Msidanganywe eti sasa hivi hali ya maisha ughaibuni ni rahisi

hao mabinti wanaopewa talaka kwa sababu ya haki ngumi waambie wajilipue waje Bongo hawatojutia....huku unaweza kuwa na madanga nane....unacollect 50k kwa kila mmoja per day...
Kwahiyo unataka kutuambia wadangaji waliopo hapa bongo Wana collect 8 *50000=400000/- kwa siku? Wanaotoa 50000 kwa malaya Hawa wapo mkoa gani?
 
Unachokisema ni sawa kabisa, sasaivi kumeoza but tuvute subra pengine 2022 kutatulia

Miongoni mwa vitu vinavyonitia Stress ni Arsenal nakosa furaha na najihisi hasira sana kila inapofungwa
Pole mkuu nimeona arsenal Wana nguvu kuliko timu yoyote kwenye EPL, maana kabeba timu zote.
 
Wapolishi wanajitumaga kubeba boksi sana halafu mabaguzi kichizi
Aisee hii mbegu ya kizungu ni wabaguzi sijawahi ona! Niliwahi kufanyiwa tukio la uongo kazini na wadada wa kipolishi! Kilichoniokoa kwenye lile kundi kulikuwa na mmoja wao alikuwa amenihusudu na alikuwa rafiki sana ndio akakanusha kwenye kikao kuwa tukio ni la uongo na walilipanga ili nifukuzwe maana nilikuwa naelekea kuwa manager wa kile kitengo na akaonyesha meseji walizokuwa wakitumiana kupanga mkakati, walisingizia nimemshika matako mwenzao!
 
Duuu kwahiyo nisikilizie kwanza,maana nishaanza kuchukua hatua za kujilipua Scandinavian countries Aisee!
Bongo ngumu Sana Aisee,Bora nusu Shari kuliko Shari kamili!

Tunatishana Sana ndugu zanguni!
Umeshaambiwa kuna msosi wa bure huko kila siku saa nne asubuhi..mambo hayo hapa bonho umeona wapi?? ..

Nenda kapambane kiume wakati wa crisis ndio wengine huona fursa hjko nakufanikiwa kiuchumi
 
Mkuu uliamua tu kurudi. Inaonekana mambo yako bongo swafi hadi unarudi kwa hiari. Mkuu lakini wakati huo wewe unarudi Norway mambo yalikuwa safi sana nakumbuka kuna show ray c ilikuwa aperform hakuja na watu walichanga hela nadhani ilikuwa 2020 walimmaindi kichizi
Mkuu usiongee usichokijua nina nyumba nne selfu bongo. Nina mashamba ya kutosha. Gari lilikuwepo wakaliharibu nikasema this is bullshit. Na hela tu ya kutosha savings ninayo. Mabenki hapa kila uchwao wananiomba nichukue mortgages na mkopo credit yangu ipo safi. Niko qualfy kuchukua hata mkopo wa million 200 za kibongo. Karibuni nafile citizenship hapa pata hii passport nyekundu. Sina shida
Nilikwenda usa mkuu.
 
Nyie vijana muende wote ulaya mkabebe maboksi lkn siku mkiamua kurudi asilimia 99.9 mtakuwa hoi mnarudi na nguo na viatu
 
Nilipokuwa USA, Walmart nishabeba boksi kwa sana. ICA, Meny, Rema 1000, Rimi, Coop, Kiwi, Bunn Pris, Nille, Burger King, Frelseesarme aka Salvation Army, Adecco, Manpower nishafanya kazi sehemu kibao Oslo na vitongokji jirani.
 
Mkuu ni vizuri mtu aje ajionee. Kuna Dogo flani mwaka jana alikuja kusoma huku. Kaingia kwa mbwembwe nikamtahadharisha asiweke ekspekteshen sana aende tu taratibu l. Nilikutana naye majuzi kati kawa mpolee.

Wachumi wametabiri hali itaanza kujirudia kawaida kwaanzia mwanzoni 2023. Fikiria walioajiriwa walikuwa wanapokea mishahara kama milion saba hadi 10 za bongo sasa wanaishi kupitia social benefits na government assistance and handouts ndo chanzo che dipreshen suicide na talaka na zimekithiri sasa. Hakuna shida mbaya kwa binadamu kukosa helamfukoni. Hasira sasa zimegamia kwetu wahamiaji
Wahamiaji mnachukua madili
 
Kuna bwana mmoja ameomba kujua abcd za nchi iitwayo austria.

Austria ya vienna..achana na ile ya sydney.

Unganisheni na uturuki.
anapoishi mbwana.
 
Mzuka wanajamvi!

Nitasema tu ukweli. Hali ya maisha sasa hivi ughaibuni / ulaya ama mamtoni ni ngumu sana.

Maisha yamekuwa Magumu sana hasa kwaanzia mwezi wa tatu mwaka jana baadaya hii Corona.

Maelfu na Maelfu wamepoteza kazi zao na kujiandikisha kwenye employment benefits.

Kazi za kubeba boksi ni za kugombania. Mfano mzuri tu Denman Norway na Sweden. Nayosema haya ni kweli kwaanzia kufagia kazi za jikoni hotelini usafi na ujenzi yani kuna uhaba. Na ukipata hizo kazi basi sana sana ni mara mbili kwa wiki au tatu tena kwa masaa machache machache.

Kingine usidanganywe eti ni rahisi tu sasa hivi ukapata visa halafu uje huku ukafanikiwa mara moja l.

Sasa kuna ushindani mkubwa kwenye hizi kazi za kubeba boksi kutoka kwa mataifa ya eastern European Polish, Ukrainians, Estonians na wengine. Pia jamii ya kihindi Nepalese, bangladeshi, pakistani na wahindi wanapewa sana kipaumbele hasa kwenye kusafisha meli na huko napo wamepunguzwa wengi safari za meli sasa hivi zimepungua.

Sasa hivi hadi baadhi ya marubani na flight attendants wa SAS Scandinavia airline wanafanya food delivery kusambaza msosi majumbani ndo angalau angalau sasa hivi ndo kazi ya boksi inayolipa.

Ni wale tu wanaofanya kazi kwa wazee ndo hawajaathiriwa na wanaingiza hela ndeefuuu kichiz nawaona mabinti wadogowadogo wanaendesha ndinga za hatarii. Kozi za kutunza wazee nizakugombaniwa kwasababu unakuta wote wenye degrees masters hadi phd za uchumi, biashara computer sayans wanagombania hizi kozi za unesi za kutunza wazee ambazo ziko kwenye level za VETA za huku.

Denmark kuna ile GreenCard yao sasa waliopata wakobmatatani kuderpotiwa kwasababu hawana kazi wamepunguzwa haki za binadamu wanajitahidi kuingilia kati kuwasaidia kwasababu ni janga limesababisha na hali hadi itulie ni mwanzoni 2023. Ila immigration policy ya Denmark siyo rafiki kabisa kwa wahamihaji. Na sasa vyama vyenye mrengo wa far rights ndo zinasomba Scandinavia. Norway ni center right kitatoka, Sweden ni left kitatoka, fina land ni left nacho kitatoka na vyote agenda ni immigeation. Na hivi viko serikalini nao wanakaza hili kuwafurahisha Wananch.

NASEMA UKWELI HAMNA KAZI ZA KUMWAGA ZA KUBEBA BOKSI SASA HIVI ULAYA. NA MSIDANGANYWE ETI UTASAIDIWA KUJA HUKU MAMBO YA KAENDA VIZURI.
Nikweli ni mbaya unaumia nini, Bora mchawi kuliko wewe! Wivu tu
 
Mkuu ni vizuri mtu aje ajionee. Kuna Dogo flani mwaka jana alikuja kusoma huku. Kaingia kwa mbwembwe nikamtahadharisha asiweke ekspekteshen sana aende tu taratibu l. Nilikutana naye majuzi kati kawa mpolee.

Wachumi wametabiri hali itaanza kujirudia kawaida kwaanzia mwanzoni 2023. Fikiria walioajiriwa walikuwa wanapokea mishahara kama milion saba hadi 10 za bongo sasa wanaishi kupitia social benefits na government assistance and handouts ndo chanzo che dipreshen suicide na talaka na zimekithiri sasa. Hakuna shida mbaya kwa binadamu kukosa helamfukoni. Hasira sasa zimegamia kwetu wahamiaji
Vipi hali imeshakaa sawa?
 
Back
Top Bottom