Mshahara wa Rais wa nini sasa iwapo hadi nguo na mataulo vinanunuliwa na Ikulu?!

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Majibu ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Salva Rweyemamu, dhidi ya tuhuma zilizotolewa na WikiLeaks iliyoandika mambo ya kashfa dhidi ya Mh. Rais wetu yameniacha nikijiuliza maswali mengine mbali ya hizo tuhuma. Katika majibu hayo, Salva ametaja kwamba mavazi ya Rais ni jukumu la serikali. (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...nies-president-bribe-claims-in-u-s-cable.html)

Ninachojiuliza, pamoja na usiri mkubwa unaogubika kiwango cha mshahara wa Rais wetu ni nini haswa matumizi ya mshahara wake wowote ule anaopata, iwe ni shs. laki nane, millioni 40 au milioni 600 kwa mwezi?? Kwani kila kitu katika maisha yake kinaonekana kuwa covered na fungu fulani kutoka katika bajeti ya Ikulu au nyingineyo.

Ulinzi, chakula, safari, mikutano ya faragha, sherehe, mavazi, malazi, matibabu, n.k., n.k... Basi, na kama binadamu na Mtanzania mwenyekustahili kipato kwa kazi yake kama walivyo wengine, ni nini matumizi ya mshahara huo ambao hata kodi haukatwi??!!!
 
Hivi mshahara wa raisi wa Tanzania hakuna kabisa anayeujua?

Na hivi kwanza mwajiri wa raisi ni nani? Manake nijuavyo mimi mwajiri wa mtu yeyote yule lazima ajue mshahara wa huyo mwajiriwa wake.

Sasa mimi ningependa kumjua huyo mwajiri wa raisi wa jamhuri yetu ili nimuulize yeye moja kwa moja kiasi cha mshahara anachomlipa na mafao mengine yanayoambatana na hiyo kazi ya uraisi.

Humu kuna wanachama 47,000 na kitu (yeah..hii idadi ni pamoja na sisi wenye majina mengi). Yaani katika hawa wote hakuna ajuaye kiasi cha mshahara wa raisi?
 
Ni nini limit ya bajeti ya mavazi ya Rais?

Hivi akiamua kuvaa suti za Savile Row na Armani tu taifa litatakiwa kugharimia pia? Mwisho wetu wa kugharamia ni kiasi gani?

Wananchi tunahaki ya kujuulishwa maswala haya.
 
Ni nini limit ya bajeti ya mavazi ya Rais?

Hivi akiamua kuvaa suti za Savile Row na Armani tu taifa litatakiwa kugharimia pia? Mwisho wetu wa kugharamia ni kiasi gani?

Wananchi tunahaki ya kujuulishwa maswala haya.

Wewe unaona wananchi tuna haki pia ya kujua raisi wetu analipwa mshahara kiasi gani kwa mwezi?
 
Wewe unaona wananchi tuna haki pia ya kujua raisi wetu analipwa mshahara kiasi gani kwa mwezi?
Nyani,
Only in Tanzania. Mshahara wa rais ni siri kwa sababu rais kajiajiri mwenyewe. Enzi za Mwalimu Nyerere tulijua alikuwa analipwa kiasi gani kwa mwezi. Enzi za mafisadi wanajidai eti ni siri ya serikali.
 
Nyani,
Only in Tanzania. Mshahara wa rais ni siri kwa sababu rais kajiajiri mwenyewe. Enzi za Mwalimu Nyerere tulijua alikuwa analipwa kiasi gani kwa mwezi. Enzi za mafisadi wanajidai eti ni siri ya serikali.

Kajiajirije mwenyewe wakati wananchi kimsingi ndiyo waajiri wake kwa sababu wanamchagua (ukiachilia mbali irregularities za chaguzi zetu)?

Yaani mambo mengine yanayoendelea Tanzania kweli ni only in Tanzania!!

Halafu watu wengi wala hawako concerned kabisa na jinsi hela zao zinavyotumika kumlipa mshahara raisi wetu!! SMH!!!

Au mshahara wake unalipwa kutoka kwenye fungu la wafadhili na wahisani?
 
Wewe unaona wananchi tuna haki pia ya kujua raisi wetu analipwa mshahara kiasi gani kwa mwezi?

That goes without saying.

Ninachotaka kushadidia ni kuwa sio mshahara tu tunaotakiwa kuelezwa, bali hata hayo marupurupu in details.

Bajeti ya chakula mwisho kiasi gani? Bajeti ya mavazi, mwisho kiasi gani?, Bajeti ya mawasiliano binafsi mwisho kiasi gani?

Na ni haki ya mwananchi kuambiwa matumizi kamili kwa kila mwaka ya rais wake.
 
