Msemaji wa Serikali: Malipo ya Trillioni 400+ za kodi, Barrick imekubali kuketi na kamati nyingine ili kujadiliana..

Sio uzalendo katika mambo makubwa na ya kitaifa kuweka ushabiki wa kivyama. Hofu ya Mungu iko wapi katika mchango wako? Kilichojadiliwa bado hakijabadilika; madai yetu ni trilioni 108, tumelipwa 700 bilioni sawa na asilimi 0.65. Tunachokisema hiki tunachokidai tungeweza kukipata bila ya kuwaita washirka wetu "majizi"! Hebu fikiria lugha yetu wakati ule na ya sasa!
Chama chetu sisi tunashangilia kila nchi inapopigwa mkuu.
Ilipokamatwa Bombadier tulisherehekea na vigelegele. Kamanda Tundu Lissu aliitisha waandishi wa habari kwa mbwembwe. Sasa hawa Barricks vipi?
Kwa nini wanatusaliti sisi ambao tunawatetea kiasi hiki?
Yaani wanatulipa wakati sie tulikuwa tukiwapigania watushitaki ili tuwalipe kama wale jamaa wa Bombadier?
Kamanda Lissu akisikia hili anaweza pata vidonda vya tumbo kwa mawazo.
 
Ni bahati mbaya tu hatuna muwakilisha anaeweza kutupa ukweli wa kilichokubaliwa.
Hivi huyu jamaa ka-doctorate chake ni cha wapi? Isije ikawa Lumumba nao wameanza kutoa vi-doctorate vyake. Maana kwa stahili hii ya usemaji inaleta maswali mengi...
 
Swali fikirishi; wenye kampuni yao wamefikia hatua ya kutulipa 300Milioni USD halafu eti kamati ndogo (may be ita involve junior people) ndio waje wakubaliane kulipa matrilioni kweli!? Siamini bado hadi nione.
Nijuavyo mimi kwenye haya makampuni makubwa hua kuna level za ku approve pesa, kiasi Fulani mtu wa level Fulani hufanya hiyo approval and so forth, sasa kamati kubwa ilio involve mwenyekiti na CEO wa Barrick wamefikia hapo how comes kamati ndogo iweze authorize miji pesa mingi!? Inafikirisha though naomba Mungu tufanikiwe.
Well said kk!
 
sasa tena waongee oooo watakimbiya oooohawajikuwekeza .nani kasema? ccm oyeeeeeeee magufuli oyeeeeee majaliwa oyeeee kabudi oyeeeeee
 
Ninyi sio wa kusikilizwa kwa sababu hamna nia njema na nchi. Mnaamini serikali 'ikifeli' ndio mtapata hoja za kusimamia. Sasa yanini kuwasikiliza?

Ona unavyokosa hoja, hayo matrilioni yatalipwa baada ya discussion. Na ni makadirio tu ya kodi kutoka TRA ambayo huenda yakawa ya juu na si ajabu yakapunguzwa baada ya uhakiki na kuwekewa payment schedule.

Kwa mwenendo wenu, naamini hata wakisema watalipa kwa Installment, mtabeza hiyo Installment!

Rudini kwenye mstari, mtasikilizwa!
Hebu tushirikishe vichwa (bongo ) zetu kwenye kujadili mambo.
Tumeanza kwa ukali kudai chetu kutoka wanaotuobia( wezi )
Baada ya miezi takriban mitatu ya mazungumzo na " wezi" tunatoka vifua mbele tunawaambia Watanzania wenzetu tuliowawakilisha kwenye hayo mazungumzo kuwa " wezi " wetu wamekubali kutupatia zawadi
( TOKEN AMOUNT )ya kiasi cha pesa
Halafu wataendelea kujadili walichotuibia baadaye
Tutakapokuwa wabia (PARTNERS)
 
View attachment 613103


"Bosi wa Barrick akiri baada ya makubaliano haya ya awali, kamati nyingine itapitia Matrilioni wanayodaiwa ili walipe"
- Dkt. Abbas, Msemaji wa Serikali.

Tujadili: Zile Dola 300 sio sehemu ya malipo ya deni la kodi? Mbona mijadala mingi huko mtaani inabeza kwamba tumelipwa Bilioni 700 tu katika Trilioni zaidi ya 400 tunazowadai?

Kipi ni kipi?
msemaji wa serikali hajakosea ni ukweli yawezekana TRA wakawemo kwenye majadiliano ndio wanaojuwa jinsi kampuni hii ilivyokwepa kodi kwa hyo lazima kamati nyingine iwepo
 
Prof Kabudi:Tunaendelea kujadiliana kuhusu matrilioni wanayodaiwa Barrick.Tunapitia kila risiti ili tulipwe haki yetu.

Tatizo la baadhi ya wenzetu mnabeza sana. Kwanza mlisema kama nchi tutashitakiwa na kulipa fidia za mabilioni. Sijui tukifeli kama taifa ni hasara kwa nani.. Siasa zisitufanye hivi wajameni!
Miezi mitano yote hiyo nini walikuwa wanajadiliana hadi tuambiwe kuna kamati zingine zitaendelea kuhusu hayo matrilioni ya fedha?! Hapa lazima ufikiri kwa kutumia fikra huru ili kutambua kuwa hayo ni maneno ya kufichia aibu ya kudanga umma kuwa wamekwepa kodi ya kiasi cha trillions 400+
 
Chama chetu sisi tunashangilia kila nchi inapopigwa mkuu.
Ilipokamatwa Bombadier tulisherehekea na vigelegele. Kamanda Tundu Lissu aliitisha waandishi wa habari kwa mbwembwe. Sasa hawa Barricks vipi?
Kwa nini wanatusaliti sisi ambao tunawatetea kiasi hiki?
Yaani wanatulipa wakati sie tulikuwa tukiwapigania watushitaki ili tuwalipe kama wale jamaa wa Bombadier?
Kamanda Lissu akisikia hili anaweza pata vidonda vya tumbo kwa mawazo.
Tuseme yote lakini kwa wakati huu tusimuhusishe Mhe. Tundu Lissu, tumuache apambane na hili lililomkabili hadi atakapopona. Ni ubinadamu tu.
 
Mkuu. Ukiwa. Ni mpingaji wa kila kitu hata fact huwezi. Kuiona. Jana alisema yule mkurugenzi kuwa suala la malipo ya malimbikizo ya kodi litafanyiwa tathmini na kamati nyingine itakayoundwa ndogo ili kupitia nyaraka zote na. Kujua kiasi halisi cha. Malipo. Doma mil 300 inalipwa kama kuonyesha uaminifu. Wa kibiashara na mahusiano mema tukielekea katika hatua kubwa ya kukokotoa deni halisi. Nina. Imani hatuwezi pata. Hizo 400+ lakini pesa ipo, itakuja. Na itakunufaisha hata wewe unaeropoka nyuma ya keypad kwa ushabiki hata kama itakuwa pungufu. Tanzania mpya, inakuja na kwa. Hakika JPM NI JKN WA II.
Miezi yote hiyo kamati ilikuwa inajadiliana kuhusu malipo ya bonus?! Kamati kubwa ineshindwa kujadiliana jambo la msingi kabisa la ukwepaji wa kodi wa matrilioni of money inaishia kujadili kuhusu kulipwa bashishi halafu kamati ndogo ndio ije kujadiliana malipo ya ukwepaji kodi ?! Hii drama imebuma na ndio maana zile reports Lissu aliziita rubbish sababu zilijaa uongo mtupu kuliko uhalisia na Jana ndio imedhihirika hivyo
 
Kilichofanyika safari hii kimefanyika katika tawala zote tena kwa kiasi kikubwa zaidi lakini kikifanyika kwa weledi sana. Lakini safari hii kimefanyika kidogo, bila weledi na kwa kelele nyingi zaidi. Matokeo yake ni kuwa tumepoteza zaidi kuliko tulichopata.

"Kilichofanyika safari hii kimefanyika katika tawala zote tena kwa kiasi kikubwa zaidi lakini kikifanyika kwa weledi sana." unaweza kutupa mifano hai????????.................................................

"Lakini safari hii kimefanyika kidogo, bila weledi na kwa kelele nyingi zaidi. Matokeo yake ni kuwa tumepoteza zaidi kuliko tulichopata."......................................unaposema tumepoteza zaidi unamaanisha nini?? Cost - benefit analysis
 
Watu ni viziwi kiasi chankutosikia alichotamka Rais, boss wa Barrick na Kabudi? Kamati ndogo itakayoundwa itafanya kazi ya kupitia disputes zilizokuwepo ili zifutwe na pia itaangalia namna bora ya kulipa hiyo 300 milioni maana hailipwi kwa mkupuo. Hela hiyo hailipwi kutoka Canada bali itatokana na uzalishaji ina maana serikali nayo itachangia kupitia ile 16% ownership.

