Elections 2010 Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Moshi Mjini asitisha Mkutano wa CHADEMA

Kamende

JF-Expert Member
Mar 1, 2008
416
45
Kwa wale wanaoujua mji wa Moshi wataweza kufuatilia kirahisi sana namna ambavyo uamuzi huu uluvyofanyika bila kufuata ukweli wa kisheria wala kimazingira.

Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi Mgombea Mwenza wa kiti cha urais kwa tiketi ya CCM Dr. Ghalib Bilal alikuwa awe mjini Moshi kesho tr. 18/10/2010. Badala yake amefika leo.

Baada ya CCM kujua kuwa Bilal atakuwepo Moshi leo walimwandikia barua Msimamizi wa uchaguzi wakimtaka ahamishe mkutano wa mgombea ubunge bw. Salakana kutoka katika kata ya Longuo B kwenda Pasua. Barua hiyo badala ya kusubiri ama kuitishiwa kikao cha pamoja cha makatibu wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi mjini Moshi ilijibiwa na Msimamizi mwenyewe kwa kuwaruhusu kufanya mkutano wanavyoona wenyewe inawafaa.

Hatua iliyofuatia Msimamizi leo amepeleka barua kwa Katibu wa CHADEMA Manispaa ya Moshi akimweleza kusitisha mkutano wa chama hicho katika kata ya Bondeni ili kupisha mkutano wa Bilal ufanyike bila usumbufu wowote.

Akielezewa kuwa mikutano hiyo iko kata tofauti Msimamizi alijibu kuwa Mkutano uko katika barabara ambayo CCM watapita wakienda kwenye mkutano wao.

Nalo jeshi la polisi mkoani hapa baada ya kupewa nakala ya barua hiyo wamepeleka magari yaliyojaza askari wa FFU wenye silaha katika uwanja ambao CHADEMA wangefanyia mkutano. Kuanzia saa 7.30 mchana leo gari la maji ya kuwasha limekuwa likivinjari katika mitaa ya Moshi kama tishio kwa yeyote atakayethubutu kwenda katika mkutano wa CHADEMA.

Muda huu nimepata habari kuwa mkutano wa Bilal ambao ulikuwa upambwe kwa kurejeshwa kwa kadi za CHADEMA ambazo wamezitengeneza wenyewe umekuwa na mahudhurio mabaya sana.
 
Wanasema you can for a while but not forever..... wananchi tumechoka, hatudanganiki na wala hatutishiki na sisiem
 
Kwa wale wanaoujua mji wa Moshi wataweza kufuatilia kirahisi sana namna ambavyo uamuzi huu uluvyofanyika bila kufuata ukweli wa kisheria wala kimazingira.

Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi Mgombea Mwenza wa kiti cha urais kwa tiketi ya CCM Dr. Ghalib Bilal alikuwa awe mjini Moshi kesho tr. 18/10/2010. Badala yake amefika leo.

Baada ya CCM kujua kuwa Bilal atakuwepo Moshi leo walimwandikia barua Msimamizi wa uchaguzi wakimtaka ahamishe mkutano wa mgombea ubunge bw. Salakana kutoka katika kata ya Longuo B kwenda Pasua. Barua hiyo badala ya kusubiri ama kuitishiwa kikao cha pamoja cha makatibu wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi mjini Moshi ilijibiwa na Msimamizi mwenyewe kwa kuwaruhusu kufanya mkutano wanavyoona wenyewe inawafaa.

Hatua iliyofuatia Msimamizi leo amepeleka barua kwa Katibu wa CHADEMA Manispaa ya Moshi akimweleza kusitisha mkutano wa chama hicho katika kata ya Bondeni ili kupisha mkutano wa Bilal ufanyike bila usumbufu wowote.

Akielezewa kuwa mikutano hiyo iko kata tofauti Msimamizi alijibu kuwa Mkutano uko katika barabara ambayo CCM watapita wakienda kwenye mkutano wao.

Nalo jeshi la polisi mkoani hapa baada ya kupewa nakala ya barua hiyo wamepeleka magari yaliyojaza askari wa FFU wenye silaha katika uwanja ambao CHADEMA wangefanyia mkutano. Kuanzia saa 7.30 mchana leo gari la maji ya kuwasha limekuwa likivinjari katika mitaa ya Moshi kama tishio kwa yeyote atakayethubutu kwenda katika mkutano wa CHADEMA.

Muda huu nimepata habari kuwa mkutano wa Bilal ambao ulikuwa upambwe kwa kurejeshwa kwa kadi za CHADEMA ambazo wamezitengeneza wenyewe umekuwa na mahudhurio mabaya sana.

Moshi hawataki upumbavu.

Wana akili. Wana Elimu. Wana mali. HAWAITAKI CCM. This is the kind of people we want in Tanzania.

CCM inawauma kweli kuhusu Moshi!!
 
Haisaidii kitu ni ulimbukeni tu . Mwisho umefika na miti yote inateleza
 
Moshi hawataki upumbavu.

Wana akili. Wana Elimu. Wana mali. HAWAITAKI CCM. This is the kind of people we want in Tanzania.

CCM inawauma kweli kuhusu Moshi!!
Kwa kweli kwa msimamo, watu wa Moshi ni mwisho, t-shirt na kofia wanavaa, nauli wanapokea na pilau wanakula, ila siku ya siku, kurua wanapeleka Chadema.

Naamini hivi ndivyo itakavyokuwa kwa Watanzania wote wanaitakia mema nchi hii, October 31, watapigia kura zao kwenye ukweli dhidi ya ubatili, japo wapendaubatili pia wapo na watapendelea ubatili uendelee ili wazidi kuneemeka na ubatili huu.
 
kwa wale wanaoujua mji wa moshi wataweza kufuatilia kirahisi sana namna ambavyo uamuzi huu uluvyofanyika bila kufuata ukweli wa kisheria wala kimazingira.

Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi mgombea mwenza wa kiti cha urais kwa tiketi ya ccm dr. Ghalib bilal alikuwa awe mjini moshi kesho tr. 18/10/2010. Badala yake amefika leo.

Baada ya ccm kujua kuwa bilal atakuwepo moshi leo walimwandikia barua msimamizi wa uchaguzi wakimtaka ahamishe mkutano wa mgombea ubunge bw. Salakana kutoka katika kata ya longuo b kwenda pasua. Barua hiyo badala ya kusubiri ama kuitishiwa kikao cha pamoja cha makatibu wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi mjini moshi ilijibiwa na msimamizi mwenyewe kwa kuwaruhusu kufanya mkutano wanavyoona wenyewe inawafaa.

Hatua iliyofuatia msimamizi leo amepeleka barua kwa katibu wa chadema manispaa ya moshi akimweleza kusitisha mkutano wa chama hicho katika kata ya bondeni ili kupisha mkutano wa bilal ufanyike bila usumbufu wowote.

Akielezewa kuwa mikutano hiyo iko kata tofauti msimamizi alijibu kuwa mkutano uko katika barabara ambayo ccm watapita wakienda kwenye mkutano wao.

Nalo jeshi la polisi mkoani hapa baada ya kupewa nakala ya barua hiyo wamepeleka magari yaliyojaza askari wa ffu wenye silaha katika uwanja ambao chadema wangefanyia mkutano. Kuanzia saa 7.30 mchana leo gari la maji ya kuwasha limekuwa likivinjari katika mitaa ya moshi kama tishio kwa yeyote atakayethubutu kwenda katika mkutano wa chadema.

Muda huu nimepata habari kuwa mkutano wa bilal ambao ulikuwa upambwe kwa kurejeshwa kwa kadi za chadema ambazo wamezitengeneza wenyewe umekuwa na mahudhurio mabaya sana.

huyo aliyekuletea habari ni muongo kwani mimi nilikuwepo ktk mkutano huo na mahudhurio ya wananchi yalikuwa makubwa na yakutia moyo hivyo wacheni propaganda zenu!!!

kama moshi ni ngome ya chadema mbona manispaa ya moshi tangu uchaguzi wa 1995 mpaka leo inaongozwa na madiwani wengi ni ccm na meya ni ccm!! Yaani hapa kuna mbunge kweli wa chadema lakini hana nguvu yoyote ya kuchangia sera za chadema kwani wenye kura nyingi ni madiwani wa ccm!!!

sasa ngome iko wapi?
 
huyo aliyekuletea habari ni muongo kwani mimi nilikuwepo ktk mkutano huo na mahudhurio ya wananchi yalikuwa makubwa na yakutia moyo hivyo wacheni propaganda zenu!!!

kama moshi ni ngome ya chadema mbona manispaa ya moshi tangu uchaguzi wa 1995 mpaka leo inaongozwa na madiwani wengi ni ccm na meya ni ccm!! Yaani hapa kuna mbunge kweli wa chadema lakini hana nguvu yoyote ya kuchangia sera za chadema kwani wenye kura nyingi ni madiwani wa ccm!!!


sasa ngome iko wapi?
Hii ishu ni kweli namlidhani kuwa mtapata wananchi wengi kwa kuwateka kisaikolojia watu wa chadema. pia inaonesha namna gani CCM haiheshimu utawala wa sheria kwa kunyonga demokrasia. mmelazimisha mkutano huo. Mmmekosa wasikilizaji mpaka wale wanachama feki wa kurejesha kadi mmekosa pia.

halafu mnatumia pesa ya umma kutoa ulinzi wa UwT kwa mgombea mwenza wakati hana status yeyote bado. Mnaona mlivyo malunatic????? Tunajua kuliko mnavyofahamu.


 
Watu wengine hawatumii hata hekima. Yaani, watu unaenda kuwaomba kura, bado unawafanyia ubabe hao hao! Labda wameshakata tamaa ya kupata kura za wananchi wa kawaida sasa wanajaribu kulinda za wanaccm wenzao.
 
Watendaji wa serikali wanaopindisha sheria kwa ajili ya kupendelea CCM wanakosa busara. Watatimuliwa siku za karibuni.
 
Watu wengine hawatumii hata hekima. Yaani, watu unaenda kuwaomba kura, bado unawafanyia ubabe hao hao! Labda wameshakata tamaa ya kupata kura za wananchi wa kawaida sasa wanajaribu kulinda za wanaccm wenzao.

UmkhontoweSiwezi niliwahi kuuliza CCM inategemea kura za maruhani kushinda? Kwani vitendo vyao dhidi ya wapiga kura si vya mtu anaetegemea kura za huyo anayemdhihaki na kumdhalilisha.
 
Someni sheria mbona iko wazi mno? Mgombea urais anapewa priority kuliko wagombea ubunge au udiwani.

Kama kwenye eneo husika kuna mgombea urais, kampeni zingine zote zinasimama.

Bila kuzielewa sheria mtakuwa mnalia kila siku na kusingizia kuonewa.

Hata Slaa akienda eneo husika, mikutano ya wabunge inabidi isimame.
 
Nimecheka sana hii:

upambwe kwa kurejeshwa kwa kadi za CHADEMA ambazo wamezitengeneza wenyewe
Imenikumbusha ile ya Mr. Bien ya kujiandikia kadi ya birth day.
Kazi ipo!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom