Kamende
JF-Expert Member
- Mar 1, 2008
- 416
- 45
Kwa wale wanaoujua mji wa Moshi wataweza kufuatilia kirahisi sana namna ambavyo uamuzi huu uluvyofanyika bila kufuata ukweli wa kisheria wala kimazingira.
Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi Mgombea Mwenza wa kiti cha urais kwa tiketi ya CCM Dr. Ghalib Bilal alikuwa awe mjini Moshi kesho tr. 18/10/2010. Badala yake amefika leo.
Baada ya CCM kujua kuwa Bilal atakuwepo Moshi leo walimwandikia barua Msimamizi wa uchaguzi wakimtaka ahamishe mkutano wa mgombea ubunge bw. Salakana kutoka katika kata ya Longuo B kwenda Pasua. Barua hiyo badala ya kusubiri ama kuitishiwa kikao cha pamoja cha makatibu wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi mjini Moshi ilijibiwa na Msimamizi mwenyewe kwa kuwaruhusu kufanya mkutano wanavyoona wenyewe inawafaa.
Hatua iliyofuatia Msimamizi leo amepeleka barua kwa Katibu wa CHADEMA Manispaa ya Moshi akimweleza kusitisha mkutano wa chama hicho katika kata ya Bondeni ili kupisha mkutano wa Bilal ufanyike bila usumbufu wowote.
Akielezewa kuwa mikutano hiyo iko kata tofauti Msimamizi alijibu kuwa Mkutano uko katika barabara ambayo CCM watapita wakienda kwenye mkutano wao.
Nalo jeshi la polisi mkoani hapa baada ya kupewa nakala ya barua hiyo wamepeleka magari yaliyojaza askari wa FFU wenye silaha katika uwanja ambao CHADEMA wangefanyia mkutano. Kuanzia saa 7.30 mchana leo gari la maji ya kuwasha limekuwa likivinjari katika mitaa ya Moshi kama tishio kwa yeyote atakayethubutu kwenda katika mkutano wa CHADEMA.
Muda huu nimepata habari kuwa mkutano wa Bilal ambao ulikuwa upambwe kwa kurejeshwa kwa kadi za CHADEMA ambazo wamezitengeneza wenyewe umekuwa na mahudhurio mabaya sana.
Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi Mgombea Mwenza wa kiti cha urais kwa tiketi ya CCM Dr. Ghalib Bilal alikuwa awe mjini Moshi kesho tr. 18/10/2010. Badala yake amefika leo.
Baada ya CCM kujua kuwa Bilal atakuwepo Moshi leo walimwandikia barua Msimamizi wa uchaguzi wakimtaka ahamishe mkutano wa mgombea ubunge bw. Salakana kutoka katika kata ya Longuo B kwenda Pasua. Barua hiyo badala ya kusubiri ama kuitishiwa kikao cha pamoja cha makatibu wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi mjini Moshi ilijibiwa na Msimamizi mwenyewe kwa kuwaruhusu kufanya mkutano wanavyoona wenyewe inawafaa.
Hatua iliyofuatia Msimamizi leo amepeleka barua kwa Katibu wa CHADEMA Manispaa ya Moshi akimweleza kusitisha mkutano wa chama hicho katika kata ya Bondeni ili kupisha mkutano wa Bilal ufanyike bila usumbufu wowote.
Akielezewa kuwa mikutano hiyo iko kata tofauti Msimamizi alijibu kuwa Mkutano uko katika barabara ambayo CCM watapita wakienda kwenye mkutano wao.
Nalo jeshi la polisi mkoani hapa baada ya kupewa nakala ya barua hiyo wamepeleka magari yaliyojaza askari wa FFU wenye silaha katika uwanja ambao CHADEMA wangefanyia mkutano. Kuanzia saa 7.30 mchana leo gari la maji ya kuwasha limekuwa likivinjari katika mitaa ya Moshi kama tishio kwa yeyote atakayethubutu kwenda katika mkutano wa CHADEMA.
Muda huu nimepata habari kuwa mkutano wa Bilal ambao ulikuwa upambwe kwa kurejeshwa kwa kadi za CHADEMA ambazo wamezitengeneza wenyewe umekuwa na mahudhurio mabaya sana.