Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,792
- 71,206
Dola hii ya awamu ya tano chini ya Magufuli imedhihirisha usemi wake kuwa Msema kweli ni mpenzi wa Mungu ila sentensi hiyo kumbe haikuwa imemalizika na kusema adui wa dola.
Haya yamedhihirika hasa kwa mwanasheria Tundu Lissu kutufahamisha kuwa ndege yetu ambayo mkulu alitambia sana kisiasa hasa baada ya kuinunua cash imekamatwa na tunadaiwa pesa mingi sana.
Serikali kupitia Zamaradi Kawawa nayo ikakiri kuwa ni kweli ndege imekamatwa, kwa hiyo Lissu hadi hapo ni msemakweli mpenzi wa Mungu. Lakini dola imeonyesha kuwa kusema kweli upenzi wake unaishia hukohuko kwa Mungu kwetu dola ni Adui na lazima ashughulikiwe.
Ni vema mzee akisimama tena jukwaani sasa amalize kabisa hiyo sentensi ili watu wajielewe, 'Msemakweli mpenzi wa Mungu na adui wa dola'.
Haya yamedhihirika hasa kwa mwanasheria Tundu Lissu kutufahamisha kuwa ndege yetu ambayo mkulu alitambia sana kisiasa hasa baada ya kuinunua cash imekamatwa na tunadaiwa pesa mingi sana.
Serikali kupitia Zamaradi Kawawa nayo ikakiri kuwa ni kweli ndege imekamatwa, kwa hiyo Lissu hadi hapo ni msemakweli mpenzi wa Mungu. Lakini dola imeonyesha kuwa kusema kweli upenzi wake unaishia hukohuko kwa Mungu kwetu dola ni Adui na lazima ashughulikiwe.
Ni vema mzee akisimama tena jukwaani sasa amalize kabisa hiyo sentensi ili watu wajielewe, 'Msemakweli mpenzi wa Mungu na adui wa dola'.