutukanwa tu na kuharibu reputaion za watu
 
Mbowe hafai hata kuongoza kijiji katika awamu hii inayohitaji akili kubwa sana na Maarifa mengi huku ukiweka Ubinafsi pembeni.

Mtu yeyeote mbinafsi awamu hii hawezi kuwa kiongozi kamwe.

Mbowe ni Mbinafsi ,Mkabila,Mdini, Bepari ,Beberu mkubwa ,Mhuni ,Mkwepa kodi na fisadi Mla ruzuku kamwe hawezi kuungwa mkono na mtu yeyote safi na mwenye madili.

Mbowe alipaswa aweke mbali ukabila,na ubinafsi wote na kila aina ya sanaa kisha Amshauri vizuri Komredi Tundu Lisu Profesa wa kweli wa sheria Duniani na kukaa mezani na kuweka maridhiano na Ikulu ya Tanzania chini ya Mh.Rais kuachana na siasa za kuchafuana na kutukana na kuanza siasa za hoja na kuweka mbele maslahi ya nchi.
Baada ya hapo wamuombe Rais pawe na maridhiano ya kitaifa kama alivyoandika barua Mbowe. Then Mbowe aachie madaraka na kumkabidhi Chama Tundu Lisu. Katibu Mkuu awe ni Juma Mwalimu.Makamu wa Mwenyekiti awe ni John Mnyika .
Mwenezi awe ni John Heche, Msemaji wa Chama awe ni Msigwa.
Hivi hapo nani anguza Chama ??
Kwa nini tunadanganyana kwa kusikiliza Porojo za Mbowe?
Karne hii msomi gani atakubali kuongozwa na Mbowe asiye na uteuzi wowote kisiasa na kiutawala ? Angekua Mbowe ni Rais watu wangemvumilia kwa kulinda Maslahi yao na usalama wao kijamii lakini kwa Chama cha upinzani haiwezekani msomi kubaki Chadema chini ya udikteta wa Mbowe.
Ni bora mtu akimbilie kwenye nafasi ya udikteta utakaompa kula vizuri na familia yake.Chama ni cha Mbowe na genge lake manasubiri nini huko mpaka muitwe mamluki na wasaliti.

Nitoe wito kwa Wasomi na wote wenye Uwezo wa kupata uteuzi wowote wenye heshima na maslahi bora wamwachie Mbowe Chama Chake wajiunge na CCM na kuweza kupata maisha bora yenye heshima na amani mana ndani ya Chadema ya Mbowe hakuna ndoto ya mtu itakayotimia zaidi ya kuitwa majina mabaya ya usaliti na mamluki.
Chadema sio mama wala baba yenu.
Hongera sana Dk. Mashinji umeona Mbali. Najua unakipenda Chama Chako cha Chadema lakini unalipenda zaidi Taifa letu na familia yako na Kabila lako. Umeona Mbali zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app

..aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Prof.Safari ni Msukuma.

..aliyekuwa Katibu Mkuu Dr.Mashinji ni Msukuma.

..aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu John Mnyika ni Msukuma.

..sasa kusema Mbowe ni mkabila mnakuwa hamumtendei haki.
 
..aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Prof.Safari ni Msukuma.

..aliyekuwa Katibu Mkuu Dr.Mashinji ni Msukuma.

..aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu John Mnyika ni Msukuma.

..sasa kusema Mbowe ni mkabila mnakuwa hamumtendei haki.

Hmm....Prof. Safari na Mnyika ni Wasukuma kweli?
 
..nimemsikia Prof kwa kinywa chake akisema yeye ni Msukuma.

..John Mnyika pia amedai kwao ni Misungwi. Na majuzi alikuwa huko kumzika baba yake mdogo.

Hmmm

Safari mbona ni jina la watu wa Kaskazini...

Na Mnyika naye nina shaka...
 
Kwa haki na kwa kulinda heshima ya chama, Mbowe hakutakiwa kugombea uenyekiti wa chama, kwa maana nyakati zilizopo zimebadirika zinahitaji mbinu nyingine ili kuuvusha upinzani kwenye huu mkwamo uliopo.
Kweli kabisa,ilibidi apewe Cecil Mwambe,hii ingekuwa habari njema sana,kwani mpaka sasa angekuwa ameunga mkono juhudi na nchi ingepiga hatua kubwa kimaendeleo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hmmm

Safari mbona ni jina la watu wa Kaskazini...

Na Mnyika naye nina shaka...

..wapo wakina Safari toka kabila la Wairaqw / Wambulu.


..lakini mimi nimemsikia Prof.Safari akisema yeye ni Msukuma. Nitatafuta video clip nikuletee usikie.


..kuhusu John Mnyika na asili yake ya Usukuma sikiliza video clip hapo chini kuanzia dakika 2:50.

NB.

..hata jina Chadema kuna wanaofahamu historia ya kuasisiwa kwa chama wanadai lilipendekezwa na Mzee wa Kisukuma toka Shinyanga ambaye ni mmoja wa waasisi wa chama.

 
Kwa ‘zengwe’ unamaanisha kuingilia mambo yao ya ndani ya chama? Kama ni hilo, hapana. Hilo si vyema.



Naona umekubaliana nami!
Unaruhusiwa kuwa na maoni, hiyo ni haki yako ya kikatiba.

Ila ujianza kushikia bango uongozi wa chama ambacho si tawala na si chako, unawe,a kuambiwa umetumwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I am very much worried, some 🧠 are frozen.
How can you celebrate such catastrophic and failure? 99% of the members are complaining!
Is it because they don't have ways to act against it?
75% of your members of Parliament are not happy,
Come on folks you will pay the price of the people tears!
 
Mzee mwanakijiji umekuwa ukitoa ushauri mzuri kila mara kwa hiki chama mfu.wenye chama Chao wameziba macho na masikio hawaishi kejeli na matusi.
Sikio la kufa halisikii dawa!
 
Kwa haki na kwa kulinda heshima ya chama, Mbowe hakutakiwa kugombea uenyekiti wa chama, kwa maana nyakati zilizopo zimebadirika zinahitaji mbinu nyingine ili kuuvusha upinzani kwenye huu mkwamo uliopo.
Sio kwamba Kuna watu walimchukulia fomu na yeye akakubali kwa kuzingatia idadi(sauti) ya Watu waliomshawishi?
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Hili ni swali ambalo linahitaji jibu. Kwenye nchi na vyama vya kidemokrasia mojawapo ya kanuni muhimu ni ile inayotaka viongozi wa juu wa chama kuwajibika mara moja pale vyama vyao vinaposhindwa uchaguzi. Hili ni kweli hasa pale kiongozi anapowekeza mkakati mzito na kuwaaminisha wanachama na mashabiki wake kuwa mkakati au msimamo waliochukua utakipa chama ushindi mkubwa. Mkakati au msimamo huo unaposhindwa viongozi wale hawatakiwi kuendelea na madaraka na badala yake hutangaza kuachia ngazi ili kutoa nafasi kwa viongozi wengine kuja na msimamo na mkakati mwingine ambao ni tofauti na ule mwingine. Nitatoa mifano michache.

Uingereza: Jeremy Corbyn
Bw. Corbyn alikuwa ni kiongozi wa chama cha Labour cha Uingereza akiwa kinyume kimisimamo na mwelekeo na uongozi wa Boris Johnson wa chama cha Conservatives. Katika mjadala wa kuondoka ama kuondoka au kubakia ndani ya Jumuiya ya Ulaya Corbyn aliongoza harakati za kubakia kwa muda mrefu. Alibeza misimamo na mipango ya chama cha Conservatives na hata kutaka uchaguzi mwingine ufanyike kuona wananchi wanasemaje.

Kufuatia matokeo ya uchaguzi mwezi Disemba mwaka jana ambayo yaliona Bw. Johnson akishinda na kupata wabunge wengi zaidi Corbyn alijua kuwa msimamo na mkakati wake umekataliwa na wananchi. Japo yeye mwenyewe alichaguliwa katika jimbo lake lakini alikiri kuwa hatokuwa tayari kukiongoza chama hicho kuelekea kampeni nyingine ya uchaguzi.

India: Rahul Gandhi
Licha ya kuwa na jina kubwa katika siasa za India, kiongozi wa chama cha Congress Gandhi alitarajiwa kubeba chama hicho ambacho familia na ukoo wake ulikuwa kama umekihodhi katika ngazi za juu kwa karibu nusu karne. Hata hivyo, baada ya kushindwa chaguzi za April na Mei mwaka jana, Gandhi alijikuta hana namna nyingine isipokuwa kukubali kuwa yeye hakuwa tena mtu sahihi wa kukiongoza chama hicho.

Katika kauli yake ya kujiuzulu Gandhi alisema "kuwajibika ni muhimu sana katika kuhakikisha chama chetu kinakua huko mbeleni. Ni kwa sababu hiyo nimeamua kujiuzulu nafasi yangu kama Rais wa chama". Hii haina maana hakuwa na mchango, au kuwa alikuwa kiongozi mbaya. Alichofanya ni somo la kawaida la demokrasia; kiongozi akishndwa kuongoza chama chake kushinda uchaguzi anatakiwa kujiuzulu siyo kutafuta udhuru.

Korea Kusini: Hoong Joon Pyo (kiongozi wa upinzani)
Mwaka 2018 chama cha Liberty Korea Party chini ya uongozi wa Bw. Pyo kilijikuta kinabwagwa vibaya kwenye uchaguzi mkuu kiasi cha kumfanya kiongozi huyo kukubali kubeba lawama zote za kushindwa huko na kuamua kujiuzulu.

Taiwan: Mwenyekiti Wu Den yii wa KMT

Baada ya kubwagwa vibaya kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka Huu uongozi mzima wa chama cha KMT uliandika barua zake kujiuzulu ili kuwajibikwa kwa matokeo mabaya ya uchaguzi huo. Mwenyekiti Wu Den yii (cheo sawa na cha Mbowe) akiongozi Sekretariati yake waliandika barua ya kujiuzulu mbele ya Kamati Kuu. Wu alikuwa ameapa kuwa mkakati wake wa uchaguzi utakipatia chama hicho angalau nusu ya viti vyote vya wabunge. Hilo halikutokea! na Walishindwa kwenye Urais kwa tofauti ya asilimia 20 ya kura!

