Mshkaji kaja kukaa kwangu akidai ni kwa muda ila sasa naona hana mpango wa kuondoka

Mkuu haujui kesho yako itakuaje..
Kisa moto wa Morogoro..
Abiria wa boda boda alikwenda kumuokoa dereva ikashindikana. Alipokwenda kutafuta kisu cha kukata mkanda ulimbana dereva ghafla moto ukawaka..
Wakafariki wote.. Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi.. Amiin
 
Hivi mtu mzima kweli unaingia mjini huna mipango yoyote unaenda kukaa tu unajielewa kweli? huy jamaa yako anapenda vya dezo mtelemk tu kama hataki kazi ni vizuri arudi kwao kuna haja gani kuja kumbana mtu wakat unakwenu mtu kama huyo ata ukimtafutia mishe atafanya wiki ataacha watu kama hao wanapenda kukaa tu vijiweni
Wewe pika misosi mibaya mibaya kila siku ugali na mboga majani kila siku we unakula ulipotoka vizuri unamwambia hali mbaya mwezi tu huyo mtu anarudi kwao
 
Kwani ukimsaidia mshkaji utapungukiwa nini? Wewe saidia tu hiyo ni akiba yako ya baadae kama sadaka vile.
 
Sidhani kama kuna mahali kaandika jamaa hataki kazi na mvivu, sema inaonesha jamaa tu hajapata channel bado, kama ni mvivu na hataki kazi huyo wa kumuondoa kama ni bado mipango yake haijajiset ni kumvumilia tu.
Hivi mtu mzima kweli unaingia mjini huna mipango yoyote unaenda kukaa tu unajielewa kweli? huy jamaa yako anapenda vya dezo mtelemk tu kama hataki kazi ni vizuri arudi kwao kuna haja gani kuja kumbana mtu wakat unakwenu mtu kama huyo ata ukimtafutia mishe atafanya wiki ataacha watu kama hao wanapenda kukaa tu vijiweni
Wewe pika misosi mibaya mibaya kila siku ugali na mboga majani kila siku we unakula ulipotoka vizuri unamwambia hali mbaya mwezi tu huyo mtu anarudi kwao
 
Jina lako emmanuel maana yake Mungu pamoja nasi sasa wewe mbona unataka kuwa shetani pamoja nawe?????

Kwani wewe kwenye hicho chumba umeoteshwa mizizi.???
Kama kweli una utu na upendo wa kusadidia tafuta chumba kingine wekeni godoro mshkaji wako ahame au wewe uhame..

Cha kwanza kabusa msaidie mshkaji wako kupata mishe ya kufanya..mkiweka malengo na wewe hpo kwenye system miezi mitano mshkaji wako atakua na getto lake..
Msaidie tu kwa kuwa huwezi jua wewe atakuja kukusaidia nani,
Tenda wema nenda zako msaada hauna risiti baba
Hichi ndio kinatufanya watanzania tuzidi kuwa masikini
 
kitu nilivchojifunza kwenye maisha ni what goes around comes around..ukimfanyia mtu ubaya tegemea kuna siku utahitaji msaada toka kwake...hiyo ndo moja ya kanuni ya maisha ili ujifunze.

Wewe msaidie tu!! kwa ushaur wangu
 
Kuna watu huwa wanapenda kitonga. Unapokaa kwa mtu mwambie utakuwepo kwa muda gani na kukitokea dharula mwambie nimeshindwa mwezi huu kwa sababu moja mbili. Na vile vile mtu aone jitihada unazofanya ili ujikwamue.

Huyu jamaa yetu kasema kamaliza chuo majuzi, ina maana hata yeye mambo hayajakaa mukide, hatakiwi kubebeshwa mzigo wa ziada.

Wazungu watoto wakifikisha miaka 18 wanasepa home, na even at 16 wanaanza kufanya kazi, inajenga culture ya kuwajibika. Huku kwetu tunabembelezana sana.
Sidhani kama kuna mahali kaandika jamaa hataki kazi na mvivu, sema inaonesha jamaa tu hajapata channel bado, kama ni mvivu na hataki kazi huyo wa kumuondoa kama ni bado mipango yake haijajiset ni kumvumilia tu.
 
I know someone with the same story, Huyo jamaa hata hakua na urafiki wala undugu (Afadhali ya wewe), Lakini alifanya wema akamvumilia yule jamaa kwa miezi minne, Mungu alivyo wa ajabu jamaa alipata shavu nene balaa, Ndo anamsaidia yule mwenyeji wake sasahivi na kasaidia tena ndugu zake kadhaa kupata kazi kwenye kampuni alilopo.


Be Kind, Be Nice, Haikugharimu kitu chochote.
 
I know someone with the same story, Huyo jamaa hata hakua na urafiki wala undugu (Afadhali ya wewe), Lakini alifanya wema akamvumilia yule jamaa kwa miezi minne, Mungu alivyo wa ajabu jamaa alipata shavu nene balaa, Ndo anamsaidia yule mwenyeji wake sasahivi na kasaidia tena ndugu zake kadhaa kupata kazi kwenye kampuni alilopo.


Be Kind, Be Nice, Haikugharimu kitu chochote.
Na mimi nimemshauri hivo asiangalie upande wa kubanwa tu..haya ni maisha na hayana formula..Maisha ni mzunguko..!!
 
Usikilize moyo wako, ninafahamu na nimeona mifano mingi unaishi na mtu anakuja kukugeuka au kuwa baraka kwako, kwa upande wangu mimi ningemwambia jamaa atafute utaratibu ahame maana hakuja kwa lengo hilo, ama hata kama alikuwa ana hilo lengo alimua makusudi kukuficha na kutokukuambia mapema ili ukubaliane nalo ama ukatae, ndani ya fikra zake naona kabisa hamna ushkaji ulionao kwenye fikra na moyo wako, na ni mbinafsi ...SIKILIZA MOYO WAKO
 
NISHAURI
NImwambie mzee baba ajisogeze niendelee na mishe zangu kwa uhuru au nimpotezee apambane na yeye hadi atakapo kuwa sawa?

Sielewi wadau nafanye nn coz hata muda atakaosepa sijui ni lini na mimi ndio sipend kabisa kubanwa

Nanitamwambiaje asepe ?
NAWASILISHA

Navojua mimi unakua zaidi kimaisha unapopata changamoto (challenges). Badala ya kuavoid hiyo changamoto hebu itatue. Mtihani haijengi wanafunzi wazuri kama itaondoa maswali magumu ili wanafunzi wafaulu.

Nyie ni vijana, pangeni shughuli mfanye ili kurahisisha maisha yenu pamoja. Use each other. Vijana wa kitanzania hatufanikiwi sana kwa sababu tunapambana wenyewe mwenyewe, ni wachoyo na wabinafsi ndo maana tunahujumiana. Ukimasaidia sasa hivi ambapo hana kitu huezi jua mbeleni atakua nani (Sijui ni kwanini cku hizi tunaona karibu tu! Yani tunawaza ugali wa leo tu)
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom