Msichana akikwambia ana mtu, mjali miezi 2 kisha kula kona ghafla...!

Wonderful strategy! Hapo mkuu kama ni wa kusogeza siku tu nenda nao wote, but kama unataka wa malengo nae, tuliza akili na moyo ndipo ufanye maamuzi.
Ila utoke hapo njia panda ulipo usiku mzito huu saa hii usije ambiwa unataka kuvunja Nazi!
hahaaaaa
anataka kuvunja Nazi tena
 
Hii ni njia bora kabisa ya kumpata mwanamke aliyekulingia na kudai anamsela mwingine tayari, proved nimewanasa mademu wawili kwa mpigo kwa njia hii.

Kwanza hapa nilipo ninayofuraha ya kumpata JULIE mtoto wa kichagga alinizingua na kunitendea ukatili sana, baada ya kuwa ananiambia habari za jamaa wake kila ninapofanya jitihada kumtongoza na kumteka akili..! Nilimwaga chozi mara nyingi ila JULIE hakunisikiliza huku akitilia mkazo kuwa angenikubali kama siyo huyo jamaa, eti huyo msela wake wametoka mbali, sikukata tamaa nilimjali kwa muda km miezi 2 simu kila lisaa nikimuulizia kama amekula kisha nikajiondoa bila yeye kutegemea.

Siku hazigandi kidume nikaamua kufake kuwa sina time naye tena, nikamtoa nishai JULIE kamind kinoma alafu nikamrudia kuomba msamaha akanisamehe huku akionya kamwe nisahau yeye kuwa mpenzi wangu, labda rafiki tuuh.

Kidume nikaua winga tena, huku nikimwacha bila yeye kujua, ila huwa naweza nikapita kazini kwake na kumsalimu kuwa ninashida na jirani yake kwenye ofisi ya jirani.

Siku zinakatika mtoto huko jamaa akimzingua kidogo demu anakasirika na kunikumbuka, tangu juzi nashangaa demu kanipigia simu yale niliyokuwa namcare kaanza kunilipa mara anigombeze eti sipendi kula, sasa usiku huu ROHO YANGU INAFURAHA SANA, jina limebadirika na kuwa MPENZI/MYDIA ONE, SWEET, sasa najiuliza sijamtongoza tena tangu animbie hawezi kuwa na mimi, na sasa naitwa hayo maneno matamu yote, ananidekea ajabu mara JOMONI BABY, hapa nashangaa ata sielewi huyu mbuzi kufia jikoni kwangu huku nina hangover atapona kweli???

Mtego umenasa wawili, MWINGINE demu mmoja alinizingua sana, kisa sina gari akasema yuko na msela wake wanapendana mno, nikaona isiwe taabu uzuri nina driving leseni nikachukua gari la my nephew RAV 4 matata akaanza kuonesha nia nikampa hadi lifti one day, ile ndiyo anaanza kuonja wema wangu nikapotea ghafla,tangu juzi simu zake ni kero baby umepotea jomoni, nikamwambia mmhh unamanisha kasema ndiyo nakupenda sana uwezi amini...! Sasa hapa kidume niko njia panda niende kwa DIANA au JULIE...! So confused aisei..
Neno dem limenikalia kushoto sana sijui kwann mnapenda kutumia DEM.
 
Hitimisho ndo umekosea.

Wanaume hatunaga muda wa kujiukiza Mara mbili kuhusu kula
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom