Msichana wa Kitanzania akipata mchumba na kufunga ndoa anajiona amepata degree (Hons)!

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,804
18,231
Hodi humu jamvini wana MMU,

Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi bila kuwachosha. Najua mnahangaika na utafutaji wa maji na mkate kwa familia wakati huu.

Kwa sababu ya suala la kuolewa kuwa gumu siku hizi binti akiolewa anajiona kama amepata degree (Hons) ya first class. Siyo siri ukimpa uchaguzi binti yako kama umlipie fedha asome degree yoyote au aolewe, bila kuchelewa wala kupepesa macho atachagua kuoelewa. Hasa ikiwa huyo mwanaume anayemchumbia ni mtoto wa kishua, utakuta amejiozesha mwenyewe bila mahari!

1668077201179.png


Juzi nilikuwa natatua kesi ya binti wa kidato cha III mwenye umri wa miaka 17 aliyeamka usiku wa saa 5 na kumfuata mwanaume mwenye umri wa miaka 23 mtaa wa pili. Huyu binti anaishi na mama wa kambo anayefanya kazi baa. Kwa kawaida, mama hurudi kutoka kazini kuanzia saa 7 usiku. Sasa siku hiyo mama alirudi mapema kabla ya saa 7 akakuta binti ametoka. Arobaini za binti zikawa zimefika.

Huyu binti hulala chumba cha uani, hivyo nafikiri ulikuwa ndiyo mchezo wake wa kila siku. Dada yake aliacha shule akiwa Kidato cha II akaolewa na lofa mmoja asiyekuwa na mbele wala nyuma. Sasa hivi anajishughulisha na uuzaji wa mboga nyumba kwa nyumba. Mdogo wake naye anatamani kuacha shule akaolewe. Hajajifunza chochote kutokana na makosa ya dada yake. Wanawake wa kizazi hiki ni kama nyani, hawajatulia hata kidogo. Hivi nyie mabinti wa kisasa mna nini lakini?

Ndoa imekuwa kama kilele cha mafanikio ya msichana. Huu ukuta unahitaji kubomolewa, hili ni gereza la kuyafunga maono ya msichana. Kuolewa ni maono ya chini kabisa, msichana unaweza kuwa na ndoto kubwa zaidi ya hii; ota ndoto kubwa zaidi.
 
Kwenye Jamii yetu mwanamke aliyeolewa ana thamani kubwa kuliko ambae hajaolewa.

Ndio maana humu thread za kuwasema ambao hawajaolewa na umri umeenda na wengine hata kuamua kuzaa tu haziishi.

Kabla hujawanyooshea vidole hao wanaokimbilia kuolewa, basi Anza kuinyooshea jamii kidole, Kwa kutufanya wanawake tujione bila ndoa si lolote na si chochote. Na aliyeolewa ndio mjanja.
 
To each their own....

Kwa Mtizamo wako inaonyesha hio Degree Hons kwako ni kipimo cha mafanikio....

Wakati huenda kwa mmasai sio miaka mingi nyuma ingeonekana umepoteza muda wako.

Wakati kwa Watawa huenda wakaona njia yao ya kutumikia ni bora zaidi..., bila kusahau yule aliyesomeshwa na kijiji na ni wa kwanza kupata degree hadi mtaa ukawa named after yeye might have different thoughts
 
Kwenye Jamii yetu mwanamke aliyeolewa ana thamani kubwa kuliko ambae hajaolewa.

Ndio maana humu thread za kuwasema ambao hawajaolewa na umri umeenda na wengine hata kuamua kuzaa tu haziishi.

Kabla hujawanyooshea vidole hao wanaokimbilia kuolewa, basi Anza kuinyooshea jamii kidole, Kwa kutufanya wanawake tujione bila ndoa si lolote na si chochote. Na aliyeolewa ndio mjanja.
Tatizo wanawake wa siku hzi mnaanza kutumika katika umri mdogo sana ndio maana thanami yenu ya kuolewa imeshuka. Sio ajabu kumkuta mtoto wa miaka 15 amEtombekA na wanaume wasiokuwa na idadi hadi amekata hisia kule chini. Sasa mtu kama huyu unamuoa wa nini?
 
Kwenye Jamii yetu mwanamke aliyeolewa ana thamani kubwa kuliko ambae hajaolewa.

Ndio maana humu thread za kuwasema ambao hawajaolewa na umri umeenda na wengine hata kuamua kuzaa tu haziishi.

Kabla hujawanyooshea vidole hao wanaokimbilia kuolewa, basi Anza kuinyooshea jamii kidole, Kwa kutufanya wanawake tujione bila ndoa si lolote na si chochote. Na aliyeolewa ndio mjanja.
- Sielewi kwa nini wanawake wanaongelewa sana, kulingana uwiano wa Ke na Me kwenye matokeo ya sensa, kama wanawake hawaolewi inamaanisha kuna wanaume hawajaoa. Thamani ya ndoa ipo kwa wote ME na KE. Mwanaume pia kama hana mke huonekana hana thamani bila kujali elimu, pesa wala umri.
 
FYI ndoa ni one of the greatest achievement kwa mwanamke

Ukiolewa unajiona kama uko na security fulani hivi
Mawazo haya yananitia uchungu sana!!!! Nina binti yangu (now 31 yrs) naona hili jambo linamfanya asianze PhD programme ati kila siku kwenda kusali. Inaniboa saaana ingawa sina la kufanya. Naamini kuolewa kupo na ukiolewa ukiwa na status ndiyo inakuwa bora zaidi au nakosea kama mzazi
 
Unaangalia upande mmoja tu wa shilingi, isitoshe Wanawake hawaolewi na mtu yoyote tu bali yule anaye qualify pia, kuna Wanaume wengi tu hawapati Mwanamke wa kuoa au mwanamke wa chaguo lao kwa maana wanawake wanaowataka wanawakataa pia, ni nature.

Hivyo hata kwa Wanaume kupata Mwanamke wa chaguo lao na akakukubali pia ni ishu!
 
Sisi ndo tunaowapeleka watoto wa kike kuwa na hiyo mentality.

There is more to life than just marriage. Am a strong advocate of marriage having been married myself lakini I never throw stones at single moms or people who have opted not to get married.

Napenda msichana awe focused, alinde usichana wake, na heshima yake. Asome au afanye biashara ajijenge kiakili na kifedha halafu aingie kwenye ndoa akiwa stable upstairs and pocketwise.

Money is always a woman's insurance.

Wadada jijengeni. Travel the world..... Soar as high as you can. Marriage shouldn't be the end of your dreams.
 
Sisi ndo tunaowapeleka watoto wa kike kuwa na hiyo mentality.

There is more to life than just marriage. Am a strong advocate of marriage having been married myself lakini I never throw stones at simgle moms or people who have opted not to get married.

Napenda msichana awe focused, alinde usichana wake, na heshima yake. Asome au afanye biashara ajijenge kiakili na kifedha halafu aingie kwenye ndoa akiea stable upstairs and pocketwise.

Money is always a woman's insurance.

Wadada jijengeni. Travel the world..... Soar as high as you can. Marriage shouldnt be the end of your dreams.
Barikiwa
 
Mawazo haya yananitia uchungu sana!!!! Nina binti yangu (now 31 yrs) naona hili jambo linamfanya asianze PhD programme ati kila siku kwenda kusali. Inaniboa saaana ingawa sina la kufanya. Naamini kuolewa kupo na ukiolewa ukiwa na status ndiyo inakuwa bora zaidi au nakosea kama mzazi
Mwenzio kachoka kupiga selfie🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom