Mzalendowadamu
JF-Expert Member
- Jul 10, 2016
- 218
- 318
Sote tumeshuhudia namna msiba wa Ruge na sarakasi zake unavyo endelea. Binafsi naiona nguvu ya Media katika shughuli za msiba huu. Kumekuwa na hamasa kubwa ya watu juu ya msiba huu, hii naamini ni kutkana na msiba huu kufanya habari ya taifa kwa takriban wiki moja mpaka sasa. Kila kukicha kumekuwa na muitikio wa watu kutaka kujua kinacho jiri juu ya msiba huu. Kiukweli ukitazama yanayo jiri utaona namna Ruge (R.I.P) alivyokua anagusa maisha ya wengi na hakupenda kujionesha, hivyo Ruge amekua Star baada ya kufa.
Katima moja ya matangazo nimekuwa nikisikia wakisema na kufanananisha msiba huu kama wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Msiba wa Baba wa taifa ndio Msiba uliopata Kuwa mkubwa na wa Taifa letu. Kila msiba unao onekana kugusa jamii kubwa basi hulunganishwa na msiba wa Baba wa taifa.
Katika miaka ya hivi karibuni tunaweza kusema kumekuwa na misiba ya namna hii, miwili. Pamoja na huu wa Ruge, msiba mwingine ni wa Steven Kanumba.
Wakati wa Kifo cha Kanumba mwaka 2012 hakukua na jamii kubwa inayo tumia mitandao ya kijamii na simu janja kama sasa, pia Kanumba hakuwa na redio maalum ya kuubeba msiba wake. Asubuhi ya Tangazo la kifo Cha Kanumba kulishuhudiya mgagasiko wa mioyo ya watu wanaume kwa wanawake na kila rika, vilio na simanzi vilitawala kila kona ya nchi. Kanumba hakupokewa Airt port, Kanumba hakusafirishwa nje ya Dar.
Watu walipoteza fahamu kila kona ya nchi.Filamu za msiba Ts hirt, Kalenda na Majarida viliuzwa kama njugu.
Afrika Mashatiki , Kusini na Kati kote waliomboleza kifo cha Kanumba.
Huko Congo DR, Kanumba alijulikana kama Hans, kutokana na jina alilo tumia katika filamu flani, Dangerous Desire kama sijakosea. Mtu mmoja ananisimulia jinsi watu walivyo kuwa wana weka turubai majumbani mwao na kuita watu kukaa matanga ya Msiba wa Kanumba, watu walifanya maombi maalum ya Kumuombea. Naamini hayo yalifanya na nchi nyinginen pia ambao sio watanzania.
Kwa taswira ya Misiba hii, Je, ni kweli Msiba wa Ruge ni zaidi ya msiba wa Kanumba? Je ni Msiba upi unao fananishwa na Msiba wa Baba wa taifa?
Katima moja ya matangazo nimekuwa nikisikia wakisema na kufanananisha msiba huu kama wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Msiba wa Baba wa taifa ndio Msiba uliopata Kuwa mkubwa na wa Taifa letu. Kila msiba unao onekana kugusa jamii kubwa basi hulunganishwa na msiba wa Baba wa taifa.
Katika miaka ya hivi karibuni tunaweza kusema kumekuwa na misiba ya namna hii, miwili. Pamoja na huu wa Ruge, msiba mwingine ni wa Steven Kanumba.
Wakati wa Kifo cha Kanumba mwaka 2012 hakukua na jamii kubwa inayo tumia mitandao ya kijamii na simu janja kama sasa, pia Kanumba hakuwa na redio maalum ya kuubeba msiba wake. Asubuhi ya Tangazo la kifo Cha Kanumba kulishuhudiya mgagasiko wa mioyo ya watu wanaume kwa wanawake na kila rika, vilio na simanzi vilitawala kila kona ya nchi. Kanumba hakupokewa Airt port, Kanumba hakusafirishwa nje ya Dar.
Watu walipoteza fahamu kila kona ya nchi.Filamu za msiba Ts hirt, Kalenda na Majarida viliuzwa kama njugu.
Afrika Mashatiki , Kusini na Kati kote waliomboleza kifo cha Kanumba.
Huko Congo DR, Kanumba alijulikana kama Hans, kutokana na jina alilo tumia katika filamu flani, Dangerous Desire kama sijakosea. Mtu mmoja ananisimulia jinsi watu walivyo kuwa wana weka turubai majumbani mwao na kuita watu kukaa matanga ya Msiba wa Kanumba, watu walifanya maombi maalum ya Kumuombea. Naamini hayo yalifanya na nchi nyinginen pia ambao sio watanzania.
Kwa taswira ya Misiba hii, Je, ni kweli Msiba wa Ruge ni zaidi ya msiba wa Kanumba? Je ni Msiba upi unao fananishwa na Msiba wa Baba wa taifa?