ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 62,123
- 72,412
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeweka Mawakala 666 katika Vituo 666 vya kuandikisha Wapigakura huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ikiweka Mawakala 55.
Msimamizi wa Uchaguzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dk. Frederick Sagamiko amesema hayo wakati mkoani humo wakati akikanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mwenendo wa uandikishaji kuwa wanaandikishwa mamluki kwenye orodha ya wapigakura.
Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina jumla ya vituo 666 vya kujiandikishia wapiga kura na vyama vyote 19 vya siasa vyenye usajili wa kudumu ambavyo vinashiriki uchaguzi mkuu vimeruhusiwa kuweka mawakala wao katika kila kituo.
“Naomba nichukue nafasi hii kuwataarifu kwamba ni vyama viwili tu vilivyofanikiwa kuweka mawakala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefanikiwa kuweka mawakala 666 katika kila kituo na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamefanikiwa kuweka mawakala 55.” Alisema.
Sagamiko alisema Chadema wameweka mawakala katika Kata sita, kati ya Kata 41 zilizopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambazo ni Kikombo (9), Kikuyu Kaskazini (12), Chamwino (7), Chihanga (4), Ng’hong’onha (19) na Mbabala (4).
Aidha, alivitaka vyama vya siasa kufuata kanuni na miongozo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili uchaguzi uwe wa huru na wa demokrasia na kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kutokushiriki katika uvunjifu wa amani katika maeneo ya vituo na kuzingatia kanuni ambazo tayari walishagawiwa.
Pia amewataka wananchi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wenye sifa za kujiandikisha kujitokeza na kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura ili waweze kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa.
Swali.
Kwa staili hii hamuoni Aibu kuingia kwenye uchaguzi? 😂😂😂😂😂😂
Chama Cha X zamani Twitter mnaona mnavyopuuzwa? Tuliona kwenye maandamano ya kutaka kuleta vurugu Hadi huku mtaani.
Mafuriko ya mitandaoni Huwa yanawadanganya sana na bahati mbaya hamjifunzi.Watu wenye uwezo wa kununua bando hawafiki hata 5% ya Watanzania wote,mkiangukia Pua Utasikia tumeibiwa 😂😂😂
Msimamizi wa Uchaguzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dk. Frederick Sagamiko amesema hayo wakati mkoani humo wakati akikanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mwenendo wa uandikishaji kuwa wanaandikishwa mamluki kwenye orodha ya wapigakura.
Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina jumla ya vituo 666 vya kujiandikishia wapiga kura na vyama vyote 19 vya siasa vyenye usajili wa kudumu ambavyo vinashiriki uchaguzi mkuu vimeruhusiwa kuweka mawakala wao katika kila kituo.
“Naomba nichukue nafasi hii kuwataarifu kwamba ni vyama viwili tu vilivyofanikiwa kuweka mawakala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefanikiwa kuweka mawakala 666 katika kila kituo na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamefanikiwa kuweka mawakala 55.” Alisema.
Sagamiko alisema Chadema wameweka mawakala katika Kata sita, kati ya Kata 41 zilizopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambazo ni Kikombo (9), Kikuyu Kaskazini (12), Chamwino (7), Chihanga (4), Ng’hong’onha (19) na Mbabala (4).
Aidha, alivitaka vyama vya siasa kufuata kanuni na miongozo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili uchaguzi uwe wa huru na wa demokrasia na kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kutokushiriki katika uvunjifu wa amani katika maeneo ya vituo na kuzingatia kanuni ambazo tayari walishagawiwa.
Pia amewataka wananchi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wenye sifa za kujiandikisha kujitokeza na kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura ili waweze kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa.
Swali.
Kwa staili hii hamuoni Aibu kuingia kwenye uchaguzi? 😂😂😂😂😂😂
Chama Cha X zamani Twitter mnaona mnavyopuuzwa? Tuliona kwenye maandamano ya kutaka kuleta vurugu Hadi huku mtaani.
Mafuriko ya mitandaoni Huwa yanawadanganya sana na bahati mbaya hamjifunzi.Watu wenye uwezo wa kununua bando hawafiki hata 5% ya Watanzania wote,mkiangukia Pua Utasikia tumeibiwa 😂😂😂