Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
Majibu ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Salva Rweyemamu, dhidi ya tuhuma zilizotolewa na WikiLeaks iliyoandika mambo ya kashfa dhidi ya Mh. Rais wetu yameniacha nikijiuliza maswali mengine mbali ya hizo tuhuma. Katika majibu hayo, Salva ametaja kwamba mavazi ya Rais ni jukumu la serikali. (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...nies-president-bribe-claims-in-u-s-cable.html)
Ninachojiuliza, pamoja na usiri mkubwa unaogubika kiwango cha mshahara wa Rais wetu ni nini haswa matumizi ya mshahara wake wowote ule anaopata, iwe ni shs. laki nane, millioni 40 au milioni 600 kwa mwezi?? Kwani kila kitu katika maisha yake kinaonekana kuwa covered na fungu fulani kutoka katika bajeti ya Ikulu au nyingineyo.
Ulinzi, chakula, safari, mikutano ya faragha, sherehe, mavazi, malazi, matibabu, n.k., n.k... Basi, na kama binadamu na Mtanzania mwenyekustahili kipato kwa kazi yake kama walivyo wengine, ni nini matumizi ya mshahara huo ambao hata kodi haukatwi??!!!
Ninachojiuliza, pamoja na usiri mkubwa unaogubika kiwango cha mshahara wa Rais wetu ni nini haswa matumizi ya mshahara wake wowote ule anaopata, iwe ni shs. laki nane, millioni 40 au milioni 600 kwa mwezi?? Kwani kila kitu katika maisha yake kinaonekana kuwa covered na fungu fulani kutoka katika bajeti ya Ikulu au nyingineyo.
Ulinzi, chakula, safari, mikutano ya faragha, sherehe, mavazi, malazi, matibabu, n.k., n.k... Basi, na kama binadamu na Mtanzania mwenyekustahili kipato kwa kazi yake kama walivyo wengine, ni nini matumizi ya mshahara huo ambao hata kodi haukatwi??!!!