Msemaji wa Serikali: Tanzania haijawahi kusema haijawahi kuwa na Virusi vya Corona, hatujadharau chanjo

Charliemic

JF-Expert Member
Feb 17, 2019
585
919
Msemaji wa Tanzania Dkt Hassan Abbas amesema Tanzania inakabiliana na janga la corona kwa kutumia dawa za asili.

DKt Abbas alimwambia mwandishi wa habari wa BBC,Salim Kikeke kuwa Tanzania haitapuuzia chanjo iliyokubalika kimataifa kuwa salama kutumia kama kinga.

Pia Ameeleza kuwa hakuna ambaye ameshawahi kusema Tanzania ni Corona free, kwani Tanzania ni sehemu ya dunia na kila siku inapokea wasafiri!

Amesema nchi ilichokataa ni kuwa sehemu ya majaribio ya chanjo ya UVIKO-19

Chanzo: BBC

======

Msemaji wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas amesema Tanzania haijawahi kusema hilo akifafanua, Tanzania ni sehemu ya dunia na kuna raia wa kigeni wanaokuja Nchini na wapo Watanzania wanaoenda nje hivyo muingiliano upo

Katika mahojiano na BBC, ameeleza Serikali inachosema ni Tanzania imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kudhibiti maambukizi ya COVID19 kwa njia za kisayansi na za asili. Pia, Serikali ilikuwa makini tangu mapema

Aidha, amesema Tanzania haijadharau chanjo za Corona na kufafanua chanjo nyingi zipo katika majaribio, hivyo ni vema zikaendelea kufanyiwa majaribio ili usahihi wake wa kisayansi uweze kuthibitika

Amesema, "Dunia nzima kuna kelele, yapo maeneo hizo Chanjo zimeleta athari kubwa kwenye Afya ya binadamu. Sisi kama Nchi hatuwezi kuwa sehemu ya majaribio"
 
Hawa jamaa hawajawahi kuwa na msimamo kwasababu kila mara wanakurupuka.
Wakubali mkuu anatupeleka chaka.
Amejibu kile mkuu wa nchi alichoagiza. Si kila dawa kutoka kwao ni dawa na inafaa. Wizara iliagizwa ifanya utafiti na kujiridhisha na chanjo hizo.

Kama zingekuwa bora wao wasingekuwa wanaita vyombo vya habari na kuihadaa dunia kuwa wanachanjwa kumbe wanaigiza tu. Amka Afrika, tumia akili yako.

Nakubaliana na wewe kuwa Watanzania hatuko salama kwa COVID19. We have to fight strongly
 
Kilichotakiwa ni kutumia Taasisi makini kwa ajili ya kuifanyia tafiti hiyo dawa watakayopitisha WHO sasa sijui huko mbele watatumia njia gani kuwaambia wananchi wachanjwe hapo Mimi niliona wale mawaziri walienda Madagascar wakinywa hadharani ule uchafu waliodanganywa ni dawa bila hata kuifanyia tafiti ya kutosha.

Hiyo chanjo yanatakiwa majibu ya kitaalamu kutoka kwa wataalamu sio kila mtu analisemea ...
 
F3B7B72F-A5C2-4E93-A763-7FFB6A4303A1.jpeg
 
Kupuuza kudharau au Kudhihaki ni pamoja kutowaelewa wananchi ukweli kwamba wanatakiw kuzingatia kanuni za afya juu ya kujikinga na kudhibiti hii pandemic. Mwendokasi, daladala etc zinajaza kama hali ipo kawaida.... taasisi za serikali hazitoi matamko juu ya uchukuaji tahadhari hasa kwenye maeneo yenye mikusanyiko.

1. Suala la social distance haliongelewi kama kwamba sio msingi wa kuepukana na maambukizi

2. Suala la kuvaa barakoa limekuwa halikubaliki miongoni mwa wanasiasa.
3. Kinachowafanya watoke huko ni vile jamii kuchukua hatua na kutupilia mbali siqsa mbovu zenye lengo la kuwahadaa wananchi juu ya suala la COVID.

Uzuri ni kwamba waathirika wakubwa ni wenye umri mkubwa na wenye magonjwa nyemelezi ambako viongozi walio wengi wa siasa wana fall upon.

Tuendelee kula mtori nyama ziko chini....
 
Ama sie watanzania wa kawaida tuna vicha, wazembe na tusioelewa chochote, au huyu msemaji wa serekali na Serekali ya chama changu wao ndio vichaa, wanafiki na wazembe.