Afrika Kusini: Mmusi Maimane wa DA
Kiongozi huyo alikuwa ni moto moto na alijaribu sana kukivutia chama cha DA kwa weusi wa Afrika ya Kusini. Hata hivyo, juhudi zake hizo hazikuweza kukifanya chama hicho kufanya vizuri zaidi kulinganisha na ANC ambayo ilikuwa inakumbwa na kashfa nyingi. Licha ya kashfa hizo chama cha DA hakikuweza kuvutia weusi wengi. Maimane aliamua kujiuzulu baada ya mikakati na mbingu zake zote kushindwa.

Mifano yote hiyo michache na ipo mingine mingi inatuonesha mambo mengi. Kubwa ni kuwa kiongozi wa chama cha siasa anaposhindwa kutimiza ndoto aliyowahidi wananchi wake yampasa yeye ajiuzulu na kama katika maamuzi hayo aliungwa mkono na viongozi wengine wa juu nao pia yawapasa kujiuzulu.

Mbowe na CHADEMA
Katika siasa zetu za Tanzania inasikitisha kuwa mikakati mbalimbali iliyobuniwa na MBowe na kutekelezwa na harakati mbalimbali imeonesha kufeli zaidi. Watu wamebakia kujivunia mavazi na rangi za magari na wingi wa misemo yenye kuvutia. Wakati umefika kwa Mbowe kujipima kama hawa viongozi wengine na kuona kama kweli anastahili kuiongoza CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020 baada ya kukiongoza chama hicho katika kufanya maamuzi mabovu, ya hatari na yenye kukidhoofisha zaidi.

Ni Tanzania tu ambapo kiongozi wa upinzani anakiongoza chama katika kushindwa katika kila uchaguzi na bado anatarajiwa kuendelea kukiongozi miaka mingine. Ni Tanzania tu kiongozi wa upinzani anahukumiwa siyo kwa kuwezesha kuingia madarakani bali kwa kuangalia ni kura ngapi zimeongezeka kwenye mahesabu!

Binafsi naamini kuondoka kwa Kashinji leo kuwe ndio msumari wa mwisho wa kuonesha ubaya, na upotofu wa maamuzi ya Mbowe kama Mwenyekiti. Suala hili ni suala la kidemokrasia na siyo suala la binafsi. Na ninaamini Sekretariati nzima ya CHADEMA isijiuzulu na kutoa nafasi kwa wanachama wengine kushika hatamu za uongozi wa chama kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020. Kuendelea kujificha kwenye kumlaumu Magufuli na CCM ni kujaribu kutafuta visingizio visivyoisha. Tangu 2005 hadi leo hii bado upinzani chini ya MBowe haujapata dawa sawasawa ya kukabiliana na CCM.

Kuukataa ukweli huu ni sawasawa na mtu anayejifumba macho kujificha na mwanga wa tochi unaommulika. Ni kweli anaweza asiuone mwanga huo lakini haina maana kwenye mwanga huo yeye haonekani.

Kudai ati "CCM iweke usawa" ati "tunapambana na dola" na kuwa "Magufuli ameminya demokrasia" ni visingizio vilivyopitwa na wakati na ambayo havina msingi katika uelewa wa siasa za kawaida za upinzani mahali popote duniani. Wale wapinzani wanaotaka chama tawala kiwatengenezee mazuria, kuwapambia maua na kuwaimbia nyimbo za kuwatia moyo hawafai hata chembe kuendelea kuuongoza upinzani huo.

Ni wakati wa Ndg. Freeman Mbowe kuamua kujiuzulu mara moja na siyo kutafuta udhuru na visingizio vya kushindwa. Afuate mfuano wa viongozi wengine ambao waliweza kuuangalia ukweli wa kushindwa kwao na kuusalimu kwa kujiuzulu.

Labda, Labda, UPINZANI wa kweli unaweza kuibuka.

MM. Mwanakijiji
Nikajua utatoa mifano ya Kenya,Uganda, Rwanda,Burundi,Zambia unatuletea habari za Uingereza,Korea na wapi sijui..bro siasa za ni afrika zina njia zake na kwa bahati nzuri tunajua kwann mnapiga kelele mbowe aondoke ni kwa sababu jamaa ni mgumu na ni Hatar sana kwenu so hatushangai..kwa roho mbaya hujataka kuonesha hata machache mazuri ambayo Mbowe kayafanya katika kipindi chake lengo ni kutuaminisha kwamba jamaa hajafanya kitu katika kipindi chake...waTanzania Wa aina hiyo walishaisha boss..tunaona,tunajua,tunaelewa na tunakumbuka so kakae andaa andiko lingine urudi huu ni uchafu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
48 Reactions
Reply
Back
Top Bottom