SANCTUS ANACLETUS
JF-Expert Member
- Mar 5, 2016
- 3,337
- 4,664
Hiyo ni mila ya Kikafiri sio ya Kiislam hao wanakusudia kuuchafua uislam tangu lini Shia akawa Muislam
Hiyo inakusudiwa kusafisha waislamu na sio kuwanajisi.Kuwatenga waislamu wadhambi wasiingie Misikitini ndio kuunajisi Uislamu wenyewe.Kuwatenga wanawake waislamu wasichangamane na waislamu wanaume wakati wa kusali ndio kuukafikirisha uislamu huko.
Msikitini kunafanyika dua mbele ya Munyazimungu.Kwani nini uwatenge waumini wakati shida yenu na hitaji la wote ni hilo hilo tu?
Kwani msikitini kunafanyika mambo ya siri ambayo wanawake hawatakiwi kuyaona wanaume wakiyafanya?
Hapa tumelalamika kuibiwa dhahabu kwa wingi kupitia maboso (makanikia) kusafirishwa tokana na kukosa Smelter ya kuchenjulia.Msikiti au Kanisa ni Smelter.Humo "wanachenjuliwa" wenye dhambi ili kupata watu wema( dhahabu na madini safi). Sasa ikiwa tuna makanikia na hatutaki yawekwe kwenye smelter dhahabu itapatikana vipi?
Sisi tunaokataa wanawake na mashoga wasijumuike na watu wengine misikitini ndio tunasababisha makanikia( watu wakosefu) waibiwe na shetwan.