Kiganyi
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 1,242
- 765
======================
Tokana na wingi wa picha Update zote zimewekwa mwanzo wa habari ili kuhakikisha ujumbe unasomeka kwa wote
wenye niya ya kutambua nini kinaendelea katika msiba wa Marehemu D. Mwambosi
========================
Tokana na wingi wa picha Update zote zimewekwa mwanzo wa habari ili kuhakikisha ujumbe unasomeka kwa wote
wenye niya ya kutambua nini kinaendelea katika msiba wa Marehemu D. Mwambosi
========================
Wakiongea kwenye mazishi ya mwandishi wa habari aliyeuwawa na polisi.kwa nyakati tofauti Mbunge wa Rungwe Profesa MARK MWANDOSYA na Katibu mkuu wa Chadema Dk W.P.SLAA wameahidi kuwasomesha watoto wa marehemu Daud Mwangosi.
Akianza Prof Mark Mwandosya amesema anajitolea kumsomesha mtoto wa kwanza alie kidato cha nne mpaka chuo kikuu.
Naye katibu mkuu wa Chadema amesema kwa kuanzia wameshatoa kiasi cha fedha na vile vile wameahidi kumsomesha mtoto wa pili ambaye sasa yuko darasa la saba.
Source.Eborn Fm
Wawakilishi Mbalimbali wakitoa salam za Pole kwa ndugu wa Marehemu
Mwakilishi wa Chanel Ten Hamis akitoa pole katika msiba huu muda huu
Mwenyekiti wa Mbeya Press Club akitoa pole zake kwa wafiwa
Mwanaharakati Francis Godwin akielezea Jinsi Mauti yalivyo mkuta Mwandishi wa Habari Daudi Mwangosi
Rais wa UTPC Kenny Simbaya ambaye pia ni kiongozi wa msafala wa kuleta Mwili wa Marehemu Daudi Mwangosi akiwa anatoa salam za Pole kwa wafiwa.
Dr Slaa akitoa pole kwa wafiwa wote Muda huu
Wakina mama wakiwa wenye majonzi makubwa sana na huzuni muda huu
Mke wa Marehemu Daudi Mwangosi akilia kwa Uchungu Muda huu
Maelfu ya watu wakiongezeka kuja katika Mazishi ya mwandishi wa habari wa Chanel 10 Daudi Mwangosi Muda huu
Mheshimiwa Mark Mwandosya ambaye ni Waziri ofisi ya Rais na pia Mbunge wa Rungwe Mashariki akitoa salam kwa Niaba ya Serikali
Watu wakiwa wengi na wenye utulivu wakisikiliaza watu mbalimbali wakitoa salam zao kwa ndugu wa Marehemu
Mjane Mke wa Marehemu Daudi Mwangosi aliye jishika, akiwa na uchungu muda huu
Ibada ikiwa inakaribia kuanza
Ibada ya mazishi ndio imeanza muda huu
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa wenye majonzi Makubwa
Waandishi wa Habari wakiwa katika msiba wa kwanza kutoka kulia ni Ndugu Joseph Mwaisango ambaye ni mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Blog, Rais wa UTPC Keny Simabaya, pamoja na Felix Mwakyembe .
Endelea kufuatilia Moja kwa moja hapa
PICHA ZOTE NA MBEYA YETU BLOG
Updates; Forever Bold, RIP D. M, Tuonane Mtoni Mkuu!!
Waandishi wa Habari wakiwa wamebeba Mwili wa Marehemu kuelekea Makabirini
Wakiwa wanafanya ibada ya Mwisho kabla ya kuanza maziko
Hapa wakiwa wanashusha mwili wa marehemu katika Nyumba yake ya milele
Mwili wa Marehemu Daudi Mwangosi ukiwa Tayari katika Kaburi
Shughuri za kuzika zimeanza
Mazishi yanaendelea
Mke wa Marehemu Daudi Mwangosi akiweka Shada la Mauwa kwa machungu
Mke wa Daudi Mwangosi akiwa analia kwa uchungu katika Kaburi la Marehemu Mumewe
Watoto wa Marehemu wakiwawanaweka mashada ya maua sasa
Ni ngumu sana Kuamini kwa mke wa Marehemu lakini hali ndivyo ilivyo kuwa akiwa na huzuni kubwa
Dr Slaa akiweka Shada la Mauwa
Dr Slaa Baada ya kumaliza kutoa heshima za mwisho
Mh. Mark Mwandosya akiweka Taji la maua pamoja na mke wake
Rais wa UTPC akiweka shada la Maua
Ndugu wa Marehemu akiweka shada la Maua
Mwenyekiti wa Mbeya Press Club akiweka shada la maua
Mwandishi Mkuu wa Mbeya yetu, Ndugu Joseph Mwaisango akiwa anatoa heshima zake za Mwisho katiaka Kaburi
Wananchi wakiwa wanarejea baada ya mazishi
Waandishi wa Habari wakichukua Tukio Live `
Na huu Ndio Mwisho wa tukio zima la Mazishi ya Ndugu yetu, Mwanaharakati, Mpiganaji Daudi Mwangosi aliyekuwa Mwandishi wa Chanel 10.