Mshukiwa aliyefungwa miaka 43 gerezani kimakosa

Bravo snr

Senior Member
Aug 16, 2020
182
472
Mshukiwa aliyefungwa miaka 43 gerezani kimakosa
Kevin Strickland, ambaye alifungwa gerezani kwa miaka 43 kimakosa kwa madaia ya hatia ya mauaji matatu katika jiji la Kansas nchini Marekani (USA), ameachiliwa huru.

Kulingana na ripoti ya Sputnik, kesi hiyo ilianzishwa baada ya mauaji yaliyofanywa mnamo Aprili 1978.

Kevin Strickland mwenye umri wa miaka 61, aliachiliwa huru wakati wa kusikilizwa kwa kesi ya kwanza mnamo 1979. Lakini mahakama ilimpata Strickland na hatia ya mauaji ya shahada ya pili kwa mara ya pili baada ya miezi 2.

Ilielezwa katika ripoti ya gazeti la ndani mnamo Aprili 1978 kwamba watu 2 waliokubali uhalifu wa mauaji walisema kwamba Strickland hakuwa pamoja nao wakati huo.

Kufuatia ripoti hiyo, Ofisi ya Wakili wa Kaunti ya Jackson ilipitia faili hiyo Novemba iliyopita.

Kama matokeo ya uchunguzi wa upande wa mashtaka, iliamuliwa siku ya Jumatatu kwamba Strickland aliachiliwa huru baada ya kutumikia kifungo cha gerezani bila hatia.

Kevin Strickland, ambaye amekuwa gerezani kwa miaka 43, alitangaza kwamba aliachiliwa baada ya ukaguzi wa matibabu.
 
Ningekuwa mimi nisingekubali kutoka..ningewaambia waniache tu nifie humo humo gerezani.sasa miaka 43 yote umeishi jela,leo wanakutoa uende wapi?
 
Back
Top Bottom