Na Rais akasema kuwa sasa hawa ndugu zetu, we are partners, tutafanya kazi pamoja. Mmekwishakubaliana tayari, mnafanya kazi pamoja, mnamiliki kampuni moja, utaendelea kuidai kampuni yenu? Lazima uwe mjinga hasa kuamini kuwa kuna pesa nyingine zaidi ya dola milioni 300 za kulipwa kwa installments.
Kwa hiyo tutakuwa tunawapa Ruzuku Barrick???
 
Angalau wewe unakaribia kuelewa elewa. It was clearly stated that the USD 300m was offered as a token of goodwill to rebuild business trust!
Unafikiri haya majitu hayaelewi mkuu! Yanajitoa fahamu kwa aibu na maneno ya kejeli yaliyotoa awali. Sasa hivi hawana pakuweka sura zao chafu zilizojaa chuki na ukabila. Ndio maana wamekimbilia hiyo bilioni 700 kama hoja yao.
Pathetic!
 
Kila mtu ana eneo lake ambalo ni ana ujuzi nalo, na hauwezi kujua kila kitu Dunia hii, hata A.Einstein ungemwambioa akuelezee mambo ya ustawi wa jamii asingejua pia, kwani yeye aneo lake ni Fizikia na Hisabati, hivyo wakati mwingine tujifunze kusema ,,sifahamu" au hata kukaa kimya tu kuliko kujaza kurasa na kurasa hapa JF kuandika mambo ambayo hakuna chochote unachokielewa, kuna watu hata wamegeuka kuwa ni wasemaji wa Barrick, watu wanabisha hata kile Mkuu wa Barrick mwenyewe alichokimtamka kwa kinywa chake mwenyewe, ...
 
Kabisa Mkuu Serikali hii ya wasema uongo ya hovyo sana. Baada ya miezi mitatu ya kuzungumza huku wakiongozwa na yule professa tuliyeambiwa ni kichwa sana na wametuletea pumba lama zile!

Kweli huyu Kalamaganda Kabugi naye ni professor.......

Ni bahati mbaya tu hatuna muwakilisha anaeweza kutupa ukweli wa kilichokubaliwa.
 
Hiyo 640b nayo imepatikana kwa jasho maana kikaoni watu wetu waligeuka kutafuta huruma ya wa canada eti tutawaambiaje wananchi wetu jamani ikiwa hat senti moja hatupati? Chonde chonde barrick tafadhali mtupunguzie hii aibu angalau na rais apate pa kuanzia kusema sema maroroso yake! Wana barrick: basi isiwe shida tutawazawadia 640 lakini msirudie tena ushamba wenu. Tumefanya hivyo kwa kuwa mmelialia sana ili sizonje wenu asipopolewe mawe na wananchi aliowathibitishia eti oh noah, oh tril. 500. Wazungu wamejionea mibongo tulivyo myeupe pee vichwani!!! Pathetic!!!
 
View attachment 613103


"Bosi wa Barrick akiri baada ya makubaliano haya ya awali, kamati nyingine itapitia Matrilioni wanayodaiwa ili walipe"
- Dkt. Abbas, Msemaji wa Serikali.

Tujadili: Zile Dola 300 sio sehemu ya malipo ya deni la kodi? Mbona mijadala mingi huko mtaani inabeza kwamba tumelipwa Bilioni 700 tu katika Trilioni zaidi ya 400 tunazowadai?

Kipi ni kipi?
Nashindwa kuelewa logic ya Watanzania. Have we really failed to understand that Magufuli has the interest of the nation at heart and that he is completely different from all of our past presidents inspite of the fact that they belong to the same party?Have we also failed to grasp the idea that he was among them and not with them?But exactly what is our problem.Is it intentional deception of the masses?
 
View attachment 613103


"Bosi wa Barrick akiri baada ya makubaliano haya ya awali, kamati nyingine itapitia Matrilioni wanayodaiwa ili walipe"
- Dkt. Abbas, Msemaji wa Serikali.

Tujadili: Zile Dola 300 sio sehemu ya malipo ya deni la kodi? Mbona mijadala mingi huko mtaani inabeza kwamba tumelipwa Bilioni 700 tu katika Trilioni zaidi ya 400 tunazowadai?

Kipi ni kipi?
Fatilia taarifa hiyo kwenye vyombo vya habari utajua mbivu na mbichi,watu wamekariri kwa bahati mbaya au maksudi kuhusiana na hizo dola Mil 300 na kupotosha watu.
 
Back
Top Bottom