Serekali isiwe na kigeugeu ikubali ilikosea. Mlitutangazia tena na Raisi mwenyewe kuwa baada ya swala za siku 3 , Corona iliondoka kwa mbio za Supersonic Tanzania. Watu walikuwa akivaa barakoa, mlikuwa mnawahujumu.

Ukweli ni kuwa Policy yetu ya Denial imewagharimu sana watanzania wengi, imeuwa watu wengi, na yote hayo ni lawama kwa Raisi wa nchi na Serekali yake. Ingekuwa nchi zingine serekali iliyofanya kosa kama hili, wangejiwajibisha, lakini sisi badala ya kujiwajibisha, mtaanza kututafuta tunaosema ukweli, ili mtuadhibu.

Ushauri wangu kwa serekali yangu na Raisi wangu, ni kweli Tumeuuwa Upinza wa vyama vingi, hauna nguvu tena, ila TUMEJENGA UPINZANI WA NDANI. Its impossible to gag all the people
 
Ama sie watanzania wa kawaida tuna vicha, wazembe na tusioelewa chochote, au huyu msemaji wa serekali na Serekali ya chama changu wao ndio vichaa, wanafiki na wazembe.

Serekali isiwe na kigeugeu ikubali ilikosea. Mlitutangazia tena na Raisi mwenyewe kuwa baada ya swala za siku 3 , Corona iliondoka kwa mbio za Supersonic Tanzania. Watu walikuwa akivaa barakoa, mlikuwa mnawahujumu.
Mkirindi ni wewe kweli au mtu ameiba ID yako? mbona tulihasema kuwa Tanzania hatuna msimamo? Leo wapiga zumari mnageuzwa tena na ni lazima na wewe ugeuke tu
 
Ndugu Q, save this well, very soon itakuja kuisuta nchi yetu.

I challenge next month either jack mack au china government, watatuletea the low quality vaccine za SINOVAC, hali the best ni SINOPHARM, na tutalizimisha watu wapigwe huo uozo wa Sinovac, ambao imefeli vibaya kwenye majaribio ya Brazil.
 
Mkirindi ni wewe kweli au mtu ameiba ID yako? mbona tulihasema kuwa Tanzania hatuna msimamo? Leo wapiga zumari mnageuzwa tena na ni lazima na wewe ugeuke tu
Ndugu ni mimi, na bado ni mwanachama wa kulipia wa CCM. Lakini haimaanishi kuwa ni lazima nikiunge mkono chama changu watendapo vibaya. No no no, nitakemea wakoseapo nitaunga mkono na kusifia wafanyapo vizuri na nitawatetea.

Ubovu wenu ni kuwa mnadhani siasa ni uadui, apana, mbona kwenye issue za Lissu kupigwa Risasi na namna alivyudhulumiwa haki yake niliunga mkono hoja za Lissu, hata michango ya matibabu yake nilichangia.

Ndugu siasa sio uadui, na pia kuna wakati tunawacha siasa za kichama na tunapigania haki zetu kwa pamoja, nchi ni yetu wote, sio ya CCM au Chadema, ni ya wananchi.
 
Msemaji wa serikali akumbushwe tu kuwa rais Mara kadhaa amesema kuwa Hakuna Korona Tanzania. Matokeo yake watu wakaanza kuacha kuchukua tahadhari, na mahali pengine serikali ililazimisha watu wazivue barakoa mfano kwenye hadhara ambazo rais yupo watu walikuwa wanashurutishwa na usalama wazivue hizo barakoa
 
Ndugu ni mimi, na bado ni mwanachama wa kulipia wa CCM. Lakini haimaanishi kuwa ni lazima nikiunge mkono chama changu watendapo vibaya. No no no, nitakemea wakoseapo nitaunga mkono na kusifia wafanyapo vizuri na nitawatetea....
Unamaanisha unachosema? Unaweza kuyasema haya hadharani? Unaweza kuwaambia CCM kuhsu wale makada wa Cahdema waliojazana mahabusu hadi leo kwa kesi za kubumba?

Unaweza kumkemea yule Mbunge wa CCM aliyetumia bunge tukutufu kuwa YUKO TAYARI KUTOA ROHO YA MTU ili kuulinda ubunge wake? Hapa ndio nitaamini siasa sio uadaui ila tusiseme wakati hatuyaishi yale tunayoyasema
 
Msemaji wa serikali akumbushwe tu kuwa rais Mara kadhaa amesema kuwa Hakuna Korona Tanzania. Matokeo yake watu wakaanza kuacha kuchukua tahadhari, na mahali pengine serikali ililazimisha watu wazivue barakoa mfano kwenye hadhara ambazo rais yupo watu walikuwa wanashurutishwa na usalama wazivue hizo barakoa
 
Back
Top Bottom