Mshindi wa kura za maoni CCM akosa dhamana

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Mshindi wa kwanza wa kura za maoni CCM katika jimbo la Singida Kaskazini (kabla ya mchakato kufutwa), Haider Gulamali ameshindwa kupata dhamana kufuatia hakimu anayesimamia kesi yake kupata dharura na hivyo kushindwa kufika mahakamani.

DRBLlMhX0AAvx_r.jpg
 
Mshindi wa kwanza wa kura za maoni CCM katika jimbo la Singida Kaskazini (kabla ya mchakato kufutwa), Haider Gulamali ameshindwa kupata dhamana kufuatia hakimu anayesimamia kesi yake kupata dharura na hivyo kushindwa kufika mahakamani.

View attachment 651092
Huyu nae alishindwa kusoma maandiko ukutani? Sio wakati wa Kikwete huu mwenye fedha ndio aliyekuwa na nguvu ya kununua uongozi!
 
Huyu nae alishindwa kusoma maandiko ukutani? Sio wakati wa Kikwete huu mwenye fedha ndio aliyekuwa na nguvu ya kununua uongozi!
Tatizo sio zama za kikwete tatizo gulamali si upande wa muheshimiwa sana , mbona kama rushwa ipo tuu na kina mnyeti wana peta nayo na takukuru wanawatizama tu na ushahid wanao? Inshu sio rushwa inshu ni bwana yule hayupo upande wa huyu jamaa
 
Tatizo sio zama za kikwete tatizo gulamali si upande wa muheshimiwa sana , mbona kama rushwa ipo tuu na kina mnyeti wana peta nayo na takukuru wanawatizama tu na ushahid wanao? Inshu sio rushwa inshu ni bwana yule hayupo upande wa huyu jamaa
Wengi hawalielewi kabisa hili ulilolisema..
Wanafikiria jamaa yupo serious na mapambano ya Rushwa..
Hakuna kitu kama hicho..
Watu wake kibao wanatumia rushwa na wanapeta bila kuguswa..
Asante sana kwa maelezo yako.
 

Salary Slip najua kabisa bila shaka kuwa huu mchezo unachagizwa na fedha! Sio kama sijui! Na nikuambie kuwa in a long run utakuja ku-backlfire vibaya sana kwa CCM. Hii ni kwasababu wote wanaokimbilia huko wanaongozwa na matumbo. Sasa mkusanyiko wa watu wenye matumbo na tamaa sehemu moja ni hatari mno. Ila bado tu haindoi ukweli kuwa Chadema ndio wanaojikaanga kwa mafuta yao. Walipotumia watu (wenye malengo yao) kuhama CCM kwenye Chadema kama silaha ya kuiadhiri na kuinyanyasa CCM nilijua lazima CCM kwa kutumia organs zake ie fedha na utawala watafanya lolote ili waonekane wako mbele. Jamni hata Wema na Nyalandu kweli wanapokewa Chadema kama mashujaa?
 
Tatizo sio zama za kikwete tatizo gulamali si upande wa muheshimiwa sana , mbona kama rushwa ipo tuu na kina mnyeti wana peta nayo na takukuru wanawatizama tu na ushahid wanao? Inshu sio rushwa inshu ni bwana yule hayupo upande wa huyu jamaa
Mkuu kwanza tusahihishane. Neno sahihi ni ishu (ambalo limetokana na neno na kiingereza issue) na sio ''inshu''. Sasa Nikuulize wewe na Chadema. Hivi kweli kweli mlitegemea huyo Mnyeti angekamatwa kwa kuhonga watu waingie CCM? Kama mlitegemea hilo poleni sana!
 
Huyo siyo mteule wa Rais, mbona Mnyeti, Bashite wanatoa rushwa wazi wazu.
Ndio nimewauliza na wenzako. Hivi mnasubiri kina Mnyeti wakamatwe? Basi kama mnasubiri hicho naona upinzani hauna clue ufanye nini! Mkuu ngoja nikumbie. Tangu chaguzi za nyuma watu wanaoona mbali wamekuwa wanawaasa sana vyama vya upinzani kuwa bila kupigania mkawa na uwanja sawa wa uchaguzi hamtafanya lolote. Lakini wamekuwa wanadharau. Matokeo yake CCM imeshakuwa na jeuri ya kufanya lolote kwani ina uhakika kuwa itatumia nguvu au hoja kushinda! Unafikiri kungekuwa na uwanja sawa wa uchaguzi wangethubutu kununua wabunge na madiwani wa upinzania? Thubutu! Wangejua wakinunua hawana uhakika wa kushinda uchaguzi wa marudio hivyo wasingethubutu!
 
Ndio nimewauliza na wenzako. Hivi mnasubiri kina Mnyeti wakamatwe? Basi kama mnasubiri hicho naona upinzani hauna clue ufanye nini! Mkuu ngoja nikumbie. Tangu chaguzi za nyuma watu wanaoona mbali wamekuwa wanawaasa sana vyama vya upinzani kuwa bila kupigania mkawa na uwanja sawa wa uchaguzi hamtafanya lolote. Lakini wamekuwa wanadharau. Matokeo yake CCM imeshakuwa na jeuri ya kufanya lolote kwani ina uhakika kuwa itatumia nguvu au hoja kushinda! Unafikiri kungekuwa na uwanja sawa wa uchaguzi wangethubutu kununua wabunge na madiwani wa upinzania? Thubutu! Wangejua wakinunua hawana uhakika wa kushinda uchaguzi wa marudio hivyo wasingethubutu!
Katika hali kama hii unafanyaje? Mbele ya risasi, kuuawa, sandarus baharini, kufungwa, mabomu, kuumizwa, ukatili wa dola etc? Unafanyaje. Nakumbuka Amin alipingwa sana mwanzoni, akaamua kuua indiscriminately kama ilivyo hapa sasa. Unafanyaje?
uwanja sawa utaudai kwa mtawala huyu? Uganda alikuwa amebaki Askofu Mkuu wa Anglican Janan Luwum, naye akamuua kwa mkono wake! Unafanyaje?
 
Katika hali kama hii unafanyaje? Mbele ya risasi, kuuawa, sandarus baharini, kufungwa, mabomu, kuumizwa, ukatili wa dola etc? Unafanyaje. Nakumbuka Amin alipingwa sana mwanzoni, akaamua kuua indiscriminately kama ilivyo hapa sasa. Unafanyaje?
uwanja sawa utaudai kwa mtawala huyu? Uganda alikuwa amebaki Askofu Mkuu wa Anglican Janan Luwum, naye akamuua kwa mkono wake! Unafanyaje?
Hayo ya uwanja sawa hayajanza leo. Yalisemwa kitambo sana. Nadhani watu wamekumbuka shuka asubuhi! Hata hivyo nikukumbushe haki hakiletwi kwenye kisahani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom