TEAM 666
JF-Expert Member
- Dec 7, 2017
- 4,330
- 8,421
Nasikia leo kwenye msafara wakupokea mwili wake moja ya gari yake ilikuwa ikiwaka motoWatu wamekua wakijiuliza kweli kama Bilionea huyu alikua na jeneza ndani..kutoka Makao Makuu Ya Zimbabwe Jijini Harare Mwanamitandao ya kijamii na mfanyabiashara, Genius Ginimbi Kadungure ambaye alikufa katika ajali ya gari Jumapili alikuwa ameripotiwa kununua jeneza lake wiki moja kabla ya kifo chake.
Kulingana na majukwaa ya habari ya Pindula, inadaiwa kuwa jeneza hilo lilipatikana katika moja ya vyumba vyake vya kulala kufuatia kifo chake.
Na ukweli kuhusu kifo chake ni kwambaa baada ya ajali na gari kushika moto ginimbi alifanikiwa kutoka nje ya gari, alichofanya ni kujaribu kuwafungulia milango rafiki zake wakati milango ya rolls royce ilikua imejilock basi ndipo mlipuko ukatokea na yeye akiwapo pale anaangaika kuwafungulia milango wenzie.
Hivyo habari za uzushi kua yawezekana alikosea masharti ni porojo tu, niseme upendo kwa wenzie ndio ulikua mkubwa zaidi, yeye kama yeye alishatoka nje tayari hivyo alikua na muda wa kusogea mbali zaidi na mlipuko.
Utajiri wa "jeneza" ni mzuri naupenda sababu hauna lawama.
R.I.P GINIMBI..you enjoyed life to the fullest.