Msema kweli mpenzi wa Mungu, Ivori jirekebisheni

Mtyela Kasanda

JF-Expert Member
Oct 13, 2018
554
818
Ivori wana condiments nzuri sana kwa muonekano, na labda zina muonekano mzuri kuliko condiments nyingine zote zinazozalishwa hapa bongo. Lakini bwana zina ladha mbaya, tomato sauce ya ivori ni kama imewekwa vinegar ina uchachu wa ajabu sana. Ukila tomato sauce ya dabaga hutamani kurudia ivori, kuna kauchachu kabaya kwenye ivori kanakufanya ule chipsi kwa shida. Chili nayo hivo hivo, nje ya ukali wa pili pili ambao mashaallah ni kali kweli kweli ila ladha yake mbaya. Hivi mnazalisha bidhaa mbaya ndomana bei zenu ndogo? Kama ni kweli tbs wawashughulikie aisee, bidhaa zenu zipo kila kona na bei ni ya kitanzania ila ladha ni mbayaaaaa kwakweli. Fanyeni tafiti zile ketchup za mbele kule wanafanyaje mpaka utamu unakua vile?
 
Ivori wana condiments nzuri sana kwa muonekano, na labda zina muonekano mzuri kuliko condiments nyingine zote zinazozalishwa hapa bongo. Lakini bwana zina ladha mbaya, tomato sauce ya ivori ni kama imewekwa vinegar ina uchachu wa ajabu sana. Ukila tomato sauce ya dabaga hutamani kurudia ivori, kuna kauchachu kabaya kwenye ivori kanakufanya ule chipsi kwa shida. Chili nayo hivo hivo, nje ya ukali wa pili pili ambao mashaallah ni kali kweli kweli ila ladha yake mbaya. Hivi mnazalisha bidhaa mbaya ndomana bei zenu ndogo? Kama ni kweli tbs wawashughulikie aisee, bidhaa zenu zipo kila kona na bei ni ya kitanzania ila ladha ni mbayaaaaa kwakweli. Fanyeni tafiti zile ketchup za mbele kule wanafanyaje mpaka utamu unakua vile?
Na hata dabaga nao wamechuja kuna kauchachu kwa kweli kiepe hakina raha kabisa
 
Wakiiga ketchup za mbelembele gharama yake pia itakuwa ya mbelembele. Kama wana quality team makini nadhani waatalifanyia kazi swala lako.
 
soko huria,hulazimishwi kununua. Kibaya kwako kizuri kwa mwenzako
Market Saturation, Market Manipulation, Dumping, flooding the market etc, nimesumbuka kupata mbadala wa Ivori, wamefurisha soko na bidhaa zao mbaya.
 
Ivori wako vizuri sana, sijawahi kuona mapungufu makubwa kiasi hicho unacholalamikia. Tomato iko on point kabisa.
 
Mi siiwezi, napenda Redgold japo ni adimu adimu. Ketchup ambazo ni imported pia zinanishida zinanukaje sijui. Zamani kulikuwa na tomato sijui dabaga wale walikuwa wanaweka unga mahindi.
 
... punguzeni kula hayo mavyakula yaliyosindikwa chemicals kibao! Mnajiongezea chances za maradhi bure. Unakuta mtu anakula chips anajaza sijui matomato zaidi ya hizo chips zenyewe.
 
Kwakweli na mimi huwa najiuliza hv wameshindwa kabisa kuiga products kama za American garden? Sio kwa ketchup tu hata Masoseji ya Tanzania hayana kiwango kushinda zile za hata jirani Kenya Mh kawapa chance ya kujitanua kwa kupandisha ushuru kwa bidhaa za nje huu ndio ulikuwa wakati wa kuboresha bidhaa zenu!yaani mnashindwa hata kuchukua sampuli moja mkaiga wenzenu wanavyofanya za kwao kuwa bora?
 
Kuna vitu vingine hata haihitaji ujue ladha yake. Sasa kama pilipili we unataka iwe na ladha gan zaid ya ule mwasho wake tu
 
Ukute ni mwanaume kaanzisha huu Uzi wa chips na tomato sauce

Atakua ni wa Dar tu huyu! wazee wa chips, yai la kisasa, chill na tomato sauce ya ivory! Huku akiteremshia na soda baridiii! Wakati sisi wengine hata hiyo chill ya ivory hatujawahi kuiona.
 
Back
Top Bottom