Msigwa amuomba mzee Mtei akaongee na Kinana ili wayamalize!

HAMY-D

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
7,149
3,817
Wana-JF!

Kuna taarifa kuwa mchungaji Msigwa amemuomba mzee Mtei ambae ni muasisi wa CHADEMA akaongee na bwana Kinana ili wasuruhishe mgogoro kati yake mchungaji Msigwa na Kinana baada ya tuhuma zake kwa Kinana kuwa ni jangili.

Inasemekana mchungaji Msigwa amefikia maamuzi hayo baada ya kuona hatma mbaya ya kesi hiyo kwa kukosekana kwa ushahidi usio na shaka wenye kuthibitisha kuwa bwana Kinana ni jangili na anajihusisha na kusafirisha pembe za ndovu.

Mchungaji Msigwa baada ya kuona mambo yamefika maji shingo ndipo hapo akaona ni vyema amuombe mzee Mtei kwa kuwa ana hekima na busara ili akamuombee radhi kwa bwana Kinana ili aifute kesi hiyo mahakamani.
 
HII id ni ile badala ya Tuntemeke kwa hiyo wana JF hakuna sababu ya kuhangaika na kikundi cha majamba aka masalia aka chale za m.a ---- aka kuua panya wote jana ulileta hii thread ikabutuliwa leo umeirudia the great liar
 
Ulikuwepo wakati anamwona Mzee Mtei. Shida yako ni elimu ndogo, Maana elimu ndogo ni sumu.

Leta mambo ya maana watu wenye fikra finyu huongea juu ya watu lakini wenye fikra pana huongelea na kujadili Masuala makubwa sio Umbea umbea tu.
 
Wana-JF!

Kuna taarifa kuwa mchungaji Msigwa amemuomba mzee Mtei ambae ni muasisi wa CHADEMA akaongee na bwana Kinana ili wasuruhishe mgogoro kati yake mchungaji Msigwa na Kinana baada ya tuhuma zake kwa Kinana kuwa ni jangili.

Inasemekana mchungaji Msigwa amefikia maamuzi hayo baada ya kuona hatma mbaya ya kesi hiyo kwa kukosekana kwa ushahidi usio na shaka wenye kuthibitisha kuwa bwana Kinana ni jangili na anajihusisha na kusafirisha pembe za ndovu.

Mchungaji Msigwa baada ya kuona mambo yamefika maji shingo ndipo hapo akaona ni vyema amuombe mzee Mtei kwa kuwa ana hekima na busara ili akamuombee radhi kwa bwana Kinana ili aifute kesi hiyo mahakamani.

Ish!! Tangu lini Mzee Mtei akawa Mzee wa Busara.
 
KAMATA.gif
Hata afanyeje huyu Msomali achomoki kwenye hii kesi ya ujangili. HILI NI JANGILI LA KIMATAIFA
 
Kutumiwa huku mi hata sikuwezi halafu baada ya muda hua wanatoweka Tu....kuna mpumbavu mwingine alikua abapost Mara zaidi ya ishirini kwa dakika, sijui keshapewa ukuu WA wilaya maana haonekani tena sasa
 
Nkumbuka miaka ile ya 90, jamaa alipokuwa mbunge wa Arusha mjini, NCCR- Mageuzi walimpania na kashfa ya uraia. Umafia ulitumika kuiba file lake, jamaa akakimbilia Havard kusubiri upepo upite. Mchungaji msigwa usiwe na haraka, kwanza tutaanza na uhalali wa Uraia wake, Biashara zake zote na Uwakala wake wa meli. Kesi hii ni ndogo, mwanafunzi wa sharia wa mwaka wa pili UDSM atashinda
 
Unamtetea jangili wa tembo?

Ushahidi mnao? mimi sitaki kuwa msukule wa kuamini mambo bila ushahidi, endapo ushahidi ukipatikana, basi Kinana tunamtoa kwenye nafasi yake ya sasa kwenye chama.

Ila ni mwendawazimu tu ndie atakae amini maneno ya kuropokwa majukwaani bila ya ushahidi.

Msigwa anamuomba Kinana a-withdraw kesi, wewe upo humu unashika bango kuwa Kinana jangili. Je, wewe una akili sawasawa?
 
Mkuu, kwani ni lazima uandike kitu? maana unapoteza muda na raslimali zako bure, kwani comments yoyote yenye lengo la kuharibu mjadala ni LAZIMA ifutwe, sasa kufanya hivi haunisumbui mimi wala Mods, ila unajisimbua wewe.

Jisomeeni sheria za JF jamani ili mjifunze kufanya mijadala kwa heshima na nidhamu inayo tatikana.

Nakupa pongezi sana kwa kujituma ku-post karibu kila siku ila kwanini siku zote huwa una-post habari za upande mmoja tu pia na upande mingine unaonyesha weakness
 
Nkumbuka miaka ile ya 90, jamaa alipokuwa mbunge wa Arusha mjini, NCCR- Mageuzi walimpania na kashfa ya uraia. Umafia ulitumika kuiba file lake, jamaa akakimbilia Havard kusubiri upepo upite. Mchungaji msigwa usiwe na haraka, kwanza tutaanza na uhalali wa Uraia wake, Biashara zake zote na Uwakala wake wa meli. Kesi hii ni ndogo, mwanafunzi wa sharia wa mwaka wa pili UDSM atashinda

Nikutumie mawasiliano ya Msigwa ili umpe matumaini?

Mwenzako ana akili ndio maana ameona hatma ya hii kesi ni 'defamation', fidia yake si chini ya Tshs 1 billion, sasa kama una ushahidi fanya umsaidie au lah atafilisiwa yeye na CHADEMA yake.
 
Back
Top Bottom