Hivi mshahara wa raisi wa Tanzania hakuna kabisa anayeujua?<br />
<br />
Na hivi kwanza mwajiri wa raisi ni nani? Manake nijuavyo mimi mwajiri wa mtu yeyote yule lazima ajue mshahara wa huyo mwajiriwa wake. <br />
<br />
Sasa mimi ningependa kumjua huyo mwajiri wa raisi wa jamhuri yetu ili nimuulize yeye moja kwa moja kiasi cha mshahara anachomlipa na mafao mengine yanayoambatana na hiyo kazi ya uraisi.<br />
<br />
Humu kuna wanachama 47,000 na kitu (yeah..hii idadi ni pamoja na sisi wenye majina mengi). Yaani katika hawa wote hakuna ajuaye kiasi cha mshahara wa raisi?
<br />
<br />
Kwaani rais anaajiriwa?, hakuna chuo cha kusomea urais, rais huchaguliwa tu tena na watu wote, i.e wasomi kwa wajinga, waumini kwa makafiri, walokole kwa mapagani, pia mafisadi na mabwia SEMBE.
 
Ni nini limit ya bajeti ya mavazi ya Rais?

Hivi akiamua kuvaa suti za Savile Row na Armani tu taifa litatakiwa kugharimia pia? Mwisho wetu wa kugharamia ni kiasi gani?

Wananchi tunahaki ya kujuulishwa maswala haya.

This is another thing, ndiyo, Rais anapendeza kwa mwonekano, but at what cost to the Nation kama si ya mshahara wake?? Kwanini PM na mawaziri wengine wasinunuliwe?? Kwanini wanafunzi wenye wazazi wasiojiweza hawanunuliwi?? Ila Rais mwenye kila kitu, madaraka ya kunyonga included, ndiye anayenunuliwa nguo kwa bajeti isiyojulikana mpaka wake...
 
<br />
<br />
Kwaani rais anaajiriwa?, hakuna chuo cha kusomea urais, rais huchaguliwa tu tena na watu wote, i.e wasomi kwa wajinga, waumini kwa makafiri, walokole kwa mapagani, pia mafisadi na mabwia SEMBE.

Sasa kazi anayofanya ni ya kujitolea?
 
This is another thing, ndiyo, Rais anapendeza kwa mwonekano, but at what cost to the Nation kama si ya mshahara wake?? Kwanini PM na mawaziri wengine wasinunuliwe?? Kwanini wanafunzi wenye wazazi wasiojiweza hawanunuliwi?? Ila Rais mwenye kila kitu, madaraka ya kunyonga included, ndiye anayenunuliwa nguo kwa bajeti isiyojulikana mpaka wake...

Kaka hapo kwa PM una uhakika kweli? Manake isije ikawa tu bado haijabumbuluka na yeye....
 
Inabidi mbunge mmojawapo aulize hili Swali katika moja ya vikao vijavyo. Nani mnafikiri aulize hili Swali. BTM, mishahara ya mawaziri tunaijua?
 
As far as I know PM na Mawaziri wengine wakienda safari nje ya nchi wanapewa pesa za mavazi.

(Ikimaanisha zile nguo zao wanazovaa kila siku Tanzania huko nje ya nchi hazifai?)
 
Hili taifa hili, daah...!! Kama ni nywele basi ni zile za kichaa!!! Maana huwezi kutambua kama amesuka, ana rasta au ana kipilipili... zinakuwa zimejisokota tu na kuwa mafungu-mafungu au fungu moja!!! Kuweza kutambua ni aina gani ya nywele jamaa anazo ni lazima kukata kipala kwanza, else huwezi kuzitibu chawa wala kuzichana!!!! :sad:
 
We definitely need more transparency in the way our government operates.

Utaambiwa mshahara wa rais hautajwi kwa sababu unahusiana na usalama wa taifa. How?

Daftari la wageni wa Kikwete ikulu haliwekwi wazi pia kutokana na "usalama wa taifa"

Mapato ya rais na kodi aliyolipa haijuulikani.

Wabunge na Mawaziri nao malipo yao hayako wazi
 
Utaambiwa mshahara wa rais hautajwi kwa sababu unahusiana na usalama wa taifa. How? <br />
<br />
Daftari la wageni wa Kikwete ikulu haliwekwi wazi pia kutokana na &quot;usalama wa taifa&quot;<br />
<br />
Mapato ya rais na kodi aliyolipa haijuulikani. <br />
<br />
Wabunge na Mawaziri nao malipo yao hayako wazi
<br />
<br />

Enyi waTz, Msiwe
na tabia ya kupenda fedha;
muwe radhi na vitu mlivyo
navyo; kwa kuwa yeye
mwenyewe amesema,
sitakupungukia kamwe, wala
sitakuacha.
(Soma Waebrania 13:5)
 
Kwa nchi zilizopiga maendeleo kila kitu kiko wazi, lakini nchi yetu kwa hii stahili yao ukiuliza utaambiwa unagusa sehemu nyeti. Maendeleo ni ndoto kwa kuwa matumizi ya msingi hayabajetiwi.

Pale bungeni wanaleta zipite tu kwa kuwa ni utaratibu, lakini haki na wajibu wa kuhoji fungu hili lipunguzwe au litolewe ni marufuku, utaambiwa unaleta uchochezi.
Kumbuka mheshimiwa John Mnyika alivyohoji kuhusu fungu la fedha kwa usalama wa taifa? Alivyoshambuliwa na wabunge wa magamba.
Tatizo watu wa zamani wakisikia usalama wa taifa matumbo moto, hakuna lolote wapo kichama zaidi na si ki nchi.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom