Mshituko: Hotuba za hayati Magufuli zinaweza kuja kutumika kuiondoa CCM madarakani

Kinuju

JF-Expert Member
Mar 20, 2021
2,390
5,310
Mshituko mkubwa nimeupata baada ya kugundua kuwa watanzania wengi wamezitunza video mbalimbali za hayati Magufuli kama reference na kipimo cha kupima utendaji wa serikali iliyopo madarakani na serikali zitazokuja.

Kiongozi yoyote sasa hivi akitoa visingizio kwamba jambo fulani haliwezekani kufanyika watanzania wanamjibu kwa kumuwekea video za Magufuli na kumuuliza mbona kipindi cha hayati Magufuli hilo jambo liliwezekana?

Alianza waziri wa nishati January Makamba kuwadanganya watanzania kuwa mgao wa umeme unaotikisa nchi kwa sasa unatokana na awamu ya tano kuzuia maintanance baada ya hayati Magufuli kusema hataki kusikia mgao wa umeme na hivyo vifaa kupata uchakavu uliosababishwa na kuwaka mfululizo kwa miaka 5.

Kabla ya uongo wake haujakauka watanzania walimshushia video za Magufuli akianika uozo na mbinu chafu za watendaji wa Tanesco kuhongwa pesa na kufungulia maji ili baadhi ya wafanyabuashara wasio waaminifu wauze jenerata zao!

Ghafla TANESCO wsmebadilika tena na kusesema mgao wa umeme unasababishwa na kupungua kwa maji kwenye mabwawa na siyo regular maintanance iliyosemwa na Makamba.

Kwenye mkumbo wa kusema uongo hadharani ameingia pia waziri wa uwekezaji Godfrey Mwambe baada ya kuwadanganya watanzania kuwa hakuna mkataba wowote uliowahi kusainiwa kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na akaonyesha kushangaa hayati Magufuli aliyatoa wapi hayo maneno!

Mwambe bila kujali onyo la wahenga linalotaka kuogopa Mungu na technologia akasahau kuwa kuna video ikionyesha rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete akiweka jiwe la msingi ujenzi wa bandari ya Bagamoyo!

Je, jiwe la msingi huwa linawekwa bila mkataba wowote? Hata mtaani mama ntilie, bodaboda, wachimbaji wadogo machinga mara kwa mara wamekuwa wakirejea hotuba za Magufuli zilizokuwa zinasisitiza kuwa sera za CCM lazima ziegemee kuwalinda wanyonge ili nao watajirike na siyo kuwafukuza na kuwanyanyasa.

Ninavyoona mbele ya safari kuna hatari ya hotuba mbalimbali za hayati rais Magufuli kutumiwa na wananchi kuibana serikali kutakakosababisha CCM kuondolewa madarakani.

Kwenye kizazi hiki CCM wana njia moja tu ya kupona nayo ni kufanya kazi zaidi kuliko hayati Magufuli na siyo kufanya kazi chini ya kiwango huku wakitoa visingizio mbalimbali.
 
Wako watanzania ni waelewa sana.

Watanzania hao ni waelewa wa nchi yetu ilikotoka ,ilipo na huko inakotaka kuelekea.....katika kundi hili hutakuta watu wa MIHEMHO....hapa watakuambia wanamsikiliza sana NYERERE....wanamsilikiza sana MWINYI ,MKAPA ,KIKWETE NA MAGUFULI.

Liko kundi la watu wanaojua kuwa nchi ni MIUNDOMBINU TU yaani MIUNDOMBINU ni kila kitu, hawa wengi wao hawana uelewa mpana wa MAMBO MTAMBUKA YA NCHI.

Ninadiriki kusema hawa HAWATAKI KUJISHUGHULISHA KUJUA malengo mengine ya SERIKALI kama yafutavyo:-

1)Kukisimamia kilimo ipasavyo.
2)Kuongeza mishahara watumishi na kuwapandisha madaraja.
3)Kuajiri vijana wanaomaliza vyuo kila uchao.
4)Kuweka sera nzuri na zenye kutabirika kuvutia wawekezaji.
5)Kuweka sera nzuri ili sekta binafsi izidi kuchanua.

Watanzania waelewa wanaendelea kuwathamini viongozi wao wote wa awamu 5 zilizopita kwani kila mmoja ametoa mchango adhimu wa kutufikisha hapa tulipo💪

#SIEMPRE JMT🙏
#NCHI KWANZA🙏
#KAZI INAENDELEA KWA KASI &WELEDI ZAIDI 💪😍👊
 
Hakuna crane ya kunyanyua milango mizito ya 26tani lazima zitoke nje January makamba
Bado unang'ang'ana tu na ubishi bwasheee?!!🤣

Iko hivi.

CRANE alizozungumzia mh.Makamba ni zile IMMOVABLE(za kupachikwa palepale).......nazo ndizo zilizo njiani kuletwa.....yeye kama Waziri mwenye dhamana hilo alilitolea tu ufafanuzi..

SIEMPRE JMT
 
Ninavyoona mbele ya safari kuna hatari ya hotuba mbalimbali za hayati rais Magufuli kutumiwa na wananchi kuibana serikali kutakakosababisha CCM kuondolewa madarakani.
Ni kweli ccm wanatakiwa kufanya kazi sana, kwa kiwango, au hata kumzidi hayati Magufuli, kama wanataka waendelee kuonekana relevant kwa wananchi. Kumtumia Magufuli as a scapegoat ya utendaji mbovu haitawasaidia.

Hilo la kuondolewa madarakani kwa sasa ni gumu kwa sababu hakuna chama mbadala. Ingekuwa chadema bado ina nguvu kama enzi zile za Dr Slaa, ccm wangepata tabu sana

Kwa sasa hivi labda wananchi waamue kuchagua chochote tu kisichokuwa CCM bila kujali athari zake ndo hilo litawezekana.
 
Njia pekee ya kujua kama kuna chama mbadala ni kupitia tume huru ya uchaguzi tu.

Zaidi ya hapo ni kupiga ramli.

Wenzetu waliostaaribika zaidi wana hadi kura za maoni za kisayansi ambazo huwa hazitofautiani sana na uchaguzi halisi lakini hawazitumii hizo kama mbadala wa sanduku huru la kura la raia wote.

Tume hata ikiwa tofauti na ya sasa, hakuna chama mbadala bwashee!
 
Kupewa nchi kivipi?

Chama kimoja kikishinda Urais, kingine tofauti kikishinda ubunge na kingine tofauti kabisa kikishinda Zanzibar ni kipi kitakuwa kimepewa nchi kati ya hivyo vitatu?
Chama gani kitapewa nchi?
 
Back
Top Bottom