Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,761
- 71,144
My take;
Hili ni kweli kabisa. Kuwa kwa kesi hii na ukubwa wake IGP Sirro, DPP, DCI na hata mkurugenzi wa TISS wote wanajua kuwa polisi wanaokwenda kutoa ushahidi wanapangwa ili watoe ushahidi wa uongo.
Na kwamba wanamdanganya hata Rais (maana kwa kesi ya aina hii lazima ahoji) kuwa kesi inakwenda kwa haki. Je, watu wenye nafasi nyeti kama hizo kushirikiana kumdandanya Rais sio HATARI kwa taifa?
Au uongo huo wanataka tuamini kuwa Rais naye anashiriki? Hatutaki kuamini hivyo maana urais ni taasisi na ikifikia huko basi utawala unakuwa umefitinika kama awamu ya tano.