Msichana wa kazi za ndani

Husninyo

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
23,724
9,188
Anahitajika housegirl umri wowote. Atakaa kwa mwajiri. Awe msafi. Mshahara elf 30 kwa mwezi.
 
Wanasumbua sana siku hizi,mi binafsi kwa mwaka huu wamepita mabei 3 wanne na wameshalala mbele,ukipata wa bush anaweza kaa kidogo.La sivyo uka hire wa kimjini mjini lakini ndo hawatulii,wako ki mishe mishe.
 
Hivi kweli mtu analipwa 30,000 tu!
Kumbuka kuwa huyu anayelipwa 30 elfu anaishi na familia. Na nahisi ni bora huyu anayelipwa 30 kwa kukaa na familia kuliko anayelipwa 100,000 wa kwenda na kurudi. Huko nje hesabu hasikubali kuishi kwa 100,000 kwa mwezi, lakini pale anapata malazi na chakula, (mara nyengine hufaidika na nguo na zawadi nyengine) na hakuna usafiri.
Kwa mfano, kiweka usafiri kwa mwezi (3.00X2X30= 18,000); + chakula tuseme 30,000 kwa wastani wa 1000 kwa siku, kodi ya chumba 30,000 minimum; huyu anayelipwa 30,000 tayari kasevu 78,000 kama angelikuwa wa kwenda na kurudi.
Hata hivyo, sikusudii kusema kuwa 30,000 ni nyingi, la hasha. Hawa wa kukaa na familia walipaswa kulipwa angalau 150,000 na wale wa kwenda na kurudi angalau 300,000 kwa mwezi.
 
Wanasumbua sana siku hizi,mi binafsi kwa mwaka huu wamepita mabei 3 wanne na wameshalala mbele,ukipata wa bush anaweza kaa kidogo.La sivyo uka hire wa kimjini mjini lakini ndo hawatulii,wako ki mishe mishe.
<br />
<br />
ni kweli wanasumbua ila hakuna namna.
 
Kumbuka kuwa huyu anayelipwa 30 elfu anaishi na familia. Na nahisi ni bora huyu anayelipwa 30 kwa kukaa na familia kuliko anayelipwa 100,000 wa kwenda na kurudi. Huko nje hesabu hasikubali kuishi kwa 100,000 kwa mwezi, lakini pale anapata malazi na chakula, (mara nyengine hufaidika na nguo na zawadi nyengine) na hakuna usafiri.<br />
Kwa mfano, kiweka usafiri kwa mwezi (3.00X2X30= 18,000); + chakula tuseme 30,000 kwa wastani wa 1000 kwa siku, kodi ya chumba 30,000 minimum; huyu anayelipwa 30,000 tayari kasevu 78,000 kama angelikuwa wa kwenda na kurudi.<br />
Hata hivyo, sikusudii kusema kuwa 30,000 ni nyingi, la hasha. Hawa wa kukaa na familia walipaswa kulipwa angalau 150,000 na wale wa kwenda na kurudi angalau 300,000 kwa mwezi.
<br />
<br />
mkuu hiyo mshahara wa 300,000/= kama bossi wake mwalimu wa primary analipwa mshahara less than hiyo atatapata wapi hela ya kumlipa hg laki 3.
Kibongo bongo bado sana. Tena wengine wanalipwa elf 10 hadi 20.
 
Ila wanaibaga ela za mboga..hizo ndio posho zao.

zile unazowaibia kwa kutumia karatasi ndo hizo na yeye anaziridisha kwa njia isiyo rasmi, teh teh teh! nakutania tu mkuu usije ukanitoa roho, mie sio m'''kwere
 
Anahitajika housegirl umri wowote. Atakaa kwa mwajiri. Awe msafi. Mshahara elf 30 kwa mwezi.

heshima mbele...

fikiria mwajiri wako angetaka kukuajiri, uishi nyumbani kwake na kisha akulipe hizo elfu 30 ungejisikiaje?

tufike pahala tujisikie aibu kutangaza vitu kama hivi......hata kama tunafanya basi na iwe kimya kimya..kutangaza ni sawa na kuona tunachokifanya ni sawa..

tufike pahala tuone kuwa ajira ni msingi wa kumfanya mtu aweze kuishi maisha ya kujitegemea na kinyume chake ni unyonyaji.
nadhani ni haki hasa kwamba hivi sasa imekuwa ni dhiki kubwa kupata mabeki tatu...pongezi kwa shule za kata...pamoja na mapungufu yake lakini zimesaidia kupunguza aina hii ya utumikishaji wa watoto walio katika umri wa kwenda shule...ni matumaini yangu kuwa vitoto hivi vitakapotoka katika shule hizo za kata havitakubali ajira za kinyonyaji kama hii na kama ikibidi basi ni kwa maslahi yenye manufaa kwa maisha yao ya baadae.

najua ntawaudhi wengi lakini huu ndiyo mtazamo wangu.

nawakilisha!
 
heshima mbele...<br />
<br />
fikiria mwajiri wako angetaka kukuajiri, uishi nyumbani kwake na kisha akulipe hizo elfu 30 ungejisikiaje?<br />
<br />
tufike pahala tujisikie aibu kutangaza vitu kama hivi......hata kama tunafanya basi na iwe kimya kimya..kutangaza ni sawa na kuona tunachokifanya ni sawa..<br />
<br />
tufike pahala tuone kuwa ajira ni msingi wa kumfanya mtu aweze kuishi maisha ya kujitegemea na kinyume chake ni unyonyaji.<br />
nadhani ni haki hasa kwamba hivi sasa imekuwa ni dhiki kubwa kupata mabeki tatu...pongezi kwa shule za kata...pamoja na mapungufu yake lakini zimesaidia kupunguza aina hii ya utumikishaji wa watoto walio katika umri wa kwenda shule...ni matumaini yangu kuwa vitoto hivi vitakapotoka katika shule hizo za kata havitakubali ajira za kinyonyaji kama hii na kama ikibidi basi ni kwa maslahi yenye manufaa kwa maisha yao ya baadae.<br />
<br />
najua ntawaudhi wengi lakini huu ndiyo mtazamo wangu.<br />
<br />
nawakilisha!
<br />
<br />
nimesema hivyo ili kuepuka maswali ya mshahara.
Mkuu hiyo ndio mishahara yao wengi wao tukubali tukatae.
Tatizo hapa kwenye keyboard watu tunajifanya wema sana tunajali maslahi ya wengine ila nimeuliza hapo chini, mfanyakazi wa kima cha chini anayelipwa laki 2 unategemea atamlipa hg sh ngapi?.
Anyways, mawazo yako yamesikika.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom